google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

ALIYEIANGUSHA MELI YA MV SPICE HIGHLANDER AOKOLEWA KUTOKA KWENYE UTUMWA WA SHETANI KWA NGUVU ZA MUNGU KATIKA MKUTANO WA MCH.KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA, JIJINI TANGA.

BINTI AITWAYE THERESIA AMBAYE ALIKUWA ANATUMIKISHWA NA SHETANI AELEZEA JINSI ALIVYOSHIRIKI KATIKA KUIZAMISHA MELI YA MV SPICE HIGHLANDER KWA NJIA ZA KISHETANI.
Theresia akiombewa na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima ili kumuweka huru kutoka katika kifungo cha kumtumikia shetani, pia alikuwa anamatatizo ya miguu na hapa anaombewa kwa jina la Yesu.

Theresia ni binti aishiye Jijini Tanga na Mama yake mzazi, na siku hii ambayo alifunguliwa kutoka kuzimu kwa shetani alikuwa amekuja kwenye Mkutano wa Injili uliokuwa umeandaliwa na Kanisa la Ufufuo na Uzima Jijini Tanga na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima.
Theresia akiwa analia kwa uchungu punde tu..baada ya kutoka kufunguliwa na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akiwa anamuhakikishia kuwa kwa sasa tayari yuko salama na hatochukuliwa tena...kwa maana kwa Yesu ni salam Daima..

Na baada ya Mchungaji Josephat Gwajima kuanza kuwaombea maelfu ya watu ambao walikuwa mkutanoni wengi walifunguliwa, na waliokuwa katika vifungo vya shetani, na  msukuleni walifunguliwa na kurejeshwa katika hali zao za kawaida.


Mchungaji Kiongzoi Josephat Gwajima akiwa na Binti Theresia pamoja na Mama mzazi wa binti Theresia

Theresia akiwa tayari kuanza kuelezea habari nzima..



ALIFIKAJE KUZIMU 
Siku moja nilikuwa nimetumwa dukani na mama yangu mkubwa, wakati navuka barabara ghafula nikakutana na mtu ana kila kiungo katika mwili wale kikiwa kimoja kimoja , akajitambulisha kwa jina la Lucifer akanipa mkono ila nikakataa, akauchukua mkono wangu kwa nguvu akanikumbatia, nikajikuta chini ya bahari. Akaja mwenyewe  nikaogopa sana akaniambia nimekuchagua kwa sababu nimekuchagua hata kabla hujazaliwa. Kwa sababu una akili sana. 
Theresia akiwa anaelezea ushuhuda wa yale aliyaona katika ulimwengu wa kishetani.
Akaniambia nilipozaliwa aliniwinda sana ila alishindwa kunichukua kwa sababu bibi yangu alikuwa ananiombea sana . Lucifer akaniambia anataka niwe mke wa mtoto wake. Tukafunga ndoa  na baada ya miezi 6 baba yake akaniambia anaweza  kunipa nguvu nyingi sana lakini anataka nimtumikie yeye. Baada ya miaka 6 akanipeleka shemu Fulani ndani ya bahari ya pacific lakini ni chini sana, sehemu hiyo ni mji kama ilivyo miji ya huku.
Tukaingia sehemu Fulani tukamkuta dragon ambae alianza kuongea na Lucifer, nikafunga macho na nikajisikia kujawa na  nguvu sana, akaniambia amenipa nguvu na mamlaka ya kumiliki na kutawala fahamu za wanadamu.

Mama mzazi wa Theresia alianza kulia kwa uchungu sana baada ya kunza kusikia habari hizi za kutisha ambazo mwanae wa kuzaa ameyapitia.


Siku moja niliamka asubuhi nikiwa na njaa sana kwa sababu usiku wake sikula chakula, Lucifer akaniambia kuna meli inaitwa Mv spice nikaenda na baadhi ya watu tukatega nyaya za kopa, ile meli ikawa inakuja tukatega pale maji yanapogawanyikia  ili watu waseme ni mkondo wa maji, kuna maneno nikayasema halafu nikasimama pembeni, ile meli ikaanza kuzama mpaka kwenye kina cha chini kabisa cha bahari ambacho nilitaka mimi, kisha  tukaunganisha mabomba mpaka kule pacific na tukapata damu nyingi sana. Mimi nilikuwa nahitaji kunywa damu kiasi cha tani 5000 kwa siku ili niwze kutena kazi kwa nguvu nyingi.

Theresia akiendelea kuelezea huku mama mzazi akiwa anaendela kusikiliza kwa umakini wakiwa na Mchungai Josephat Gwajima

Pia kazi yetu nyingine ilikuwa kuwafanya watu wanaompenda Mungu waache kabisa na kuanza kuwaza vitu vilivyo tofauti kabisa na mapenzi ya Mungu, na waliuwa wakiifanya kazi hii kwa ku-control akili na fikra za wanadamu, yani utawala mkubwa  wa shetani ni kuzishika na kuzikamata fikra za wanadamu ili watende mambo ya kumchukiza Mungu na kujiondolea neema ya Mungu, na walikuwa na uwezo wa kumfanya binadamu atende jambo lolote baya iwe kuuwa,kulewa kutokwenda kanisani.

ULITOKAJE HUKO?
Nakumbuka ilikuwa muda wa kulala huko kuzimu kama kawaida huwa tunalala ila siku hii ikawa tofauti kwa maana nilianza kusikia sauti za watu wanaita njooo njoooo kwa jina la Yesu, mara nikasikia nguvu zinaniishia na nikawa sijielewi kabisa mara nikashanga nimetokea katika viwanja vya tangamano.
Mama yake Theresia anasema kabla ya mtoto wake kurudi alikuwa na matatizo ya kuumwa magojwa yasiyoisha ya kila wakati. Pia alikuwa na tabia ya uvivu na kulala sana , pia hakupenda kusali kabisa, pia kipindi cha mitihani aliugua sana, mama yake Theresia aliongea haya huku akibubujikwa na machozi maana alikuwa hajui kama alikuwa anaishi akiwa na picha picha tu ya mtoto wake na kumbe mtoto halisi alikuwa yuko kuzimu tena ameolewa na shetani na anaifanyia Dunia mambo ya ajabu ya kuiteketeza.
Theresia akimshukuru sana Bwana Yesu kwa kumuokoa na kumrejesha tena katika ulimwengu huu...maana alikiri amekuwa akitafuta ukombozi kwa muda mrefu...

Theresia akiombewa na Mchugaji Kiongozi Josephat Gwajima na Mchungaji Mwandamizi Eng.Yekonia Bihagaze ili kujazwa roho mtakatifu baada ya kuongozwa sala ya toba na kummpokea Yesu kwa Bwana na Mwokozi binafsi wa Maisha yake.

Theresia akiwa amejazwa roho mtakatifu na akinena kwa lugha.
Mchungaji Josephat Gwajima akitoa ufafanuzi.
Shetani anauwezo wa kumuona mtu na maisha yake,vipawa na karama ambazo Mungu amempatia mtu tangu akiwa tumboni mwa mama yake, na ndio maana Theresia alivyofika kuzimu akaambiwa amekuwa akitafutwa siku nyingi sana toka akiwa tumboni ila maombi ya bibi yake yalimkwamisha kuchukuliwa mapema.
Mchungaji Josephat Gwajima akifafanua.
Pia mchungaji Josephat Gwajima aliendelea kuelezea kuhusu kazi hasa aliyoielezea Theresia, Theresia alisema kuwa alikuwa anauwezo wa kuwashikilia fikra, akili na fahamu mwanadamu yeyote..ni hio ndio nguvu hasa ya utawala wa kishetani, kwa lugha nyingine ni typical LUCIFERIC KINGDOM agenda kucheza na mawazo ya wanadamu na kuwapandia mapando ya mawazo ya ajabu ya kutenda dhambi,na ndio roho ya Mpinga Kristo inavyotenda kazi (THE ANTICHRIST)
Mchungaji Josephat Gwajima akiwa anasisitiza kuwa ni lazima kila mtu awe na uwezo wa kuomba na kuishinda roho ya mpinga Kristo na kuushinda ule uwezo wa Shetani wa kumvuvia mtu kufanya maovu, kwa maana shetani ndio anayesababisha mambo yote maovu kufanyika na mwanadamu..

Hapa Mchungaji alikuwa anamaanisha,kwa mfano shetani akiwa anataka kumtumbukiza mtu kwenye ulevu,hawezi akawa anamshushia pombe kutoka mawinguni zimjie alipokaa...bali atamuingizia wazo la kunywa pombe na kumshawishi kuwa anakibali cha kunywa na ndipo mtu mwisho wa siku unamkuta kalala kwenye mitaro kapoteza fahamu kwa ulevi au kafa kabisa...lakini chanzo ni uvuvio wa kishetani kwenye akili ya mwanadamu.

USHAURI ANAOTOA THERESIA KWA WATU WENGINE
Watu inabidi wamtafute Yesu kwa kiwango cha juu sana, kwa sababu yeye ndiye atakayeweza kuwapa kila kitu wanachokihitaji, pia anasema vijana wengi wapo kwenye hatari ya kuangamia hivyo kama hawatamtafuta Mungu hakika wataangamia .

Theresia akiwa anamsifu Mungu kwa Nyimbo kwa maana kuwa kumbe alikuwa anakipaji cha kuimba pia lakini kumbe shetani alikuwa amekifunika.

Pia anamshukuru Mungu kwa kumrudisha kutoka katika vifungo vya shetani maana yeye mwenyewe ilikuwa ni ngumu sana kutoka huko, anachoweza kufanya ni kumtumikia Mungu na kumpenda daima na akaahidi kumuimbia Mungu siku zote kwa kuwa Mungu ndiye mkombozi wake.AMEN 

Post a Comment

0 Comments