google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Misukule warudishwa “fresh from Shamba”


Mmoja wa misukule fresh from shamba Mohamedi Mustapha, akioneshwa mbele ya maelfu ya watu na Mchungaji Josephat Gwajima katika ibada ya ijumaa ndani ya nyumba ya ufufuo na uzima.


Takribani wiki mbili zilizpopita Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima wa Kanisa la Glory of Christ (T) Church maarufu kama “nyumba ya Ufufuo na Uzima” aliahidi kuwarudisha na hatimaye kulionesha kanisa misukule wakiwa katika hali yao ya kimsukule akitumia msemo wenye mchanganyiko wa lugha ya kiingereza na Kiswahili “misukule fresh from shamba” ili kuweka msisitizo kuwa misukule hao wamerudishwa kwa nguvu na uweza wa jina la Yesu.
Maelfu ya watu katika nyumba ya Ufufuo na Uzima wakiwa katika bonde la kukata maneno kwa mfululizo wa siku tatu, jumatatu, jumatano na ijumaa za tarehe 8, 10 na 12 mwezi Machi 2010 walipata fursa ya kuwashuhudia misukule waliorudishwa kutoka kwa wachawi waliokuwa wakiwashikilia.
Misukule hao waliokuwa wamekatwa ulimi kipindi walipokuwa msukuleni huku watu wakidhania kuwa hawataweza kuongea tena ila BWANA Yesu aliwaponya na mara baada ya kufanyiwa maombezi misukule hao walianza kuongea na kuelezea kwa kina ni nani aliyewachukua, chakula walichokuwa wakila na mahali walipokuwa wakitumikishwa waliopokuwa misukule. Watu hao waliorudishwa kutoka msukuleni ni pamoja na Jeremiah, Charles Nduru na Mohamedi Mustapha.

Post a Comment

0 Comments