Josephat Gwajima SENIOR PASTOR G.C.T.C |
UTANGULIZI:
Watu wengi wanajiuliza kwanini tunazungumzia uchawi mara
nyingi, hii ni kwasababu shetani hutumia wachawi katika kutenda kazi duniani;
na ndio maana katika Biblia kuna maandiko mengi yanayotaja uchawi na wachawi
kama ifuatavyo:- Hesabu 23:23 24:1; 1Wafalme
9:22; 2Wafalme 17:17; Isaya 47:9,12; Mika 1:12; Nahumu 3:4; Matendo ya Mitume 8:9;
18:11; Wagalatia 5:20; 3:1; Ufu 9:21. Ni kweli tumepewa mambo yote
na Mungu kama vile afya na mafanikio lakini shetani kupitia wachawi amekuwa akizuia, hivyo tunatakiwa kushughulika nao katika ulimwengu wa roho.. Katika sehemu ya
kwanza ya somo hili tuliona kwa habari ya Ayubu ambapo shetani alipata ruhusa
ya kugusa maisha yake. Shetani hakumtokea Ayubu kwa namna ambayo angemfahamu
kuwa ni shetani, lakini alimjia kwa njia ya matukio, kumbe waweza kuwa unapitia
kwenye hali mbaya kumbe ni matukio yanayosababishwa na wachawi.
Wakristo walio wengi wanapambana na shetani bila kujua nguvu
za adui wanae pamaba nae. Nchi ya Japani ilipokuwa haijui kuwa Marekani wana bomu la
nyuklia; waliwachokoza wakidhania kuwa watashinda, Lakini matokeo yake
walishindwa kwasababu walikuwa hawajui nguvu ya wanayeshindana naye. Mara nyingi
watu wengi hupambana na shetani bila kujua nguvu zake na matokeo yake wengi huishia
kushindwa. Huwezi kupambana na adui usiyemjua, vivyohivyo ili uweze kumshinda shetani ni
lazima uanze kwa kutafuta maarifa kuhusu yeye.
MAFURIKO YA KICHAWI:
Ufunuo 12:13-16 Yule Joka alikuwa shetani, Biblia
inasema Yule joka akatoa maji kama mto; kwa kawaida ingeonekana kama mafuriko ya
maji dhidi ya yule mwanamke. Kumbe kuna matukio yanaweza kutokea kwenye maisha
yako au kwenye nchi, na kumbe yamesababishwa na wachawi. Si kila moto au
mafuriko ni ya kiasili, mengi huwa yanasababishwa na shetani ili kuua watu ili
awashushe kuzimu. Kuna matukio yanatokea unadhania kuwa ni ya kawaida kumbe
yameletwa na wachawi ili kuangamiza watu. Ni muhimu kujifunza kuyaangalia
matukio kwa jicho la rohoni.
BIASHARA ZA KICHAWI:
Ezekieli 28:16, 18. “kwa wingi wa uchuuzi wako; watu
walikujaza udhalimu” shetani mfanya biashara naye hutenda kazi pamoja na
wachawi na waganga wa kienyeji. Kwa njia hii shetani anafunga maisha ya watu,
na ndio maana kuna watu wanafanya biashara za kichawi, Yaani wanamwendea
shetani halafu wanamuomba aiwezeshe biashara yao kwa kumpa shetani ama damu au
kafara. Wachawi wanapokuwa wanatoa kafara, huwa wanakuwa wanafanya biashara na
shetani. Ufunuo 18:1- mstari 5” “wafanya biashara wa nchi wamepata mali
kwasababu ya kiburi chake” mstari 11” “nao wafanya biashara wa nchi walia na kuomboleza maana hapana mtu anunuaye
bidhaa zao tena” mstari 13” biashara ya
roho na miili ya wanadamu. Kumbe biashara nyingi unazoona watu wanafanya duniani,
ni biashara za kichawi. Yaani mtu anafanya biashara lakini ndani yake kuna uvuvio
wa kishetani, Nahumu 3:4. Ndio maana biashara za watu wengi hazifanikiwi wakati
huohuo watu wanaomtegemea shetani wanafanikiwa kwa haraka ni kwasababu wameuza
roho zao kwa shetani.
Matendo ya Mitume 16:16-17;
19:24 “aliyewapatia
bwana zake faida nyingi” biashara hizi zipo kabisa, na ndio maana unaweza
kufanya biashara lakini wenzako wanauza zaidi kuliko wewe hata kama wote mnauza
bidhaa ileile, kumbe wenzako wamenuiza ili wao wauze na wewe usiuze. Ni vizuri
kuanza kufanyabiashara na BWANA, yaani kabla ya kuanza biashara ni muhimu
kufanya maombi kwanza ili kuiweka biashara yako katika ulinzi wa Mungu. Unapotaka
kuanza biashara fanya na BWANA.
MAGONJWA YA KISHETANI:
Kuna watu ni wagonjwa sasa kwasababu ya wachawi. Magonjwa mengi
sana husababishwa na wachawi. Unaweza kuwa unasumbuliwa na magonjwa yasiyopona
kwasababu ya chanzo chake ni cha rohoni. Na ndio maana unapooumwa hata kama
utaenda hospitali unatakiwa usiache maombi kwasababu shetani anaweza
kusababisha magonjwa, hata Ayubu aliumwa majipu mabaya ambayo kimsingi
yalisababishwa na shetani.
BIBLIA NA MATUKIO YA
KICHAWI:
Mathayo 9:32 “tazama walimletea mtu bubu mwenye
pepo, na yule pepo alipotolewa alinena” huyu ni mtu ambaye watu walipomuangalia
walimuona ni bubu. Cha ajabu Yesu alipomuona hakushughulika na ububu bali
alishughilika na pepo kuonyesha kwamba ule ububu ulisababishwa na pepo. Kuna mambo
mengi ambayo yanasababishwa na shetani, hivyo unatakiwa kuyashughulikia.
Mathayo 13:10-15 “alikuwa na pepo wa udhaifu kwa muda
wa miaka kumi na nane…” 15” “na huyu
mwanamke aliye uzao wa Ibrahimu ambaye shetani shetani amemfunga” watu
walishamzoea kumwona kuwa ni mama mwenye kibiyongo yaani hawezi kujinyoosha
kabisa lakini Yesu alipomtoa pepo Yule mama alipona.
Wachawi wapo na watu wengi wanalogwa, Kumbukumbu la Torati 18:11; watu wanalogwa na wanalogeka, matatizo
ya watu wengi yanasababishwa na shetani kupitia matukio ya kichawi. Marko 9:17; kuna magonjwa ambayo
yanakuja kwenye maisha ya mtu kwasababu ya kulogwa. Katika utendaji kazi wa
shetani anaweza akaingia ndani ya mtu na kumfunga, lakini pia shetani anaweza
kumkandamiza mtu akiwa nje ya mwili na ndio maana kwa watu waliokoka lakini
hawapigani vita ya rohoni wanaweza kujikuta wanakandamizwa na shetani akiwa nje
yao. 1Wathesalonike 2:18, Paulo
hakuwa amepagawa na pepo lakini shetani alimzuia. Zekaria 3:1. Shetani anaweza
kukuzuia kutokea nje, yaani unahitaji kwenda nje ya nchi lakini shetani
anakuzuia kupitia mtoa pasi ya kusafiria. Matendo
ya Mitume 13:6 hata wachawi hupambana pia ili kukuzuia, ni muhimu kuishi
maisha huku ukijua kunakushindana rohoni.
JINSI YA KUSHINDA DHIDI
YA MATUKIO YA KICHAWI
Mpokee Yesu kwanza; huwezi kushindana na shetani kama hujaokoka,
ni muhimu umpokee Yesu kwanza ili akuwezeshe kupigana katika vita dhidi ya
shetani. Jifunze kuomba mwenyewe; baada ya kuokoka kuna amani ya mwanzo unayoipata
ile isikufanye ukasahau kuwa tupo vitani, kama tulivyoona hapo juu
wanaoshindana nawe wanaweza kuwa ndani yako au nje yako. Katika hali hiyo
unachotakiwa kufanya ni kujifunza kuomba mwenyewe kwasababu hata ukitegemea
kuombewa kila siku, kuna muda utakuwa mwenyewe, na hapo unatakiwa usimame
mwenyewe. Mtu uliyeokoka unatakiwa uhame kwenye ule wokovu wa kuombewa uhamie
kwenye wokovu wa maarifa na kupambana kwa kutumia Jina la Yesu Kristo.
-Josephat Gwajima-
Senior Pastor G.C.T.C
0 Comments