google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Somo PART TWO: Kulishwa Chakula Ndotoni

Na Mchungaji Kiongozi-Rev. Josephat Gwajima
12 Februari 2012


Nini maana ya kulishwa Chakula ndotoni

Wachawi wapo an wanapenda kazi duniani, mfano kwenye vikao vyao usiku wanajadili mambo ya kuwafanyia watu baada ya mashaka kutumwa.. Duniani wachawi hata kuvaa vizuri ni sababu tosha kukuangamiza na hapo Jina lako linakuwa limes hakuwa kwenye vikao vya kichawi.
Kwenye biblia kuna vyakula vya aina mbili 1 kor 10: 1-3. chakula cha kutoka mbinguni chakula cha roho , Yohana 6 Yesu anasema " Mimi ni chakula kitokacho mbinguni" na chakula cha Kutoka chini, majini. Limetoka kuzimu. Ni muhimu kujua kuna chakula cha kiroho na chakula cha kimwili, chakula cha kutoka mbinguni na chakula cha Kutoka kuzimu.

Kwahiyo wachawi wanapokuwekea shetani wa balaa au wa mikosi ndani yako, Zakaria 3:1 shetani anaweza kukaa ndani ya mtu au karibu na mtu kutokea nje au anaweza ingia ndani... Yaani kupagawa yaani kuwa ( possessed ) na hapo wachawi watakuwa ili kumlisha Yule pepo aliye ndani yako Matendo 13:6-11 kwahiyo utamwona mtu anatafuna usiku ikionyesha kuwa lile pepo liliko ndani linalishwa chakula, ili likue na kupata nguvu zaidi.

Mshetani wapo aina mbalimbali

Majoka - yaliyo Shushwa pamoja na shetani Kutoka mbinguni.
Majini - wanaofuta mila za kiarabu.
Mizimu - mashetani ya ukoo.
Miungu - mfano sehemu nyingi za Asia nk.

Kwahiyo muda wachawi wanamtia nguvu Yule shetani, napo mtu yule ataota anatafuna au analishwa usiku. Watu wa namna hii unakuta tatizo linakua Kila kukicha kwasababu ya hivyo.
Unaweza hisi ni ndoto tu, kumbe rohoni wanakutia udhafu zaidi, ili ushindwe kuendelea... Na hapo tatizo linazidi kuwa kubwa zaidi.
Ndoto inaweza chelewa lakini itatimia....