google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MATUKIO YA JUMAPILI YA TAR. 17 Feb 2013 KATIKA PICHA

Tarehe 17.02.2013; Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima alifundisha kuhusu Zindiko la nchi (Laana ya Nchi), katika ibada hiyo kulikuwepo pia na aliyekuwa shehe wa kiislamu, aitwaye Omari Mnyeshani. Shehe Omari ambaye alikuwa mmoja wa watu waliozindika nchi alitoa ushuhuda jinsi walivyozindika na mambo waliyofanya katika kuizindika nchi ya Tanzania.

Hapa tunakuletea matukio katika picha ya ibada hiyo.
Watoto wa Showers wakimwimbia BWANA katika ibada ya leo

Platform Choir wakimsifu Mungu, mapema asubuhi ibadani leo

Baba Mchungaji Josephat Gwajima akiwasili ibadani

Platform Choir wakimsifu Mungu ibadi, Mungu hushuka kupitia sifa


Madhabahuni kabla ya Mchungaji kiongozi kuanza kufundisha

Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akifundisha madhabahuni

Sheik Omari akitoa ushuhuda wake alipokuwa akifanya uchawi

Baba Mchungaji akipita katikati ya watu kuwaombea waliokuwa hawewezi na wagonjwa

Mama akieleza juu ya mwanaye mwenye matatizo ambaye alizunguka maeneo mengi bila mafanikio yoyote

Mchungaji Kiongozi akimfungua, aliyekuwa amefungwa na mapepo na nguvu za giza

Mchungaji Kiongozi akipita katikati ya watu na kuwafungua wote waliokuwa hawawezi na waliokuwa katika tabu na mateso mbalimbali.

wakati huo alikuwa akiruhusu maswali kwa mtu mmoja mmoja, na kupitia maswali hayo wengi walifunguliwa.


Mtoto ambaye alikuwa anatokewa na bibi yake usiku na kumpeleka kula nyama na damu za watu, akifunguliwa katika ibada ya jumapili hii

dada ambaye katika familia ya watoto tisa yeye pekee ndiye alikuwa hajafanikiwa na shetani alikuwa amemfunga
alifunguliwa baada ya maombezi

Msichana ana aliyezaliwa huku akiwa analilia jina la bibi yake, walipompa jina akaacha kulia
jambo ambalo limemletea vifungo vingi katika maisha yake.
alifunguliwa baada ya maombezi

Maelfu wa watu waliojitokeza kumpokea Yesu kwa mara ya kwanza kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yao

Moto ulishuka wakati  baba akiwa anawaombea waliokuja kumpokea Yesu

Baba Mchungaji akiwaombea watu waliojitokeza kumpokea Yesu Kristo

Post a Comment

0 Comments