KUHARIBU MAZAO YA KISHETANI/KICHAWI
PASTOR: JOSEPHAT GWAJIMA
1samweli3:4 basi, wakati
huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.
5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.
6 Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.
7 Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.
9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.
10 Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.
6 Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.
7 Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.
9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.
10 Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
Mungu anamwita samweli mara tatu na sauti ya Mungu inafanana kabisa na Baba
yake wa kiroho Eli na anamwendea mara tatu ndipo Eli alimfundisha jinsi ya
kuitika na akamwambia aseme 'sema Bwana mtumishi wako anakusikia ' na Mungu
anatufundisha kuwa anaweza kututokea na katufundisha jinsi ya mfanop wa Baba wa
kiroho.
Ukiona mtu anafanya vizuri jua kuna nguvu ya kiroho na ukiona anasuasua jua
pia kuna nguvu za kiroho zinazofanya kazi na kukusababisha mambo yakutokee
kimwili.
Mungu tunaye mwabudu anatuponya magonjwa na tabu zote za maisha yetu.na
watu wengi wanapenda kudharau ndoto.
yuda1:1 Yuda, mtumwa wa
Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, kwa hao walioitwa, waliopendwa katika Mungu
Baba, na kuhifadhiwa kwa ajili ya Yesu Kristo.
2 Mwongezewe rehema na amani na upendano.
3 Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.
4 Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.
5 Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasioamini.
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
9 Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.
2 Mwongezewe rehema na amani na upendano.
3 Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.
4 Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.
5 Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasioamini.
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
9 Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.
ufunuo12:9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na
Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake
wakatupwa pamoja naye.
mashetani ni malaika waovu ambao wameshushwa kutoka Mbinguni na kuna
malaika wachafu(wa giza) na malaika wazuri na wanapoitwa malaika wanakuwa na
uwezo wa kubadilisha maumbo, pia utaona kwenye biblia malaika wakaenda sodoma
na gomora na Lutu alikuwa kwenye lindo la mlango siku hiyo na alipo waangalia
akaona sio watu wa kawaida akawabeba akawapeleka mpaka nyumbani kwake na Biblia
inasema wenyeji wa sodoma na gomora wakawaona wale malaika kuwa ni wazuri kwa
maumbo yao wakawataka wawaoe! na hapa tunajifunza kumbe malaika wa aina ya
kijini wanaweza kuvaa maumbo ya kibinadamu na wakaolewa.
kwahiyo anavaa umbo ili awe na mahusihano na wewe na baadaye mkiachana
mkagombana na yeye anabaki ndani yako ni malaika wa giza lakini si mtu na
mnaweza mpaka kuzaa watoto na wanakuwa waluwalu ama ana akili sana ama hana
akili; na ukiangalia majini hawa hata akicheka ndita haitoki usoni kwasababu
asili yake ni kifo ni motoni kwasababu ni (Jini wakala wa shetani).
Si siku zote majini wanaweza wakavaa miili wakaenda kuoa au kuolewa na mtu
lakini wanafanya hivyo kwa mtu aliyeshushwa na Mungu kwasababu ya alicho nacho
kinaweza kuwa ni kusudi la kuwa daktari ama mtumishi wa Mungu ama raisi. na
jini anatumwa aje kuwaingilia katika maisha yao katika kufunga na huyu mtu wa
Mungu ndoa ili ampindishe lile kusudi lake alilowekewa.
Hawa majini ama mashetani wanavaa miili kwasababu wanakuwa wanafahamu watu
waliotumwa na Mungu kuja kufanya kazi ya Bwana ili kuwaharibia kusudi
lililowekwa na Mungu lisitendeke kupitia maisha mikoni yao.
Mungu amekupa safari ya kuanza na kumaliza na utaimaliza kwa maana
imeandikwa "nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu."
Ukiona kila kitu kipo vizuri jua kwamba shetani ni rafiki yako na unahatari
kubwa, kama gari unalotaka unalo, kazi unayoitaka unayo jua unahatari kubwa kwa
maana hakuna mteremko katika wokovu na unatakiwa kupigana. Na shetani hawapendi
watu wa Mungu na huwavuruga na kuwa kwamisha. na hatuna matatizo bali tuna
changamoto na tunatakiwa tupambane kwa silaha tunazojifunza.
kila aliyetoka Mbinguni ana makusudi ya Mungu na hataenda Mbinguni mpaka
kazi aliyotumwa na Mungu ikamilike.kuna vyanzo vya rohonni vinakuzuia usifike
katika kusudi lako sio kwamba huna hela Mungu ameacha mambo hayo yatendeke ili
ujifunze kupigana vita."we have no failure in chrit but it is just a
message that try other way allowed"
Yeremia1:4 Neno la Bwana
lilinijia, kusema,
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.
7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.
8 Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.
9 Ndipo Bwana akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;
10 angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.
7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.
8 Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.
9 Ndipo Bwana akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;
10 angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.
Mungu alikujua tangu tumboni kabla mama na baba yako hawaja
fahamiana.aliandaa kazi yako na majukumu yako yaliandaliwa kabla hujazaliwa na
unapozaliwa shetani kupitia waganga wa kienyeji na wachawi na malaika wake
wanajua amezaliwa Rais ndiyo maana Yesu alipozaliwa mamajusi walitoka
mashariki. na mambo yale ambayo hujawahi kuyaona na kuyawaza na kuyamiliki
ameyaweka kwetu na ametufunulia kwa uweza wa Roho wake kwamaana siku moja Mungu
anaweza kuibadilisha kwa miaka yako 60 uliyo nayo na kubadilishia maisha yako
ukafanya kazi ya miaka elfu moja ukawa tajiri kutoka kwenye ufukara.
kwahiyo shetani akiona huyu dada,mama,mchungaji,binti,baba anakitu kule
mbele cha ajabu tumejaribu kumzuia imeshindikana basi tumtumie mtu atakaye
pindisha kesho yake kutoka kuuzimu na mtu aliyetumwa ayapindishe maisha yako
anaweza kufanya kitu chochote.
kama unakitu cha Mungu utajisikia kawaida wala hutajisikia tofauti yeyote
na unakuwa unaweza kukosea kama binadamu.
Rada na decoda za kishetani zinaweza kurekodi maisha yako na wanaweza kujua
kwenye chuo kikuu cha dar es salaam kuna mtu pale lakini wewe hujijui na
unaweza kuitwa lakini wewe hujijui kama yohana mbatizaji alivyokuwa anabatiza
na kuwaonyesha watu kuwa mwanakondoo wa Mungu akiwa na miaka 30 na wayaudi wa
kawaida wakamwona kijana wa kawaida kutokea nazareti lakini yohana alikuwa
anaona ndani yake kuwa ni Mungu aliye umba mbingu na nchi akawaambia nayeye
anakuja kubatizwa hapa na yohana akamwambia mimi ndio unibatize wewe na Yesu
akawaambia ambatize ili yote yatimie.
Inafika sehemu mtu anapokuwa ana hatima kubwa shetani kuzimu anatumwa kuja
kuipindisha hatima yako na anaweza asiwe mume hata bosi anaweza kutumwa na sio
lazima awe ni jini anaweza akawa mtu anakuja katika maisha yako ili ushindwe
kuifanya hatima yako uliyopewa na Mungu na hata kama amesha kupiga chini simama
na uanze
unachotakiwa ukifanye ili usimame tena na kupigana ni mambo haya yafuatayo:
1 Jaribu na ubaini aliye fanya
maisha yako yaanze kubadilika anaweza akawa mtu ama jini ulipo kuwa na nani au
unafanya nini au kitu ulichokuwa nacho
2 Ubaini yupo wapi huyu mtu na
anafanya nini ili asije akarudi tena anaweza kuwa ni shetani anajua hauja
mfahamu na ukisha mjua unatakiwa uanze kufyeka katika Jina la Yesu; Na kipindi
ambacho unahitaji unatakiwa uwe makini kwasababu unaweza ukaletewa kitu cha
kukuharibia maisha yako na ndio maana hayo maisha yako uliyo nayo sasa
hukutakiwa kuwa hivyo na Mbinguni wanajua wewe ni mkurugenzi,daktari,waziri ila
kuna mashetani ama watu yametumwa kukuzuia.
3 Amua kuacha mara moja na utaachaje unatakiwa umwambie Mungu naomba uniondolee huyu wakala
aliyekuja kwenye maisha yangu"ukisema katika jina la Yesu nakuponda
,nakuvunja,nakufyeka ana fyekwa kwasababu una nguvu ya Jina la Yesu pekee jina
lipotalo majina yote tunaweza kushinda mamlaka za giza kwa jina la Yesu na sio
dhehebu,sio mtu ni jina la Yesu pekee
mathayo10:Akawaita
wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na
kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
Tuna mamlaka ya kumwambia wakala wa shetani yeyote aondoke kwenye maisha
yetu kwa jina la Yesu na inawezekana wale majini wanakaa ndani yako kwahiyo
warudishe waliko toka kwa jina la Yesu.
Unakuta unaanza dalili za kumalizia vibaya unasema ni kusudi la Mungu
ametaka umalizie, si kwamba Mungu ametaka unatakiwa ukatae kwa jina la Yesu na
ukifanya hivyo anaondoka awe ni jini,pepo,shetani,mchawi,mganga,mzimu ama
binadam ametumwa kwenye maisha yako anaondoka
waefeso6:12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na
nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya
majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
4 Uwe tayari kushindana kwa mamlaka ya Jina la Yesu na vita hizi za
mashetani kuwaingilia maisha na kuwa na uhusiano nao yanatokana kwa wale walio
na kitu cha ki Mungu ndani yao na tunashindana
kwa jina na Damu ya Yesu kristo wa Nazareti.
0 Comments