google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MOROGORO YAZIDI KUTIKISWA KWA UWEZA WA MUNGU
Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima akifundisha aina nne za misukule siku ya pili ya mkutano Morogoro

John Lisu na waimbaji wenzake wakimtukuza Mungu ndani ya Morogoro

John Lisu akiimba wimbo wa Yu hai Jehova

Mchungaji Gwajima akifundihsa neno la Mungu ndani ya Morogoro

Baada ya kufundisha alianza kuomba maombi kwaajili ya kuwarudisha wote waliochukuliwa katika mazingira ya kutatanisha

Sehemu ya umati uliohudhuria mkutano






Ikiwa ni siku ya pili ya mkutano wa kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na mchungaji Josephat Gwajima mjini Morogoro maelfu ya watu wemehudhuria katika viwanja vya shule ya sekondari ya Morogoro kushuhudia mambo ambayo Yesu Kristo akiyafanya kupitia mtumishi wake.

Mkutano huo unaoanza kila siku ya saa tisa jioni ulionekana kuhudhuriwa na maelfu ya watu walioanza kufika uwanjani hapo mapema  ili kushuhudia yale mambo ambayo Mungu anatenda.

Mchungaji Josephat Gwajima aliongozana na waimbaji maarufu kama vile Flora mbasha, John Lisu na wengine wengi ambao walikua wakimtukuza Mungu wakati wa Mkutano.

Mchungaji Gwajima alifundisha somo la aina nne za misukule na baada ya hapo yalifuata maombi ya nguvu ili kuwarudisha watu hao waliokua wamechukuliwa katika mazingira ya kutatanisha.

Hali akiwa amejaa nguvu za Roho mtakatifu aliamuru watu waliokua wamechukuliwa msukule kurudi mara moja ndipo maajabu yalipoanza kutokea na kushuhudia watu ambao hapo kwanza walikua wamepotea na wengine walikufa zamani walipoanza kutokea mahali hapo. Ambao baadhi yao walishuhudia dakika chache baada ya kurudishwa kutoka msukuleni.

Wakazi wa Morogoro walionekana kushangazwa kwa namna ya ajabu jinsi Mungu alivyowafungua watu hao na kuwaweka huru kabisa kwa jina la mpakwa mafuta wake Yesu Kristo.

Uwanja mzima ulisikika kwa sherehe za shangwe huku watu wakimtukuza Mungu kwa matendo yake makuu aliyotatenda siku hiyo

Post a Comment

0 Comments