google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

UJUMBE: ALITUMWA KUKUTESA

Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima. Jumapili 12.8.2012

MSTARI WA KUKUMBUKA: Mathayo 8:28 “Naye alipofika ng'ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.”

Utangulizi:
Mathayo 8:23-32.. “..Naye alipofika ng'ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile…” habari hii ya kwenye kitabu cha Mathayo, imeandikwa pia na Marko, waandishi hawa ni tofauti lakini habari ni ileile. Kwahiyo kila mmoja ameandika kulingana na alivyoshuhudia tukio lile. Marko 5:1-10’ “Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.” Hii ni kwa mujibu wa Marko, naye ameandika hadi jina la wale mashetani waliokuwa ndani kama Legioni. Tuone Luka 8: 26-36 , Luka anaanza kueleza kuwa Yule mtu ni mwenyeji wa mji ule, Luka 8:31 “Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni.”

LEGIONI (JESHI)
Legioni maana yake ni kundi la wanajeshi zaidi ya elfu kumi, wenye silaha na wanatenda kazi kwa ushirikiano. Nao wanashughuli mbalimbali za kijeshi. Marko 5:9 “Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, a kwa kuwa tu wengi.” Kwahiyo ndani ya Yule mtu kulikuwa na jeshi la mapepo, ndani yake.

MJI WA DEKAPOLIS:
Huu ni mji ulikuwa na miji ndani yake kumi, nah ii ilikuwa Tafsiri yake. Nna hiyo miji kumi kwa ujumla ilikuwa inaitwa Dekapolis. Hii miji ilikuwa na utajili sana, unaweza kujua kama lilikuwa tajiri katika karne ya kwanza, kwa uwepo wa nguruwe ambao hawakuwepo kwa wayahudi. Na kwa kuwa ulikuwa mji wa biashara, watu wengi kutoka sehemu tofauti mbalimbali waliishi pale.

Kulikuwa na njia kuu inayokwenda kwenye hiyo miji, na njia hiyo ilikuwa inapita makaburini. Kama tulivyosoma kwenye kitabu cha MATHAYO, pale njia kulikuwa na watu wawili wana mapepo wakali mno, hata mtu asiweze kupita pale. Yaani lile pepo lilikuwa na uwezo wa kuruhusu mtu kupita au kutokupita.

TAFSIRI YA JAMBO HILI:
Yaani katika huo mji ndio kuna biashara na mafanikio, lakini pepo yupo ndani ya mtu na anaruhusu nani apite na nani asipite. Kama tulivyoona haya mapepo yalikuwa ni jeshi, lenye mbinu za kuzuia watu (legioni) na ndio maana walipomuona Yesu anataka kupita wakajitokeza ili wamzuie asipite.

Na ndio maana unaweza ukajaribu kuomba kazi mahali, ukakuta Yule anayetakiwa kukupa kazi, hatoi kibali sio kwasababu huna vigezo bali ni pepo yuko ndani yake. Anayechagua nani apite na nani asipite. Hili jambo ni bayana kuna mashetani kazi yao ni kukuzuia usiende unapotakiwa kwenda. Na ndio maana unaweza kuona kuwa wale wachungaji wa nguruwe waliruhusiwa kuchunga bila kuwadhuru, lakini Yesu alipoamua kupIta wakaja kumzuia.

VITA YA BAHARINI:
Wakati yesu alipowambia wanafunzi wake waende kwenye mji wa Dekapolisi, jambo la ajabu likatokea baharini. Mashua waliokuwa wamepanda ilitaka kuzama (Marko 4:36-41). Utajiuliza hili jambo ni bahati mbaya, hili halikuwa bahati mbaya ni wale mashetani waliokuwa ndani ya yule yalimuona Yesu akiwa anakuja, hivyo wakamletea dhoruba ili wamuangamizi. Jambo hili linatufundisha kuwa shetani anaye kuzuia yuko tayari kumshambulia mtu anayetaka kukupa msaada.

ALIYETUMWA KUKUTESA:
Utawala wa shetani upo katika ngazi tofauti, yaani kuna shetani wa ngazi tofauti, kuna waliokatika ngazi ya majoka, ambao wao walishuka pamoja na shetani kutoka mbinguni, na wengini ni majini ambao ni mapepo wanaotokana na desturi za kiarabu. Na ndio maana yale mapepo yalimwomba Yesu asiwatoe kutoka katika ule mji. Yaani wametumwa kabisa ili kukutesa.
Haya mateso yalikaa ndani ya wale watu ili kuwatesa katika maeneo tofauti:
>Anakaa uchi:
Na ndio maana waweza kuona mtu anavaa nguo nusu uchi, kumbe ni pepo amewekwa ndani yake, huyu mtu alikuwa uchi makaburini. Mapepo yaweza kumfanya mtu akose maadili. Mtu anabadilika tabia kumbe ni msukumo wa kipepo.
>Anajikatakata kwa mawe
>Hakai nyumbani, anakaa mlimani makaburini.
Na ndio maana unaweza kumwona mtu, hatulii. Kumbe pepo limewekwa ili maisha yasitulie yaani ukipata kazi hudumu kwenye hiyo kazi. Kumbe asilimia kubwa ya matatizo ya ndoa, biashara, masomo na hata magonjwa, yanasababishwa na mapepo yaliyotumwa kukutesa.

Tumia mamlaka ya jina la YESU, kuharibu kazi za aliyetumwa kukutesa, Tumepewa mamlaka dhidi ya mashetani wanakuja kututesa, tumia mamlaka. Kwa jinala Yesu.

UFUFUO NA UZIMA (THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)

TANGANYIKA PACKERS,

KAWE, DAR ES SALAAM.

Post a Comment

0 Comments