google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Somo PART ONE: Asali ndani ya Mzoga

Na Mchungaji Kiongozi-Rev Josephat Gwajima
12 Februari 2012-Jumapili


Waamuzi 14:1- 8 Samson alimwuua simba na kwa kawaida katikati ya mzoga mtu angetarajia akute pameoza. Na alitarajia akute hata funza , lakini akakuta Asali ambayo si kawaida kukuta nyuki. Na akachua ile asali ili awape baba na mama yake, ni muhimu kujua kuwa kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafunndisho, kwahiyo andiko hili tunaweza kulilinganisha na andiko lingine...... 2wafalme 4:1- Hii ni habari ya mama mane ambaye alikuwa na made ni, na wadai wake walitaka kuchukua watoto wake wawe watumwa. Basi Yule mama alilia mbele ya mtumishi wa Mungu Elisha .

Jambo tunalojifunza kutoka kwenye Maandiko hayo( Asali ndani ya mzoga )

Baba na mama yake wlimkataza Samson kwenda kwa wafilisti lakini alikwenda na akaua simba na ndani ya mzoga wake alipata asali na akawapa baba na mama yake,
Mzoga ni nini?

Ni hile Hali ya kukukatisha tamaa mfano nchi Kama Tanzania ,inaonekana mizoga tabu, matatizo, migomo nk. Na hapa ni muhimu kujua katikati ya mzoga huo na matatizo itatoka asali ...ni muhimu kujua taifa Kama Marekani lilianza vizuri na Mungu, lakini leo ndio taifa linaloshinikiza ndoa za jinsia moja, nchi kama Uingereza nk. Lakini Africa ilianza kwa tabu, vita, kutomjua Mungu lakini wakwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa kwanza

Ndio maana hata Yesu walimdharau kwa kusema Nazareth anaweza tokea mwokozi , mji unaopuuzwa lakini alipoanza kuishi maisha yake yakabadilika, na sasa amepewa Jina lipitalo majina yote. Na nchi yetu ni vilevile.

Ni muhimu kujua hata maisha yetu yanaweza kuanza katika shida, matatizo, tupo katika shida lakini tunaye Mungu, na Mungu akiwa upande wetu hakuna aliye juu yetu. Kwa hiyo hakuna haja ya kukata tamaa kwa maana katikati ya mzoga itatoka asali, na pia ni muhimu kujua kuwa Samos kabla ya kupata asali alilazimika kumchanachana mwana simba. Na ili kupata asali nzuri je mwana simba ni nini? Mwana simba ni mafisadi, viongozi wabaya, matatizo yaliyopo. Kwahiyo tunatakiwa tuchanechane wana simba ili kupata asali baadaye kwa kutumia mamlaka tuliyonayo ( authority )