Na Mwandishi wetu.
Kanisa la Ufufuo na Uzima kama ilivyokawaida yake kila mwanzoni mwa mwaka kubatiza ubatatizo wa Kibiblia wakristo wachanga. Ubatizo wa mwaka huu umefanyika leo tarehe 1 Januari 2013 katika fukwe za Kawe mita chache kutoka lilipo kanisa la Ufufuo na Uzima ambalo Kawe Tanganyika Packers. Ubatizo huo ulianza majira ya saa 6 mchana na kumalizika saa 8.30 mchana.
Wakristo wachanga waliobatizwa ubatizo wa Kiblia wanakadiriwa kuwa zaidi ya 1,000 ambapo Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima aliongoza wachungaji wengine wa kanisa hilo (Resident Pastors) wachungaji wakazi kubatiza watu hao.
Katika habari hii tunakuletea matukio ya Ubatizo katika picha
|
Mchungaji Maximilian Machumu akibatiza |
|
Wachungaji wakiombea maji na kufanya maombi kabla ya kuanza kubatiza |
|
Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima (Kushoto) akishiriki zoezi la Kubatiza |
|
Mchungaji Ernest akibatiza |
|
Wachungaji wasaidizi (MPs, Ministry Pastors) wakijiandaa kushiriki zoezi la Kubatiza |
|
Watu wakijiandaa kubatizwa |
|
Baadhi ya wachungaji wasaidizi wakijiandaa kusaidia katika kubatiza |
0 Comments