Na Mwandishi wetu. Dar es Salaam.
Jumapili 23th Juni 2013.
Katika jambo ambalo linampatia Mungu utukufu ni mtu mmoja
kuamua kuipa dhambi kisogo na kuamua kuyaachia maisha yake kwa Yesu, kuacha
dhambi na kuanza kuishi maisha matakatifu.Vivyo hivyo kuna furaha mbinguni kwa
mwenye dhambi mmoja atubuye, Luka 15:7.
Hali leo ni tofauti sana katika Nyumba ya Ufufuo na Uzima kwani
shangwe na nderemo mbinguni na duniani ni nyingi zaidi ambapo watu zaidi ya
laki mbili (200,000) wamehudhuria ibada ya Uponyaji.
Katika Ibada ya Uponyaji iliyoongozwa na Mchungaji Kiongozi
Josephat Gwajima, watu zaidi ya 1000
kama wanavyoonekana Pichani) ambao wanatokea katika vitongoji mbali mbali vya
kata na mitaa ya Dar es Salaam wamempa Yesu Maisha yao.
Jambo hili linampatia
Mungu utukufu kwa kundi kubwa kama hili kuamua kuipa dhambi kisogo na kuamua
kumpa Yesu maisha yao ili awe BWANA na mwokozi wa maisha yao na kuungana na
familia ya watu waendao mbinguni.
Jambo hili la kuwaongoza watu wengi kwenda kwa Yesu ni mpango
mahususi wa Yesu kumpokonya shetani watu aliokuwa akiwamiliki muda mrefu kwa
kuwa ukiwa chini ya dhambi unakuwa mateka wa shetani.
Mchungaji kiongozi amesema kuwa hakuna dini “itakayompeleka
mtu Mbinguni isipokuwa Yesu ndiye aliyekufa msalabani kwa ajili ya watu wote,
na kuwa Yesu ndiye njia kweli na Uzima, hakuna aendaye Mbinguni isipokuwa kwa
njia ya Yesu.”
1 Comments
Hakika tunajivunia mungu wa ufufuo na uzima.hakika mungu wa mchungaji Josephat Gwajima yuko hai na anaishi..
ReplyDelete