google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MIKATABA INAYOTOKANA NA KAFARA Tar. 2.9.2012

Na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima

Utangulizi:
Wakristo wengi huwa hawazungumzii neno kafara kwasababu wanahisi kuwa ni la waganga wa kienyeji, lakini hili neno limeandikwa kwenye biblia mara nyingi sana. Hii ni kuonyesha kuwa  wapo watu wanatoa kafara.

KAFARA KWENYE BIBLIA:
Baada ya Yoshua na wana wa Israeli kuangusha ukuta wa Yeriko, Yoshua aliweka agano kuwa atakayeamua kujenga ukuta ataanza kwa kufiwa na mwanawe wa kwanza na akasema akimaliza atafiwa na mwanae wa pili. Yoshua 6:20-27. Lakini miaka mingi baadaye mtu mmoja akatoa kafara ya wanawe ili aweze kujenga ngome ya Yeriko kwa upya, Kumbe kafara yaweza kutolewa kwa ajili ya kujenga kitu duniani. Imeandikwa katika  1Wafalme 16:38.  

2Wafalme 3:20-27, Hapa tunaona habari ya Huyu Mfalme ambaye baada ya kuona anashindwa vita dhidi ya wana wa Israeli, akaamua kumtoa kafara mwanaye na hilo jambo likawa hasira juu ya Israeli na kashinda vita. Kumbe kafara inaweza ikamwezesha mtu kushinda vita. Ukisoma maandiko haya kwa haraka hutoweza kuelewa lakini ukikaa ukatafakari utaona kuna jambo la muhimu  sana hapo.

Kafara ya mtu kwenye biblia; 2Wafalme17:17,“Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha” kumpitisha mtoto motoni ni kumchoma moto kama kafara yaani ukisoma biblia ya kingereza inatumia neno “sacrifices “ Ezekieli 16:20-21, kumbe jambo la kafara lipo kwenye biblia,na hapa Ezekieli anasema wakawatoa kafara wanao kuwa chakula; na pia neno hili limeoneka na pia katika kitabu cha Ezekieli 20:31-32.

KWELI KUHUSU KAFARA:
Mtoto au mtu akitolewa kafara anakuwa ameuwawa Mwili na kupewa majini au mashetani, katika biblia shetani anayehusika na mambo ya kafara, Mambo ya Walawi 18:21;  ukisoma biblia ya Kiswahili unaweza ukahisi moleki ni mtu lakini tuangalie kwenye biblia ya kingereza “do not give out your children to be sacrifices..” Mambo ya Walawi 20:2 “who sacrifices..  kumbe inawezekana unaumwa na upo kwenye ugonjwa kumbe ndio unatolewa kafara hivyo..

Kumbe sasa waweza  kumwona mtu amekufa na ugonjwa Fulani kumbe ni kafara, mwingine anatoa kafara kwa ajili ya utajiri. Mambo ya Walawi 20:3, pia tunaona kuwa kumbe wachawi hawa wanatoa ndugu na si mtu ambaye hamjui. Yaani kama una ndugu wa karibu au wa mbali ambaye ni mchawi, Yule ndiye anayeweza kukutoa kafara, na kwenye kitabu cha Mambo ya walawi  shetani aliyekuwa anahusika na kafara aliitwa Moleki. Walawi 20:4,5  2Wafalme 20:10

Hayo maandiko ni ya agano la kale lakini pia katika agano jipya jambo hili limetajwa pia; 2Wakorintho 10:20.

KWANINI WATU WANATOA KAFARA:
Ukiangalia habari ya Nuhu baada ya kutoka kwenye safina nuhu alimtolea Mungu sadaka na ile harufu ilipofika kwa Mungu; akasema hatailaani nchi tena kumbe ile harufu ina maana sana kwenye ulimwengu wa roho; vivyo hivyo wanapo mtolea shetani kafara wanalenga kumpa ile harufu na ile harufu inamfanya shetani awa tekelezee wanayohitaji. Mtu anamtoa mwanawe ili kuwapa kafara mashetani, wamtekelezee anacho hitaji kama utajiri n.k.

Mambo ya Walawi 2:12 Vitu hivyo mtavisongeza kwa Bwana kuwa ni malimbuko; lakini visifike juu ya madhabahu kuwa ni harufu ya kupendeza.” Utajiuliza hii harufu na sadaka; hapa ni kafara inayotolewa kwa mashetani. Mambo ya Walawi 3:15, 16, Hesabu 5:17, Sadaka ya vinywaji hii ni baadhi ya mila hapa kwetu ni pale mtu anakunywa pombe alafu anawapulizia watu, hii ndio inaitwa sadaka ya vinywaji inayotolewa. Sasa hii inapotolewa kwa mashetani kwenye ulimwengu wa roho wanakuja mahali pale. Hesabu 15:10; 17:24; 18:7

KUWA MAKINI NA KAFARA ZILIZOTOLEWA KWA MASHETANI:
Kumbe shetani anaweza kutolewa kafaraza aina mbalimbali inaweza kuwa ya vinywaji, uji, nafaka, harufu, watoto au watu wazima; na ni muhimu kuwa makini sana na kuhudhuria sherehe ambazo si za ki Mungu kwasababu waweza kujikuta unashiriki kwenye sadaka hiyo. Kuna watu ambao matatizo yao yamewaanza baada ya kushiriki chakula cha kafara jambo hili biblia imekataza kwasababu ya madhara yake.

Ufunuo 5:8; 8:3 hapa biblia inataja sadaka ya harufu, na ndio maana ukienda kwenye maduka mengi utakuta wameweka vitu vinaitwa ubani; Hii ni sadaka au kafala ya kuteketezwa kwa majini, Isaya 43:23; Yeremia 6:20; 17:26, Ubani na Udi ni sadaka ya kuteketezwa, kimsingi; ile harufu ndiyo inayoifanya iitwe sadaka ya kuteketezwa, kwahiyo mtu unayemuona anachoma ubani ni anakuwa anatoa kafara ya ubani. Nehemia 13:9.. sadaka za unga na sadaka za ubani. Kimsingi watu tuliookolewa hatutoi sadaka za ubani kwasababu biblia inasema maombi ya watakatifu ndio sadaka ya harufu kwa Mungu. (Yohana 19:39)

Kumbe unapoona mahali au duka ukakuta wanachoma udi kimsingi ni kwamba wanaita Mashetani ambayo yanawasaidia kuleta wateja. Na ndio maana maduka mengi yana kuwa na vitu hivi ambavyo ni kafara au sadaka ya harufu; ili majini yaite wateja. Na ndio maana watu wengi wenye majini wanapenda ubani kwasababu kile ndio chakula chao.

KAFARA YA NCHI:
Kuna uwezekano nchi ikawekewa kafara ili wananchi wasiongee, yaani kunakuwa na matatizo katika nchi lakini kumbe ni kwasababu ya kuwaita mashetani ili kufanya wananchi wasidai haki yao. Na ndio maana kuna vitu ambavyo vinapitishwa kwenye nchi ambavyo kwa hakika ni kafara ya harufu kwa shetani. Mambo kama mwenge unaopita ni sadaka kwa mashetani kwa ajili ya nchi, kama unahitaji kujua ukweli wa jambo hili muombe Mungu akuonyeshe; katika ulimwengu wa roho, utajua wazi kuwa ni kafara kabisa kwa ajili ya nchi nzima.

Biblia iko wazi kuhusu kafara inayotolewa kwa ajili ya nchi; Katika biblia Kumbukumbu La Torati 32:43Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake; Kwa maana atatwaa kisasi kwa damu ya watumwa wake, Atawatoza kisasi adui zake,  Tena atafanya kafara kwa nchi yake, na watu wake.” Kumbe kuna uwezakano wa nchi kutolewa kafara yaani mtu anatoa sadaka ili kuita mashetani kwenye nchi. Ni muhimu unapokuwa unaomba uwe unavunja na kusambaratisha kafara zilizo tolewa katika nchi. Nchi ya Tanzania inatakiwa ikombolewe kutoka kwenye kafala.

NGUVU YA KAFARA:
Unaweza ukajiuliza kafara inafanyaje kazi; kimsingi; sadaka au kafara ya vinywaji, damu au vyote tulivyoona ni chakula cha mashetani. Na kimsingi mashetani yapo katika ngazi mbalimbali kuanzia majoka mpaka kwenye majini majini madogo; kwahiyo wachawi au washirikina huita mashetani kulingana na ukubwa wa kafara kama ikitolewa kafara ya kuku anakuja shetani wa ngazi ndogo. Na ikitolewa kafara kubwa kama ya mtu inaliita shetani la ngazi ya juu sana. Hivyo kama mtu hajaokoka ni rahisi kutolewa kafara kwasababu anakuwa hana ulinzi wa Mungu.



UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

Post a Comment

0 Comments