google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

UFUFUO NA UZIMA KUITEKA DAR ES SALAAM KWA MOTO WA MUNGU MWAKA 2013


Na mwandisi wetu.

Sehemu ya Maelfu wa Washirika wa Ufufuo na Uzima
wakiwa Tanganyika Packers ibadani
(Majeshi ya BWANA)
Mwaka mpya wa 2013 Dar es Salaam itatekwa na moto wa Mungu kwa namna isiyo ya kawaida ambapo maelfu na maelfu ya roho za watu zitavunwa kumwelekea Mungu kuliko kipindi kingine chochote katika historia ya moto wa Mungu hapa jijini.

Akitoa sehemu ya salamu za mwaka mpya Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Mch. Josephat Gwajima alisema hayo leo tarehe 29 Disemba 2012 alipokuwa akifundisha kundi kubwa la viongozi wa  wapatao elfu 10,000 wa kanisa hilo lenye washirika zaidi ya 70,000.

Mchungaji kiongozi alisema kuwa ameamua kusitisha mikutano yote ya Injili ya nje ya nchi kwa mwaka 2013 isipokuwa mikutano miwili itakayofanyika China na Marekani. Kanisa la Ufufuo na Uzima lenye makao yake makuu Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam litaanza rasmi mikutano ya injili itakayofanyika nchi nzima kwa mwaka 2013 ambapo maefu ya watu wanatarajiwa kuokoka, kuipa dunia kisogo, kuacha dhambi na kuwa watoto wa Mungu.

Mkutano wa kwanza wa Ufufuo na Uzima unatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Biafra kwa muda wa juma moja mpaka majuma matatu mwaka 2013. Mikutano itakayofuata itafanyika katika wilaya zote za Dar es Salaam katika viwanja vya Mwembe Yanga (Temeke), Biafra (Kinondoni) na Kidongo chekundu (Ilala).

Post a Comment

0 Comments