google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Semina Ya Pasaka: Moto wa Ufufuo na Uzima

Ujumbe wa Leo Kwa Ufupi: 6 April 2010

Na Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima
Somo: Roho aliyemfufua Yesu katika wafu
Neno la Msingi: Warumi 8: 11

Warumi 8: 11 imeandikwa “Lakini , ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu”
Katika somo hili Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima anaanza kwa kufundisha akisema……
“……….Tunaanza kusoma mambo kadha wa kadha hapa. Tunajua Yesu alikufa akazikwa, lakini tunaaza kupata picha kwamba kumbe yupo Roho aliyemfufu Yesu katika wafu. Na taarifa zinaendelea kwamba eti, Roho Yule aliyemfufua Yesu katika wafu pia anakaa ndani yetu. Hili ni jambo la ajabu sana kwamba eti Roho aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu………”
“…………………….Tunaanza kupata maswali kadha wa kadha hapa, kwamba kumbe Yesu alipokufa alifufuliwa na Roho wa Mungu. Na huyu Roho aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa pia ndani yetu. Tunapewa majibu kuwa Roho huyu ataifufua na miili yetu iliyo katika hali ya kufa………………..”
Ujumbe huu wa leo tarehe 6 April 2010 unaofundishwa na Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima umewekwa hapa kwa ufupi tu. Na masomo haya yanaendelea katika mfululizo wa Siku zote za semina hii ya Pasaka yenye lengo la kujifunza namna ya kukamata upako au nguvu za Roho Mtakatifu katika Ufufuo na Uzima. Na tunapenda upate nakala yako katika mfumo wa VCD, DVD, AUDIO CD na Kaseti.

Ili kupata ujumbe huu katika VCD, DVD, AUDIO CD, tafadhali wasiliana na Wachungaji wa Media Outreach na Audio Outreach kupitia namba zifuatazo 0713559152 /0716369190 0714117196 /0652033638 /0715808283.

Post a Comment

0 Comments