google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MISUKULE WAENDELEA KURUDISHWA KATIKA MKUTANO WA UFUFUO NA UZIMA

Ikiwa ni siku ya tatu ya mkutano wa Ufufuo na Uzima mjini Morogoro  maelfu ya watu waliendelea kuhudhuria huku uweza wa Mungu wa namn aya ajabu ukiendelea kudhihirishwa kupitia mchungaji Josephat Gwajima

Mchungaji Josephat Gwajima alifundisha somo la NYOTA YAKO INATUMIWA NA MTU. Akifundisha alisema kila mtu anayo nyota katika maisha yake au kipawa ambacho Mungu ameweka ndani yake ili kupitia hiyo aweze kufanikiwa

Lakini wachawi na waganga wa kienyeji wanakua na uwezo wa kuichukua nyota ya mtu na kuitumia kwaajili ya kazi zao binafsi, akielezea mtu aliyechukuliwa nyota ana dalili zipi, mchungaji Josephat Gwajima alisema unakuta kwa mfano mtoto alikua ana akili darasani lakini  baada ya kuchukuliwa nyota yake unakuta ule uwezo wote unaondoka na anakua hawezi tena kufanya vile vitu alivyokua anafanya mwanzoni.

Baada ya kufundisha mchungaji Josephat gwajima alianza kuomba maombi ya kuwarudishia watu nyota zao na baada ya hapo aliwarudisha wale waliokua wamechukuliwa msukule.
Jina:Rose Mwakipesile
Anaishi mzumbe alichukuliwa na wachawi na wakampeleka kariakoo ambako alikua akitumiwa na wachawi kufanya biashara kariakoo ya nguo na alisikia sauti ikimuita njoo akajikuta yuko mkutanoni

Jina :Esther Anatory
Anaishi Modeko alichukuliwa shimoni na kazi yake ilikua kunyonyesha watoto baharini alisikia sauti inamuita njoo akajikuta yuko mkutanoni

Jina:Flora Mizambwa
Alichukuliwa msukule akawa anakaa msituni alichukuliwa na mwalimu ambae hamjui jina lakini ni mwanaume anaishi mazimbu alikua hali chochote na alisikia sauti inamuita njoo akajikuta yuko mkutanoni

Latifa Jane
Alichukuliwa akakaa polini na alikua analimishwa na wachawi chakula chake ilikua pumba na damu za watu alisikikia anaitwa njoo akajikuta yuko mkutanoni na ameacha watu wengi huko

Jina:Pendo Bahati
Alikua uvunguni alichukuliwa na mama mkwe wa kaka yake, alimkuta shuleni akamchukua, sababu iliyopelekea kumchukua ni kwasababu alikua na akili darasani, yule mchawi alipomchukua akamgeuza mbwa mweusi kichawi na kumpeleka kwao akawa kama ndie yeye hapo nyumbani kwao

Ashura Mohamed
Alichukuliwa akakaa pangoni na alisikia sauti inamuita njoo akajikuta yuko mkutanoni anaishi kirakala


Post a Comment

0 Comments