BARAKA KUMI ZA KORESHI
PASTOR JOSEPHAT GWAJIMA
Pastor Josephat Gwajima |
Isaya 45: Haya ndiyo Bwana amwambiayo Koreshi, masihi wake,ambaye nimemshika mkono wake wa kuume,ili kutiisha mataifa mbele yake,name nitalegeza viuno vya wafalme;ili kufungua milango mbele yake,hata malango hayatafungwa.
nimeiumba.
Koreshi ni nani?
Koreshi alikua ni mfalme ambae hakua myahudi na baada ya
wayahudi kuwa wamekaa utumwani siku nyingi yeye aliona ni vema kuwarudisha
nyumbani, baba yake mfalme Nebukadneza aliwachukua utumwani lakini yeye aliona si vema
waendelee kukaa utumwani, akawaruhusu waondoke. Si jambo la kawaida kuwaruhusu watumwa kwenda
nyumbani na kuacha kukutumikia.
Kwahiyo pamoja na kuwa hakua myahudi wala hakua katika agano
la wayahudi lakini Mungu aliamua kumuita Koreshi masihi wake.
Hapa tunaanza kujifunza kumbe yule mtu anayetumiwa na Mungu
na kuwafanya watu kupokea kile walichopoteza , yawezekana walikua na afya
lakini wakapoteza, utajiri, mali au masomo lakini wakavipoteza mtu huyo anaye wasaidia watu wa Mungu
kuvipata walivyopoteza unaweza ukamuita Koreshi na Mungu anamuita masihi wake
na anamstahilisha.
Koreshi alikua ni mfalme wa kawaida na ikafika mahali moyo
wake ukamsukuma awaachie wayahudi waende zao kutoka utumwani, ni kitu kigumu
sana kama ulipigana ukaliteka taifa na kuwafanya watu wa taifa hilo kuwa
watumwa wako. Ilikua ngumu kwa Farao na ni ngumu hata kwa falme nyingine za
dunia yetu ya leo.
Baada ya kitendo hicho Mungu akamuita Koreshi masihi wake au
mpakwa mafuta wake. Sasa mtu yeyote ambaye anafanya kazi kama ya Koreshi zipo baraka za Mungu zinaambatana na yeye na familia yake.
Zipo Baraka kwa mtu wa Mungu ambae amejitolea kuhakikisha
anawaweka huru watu wa Mungu kutoka kwenye shida mbali mbali.
Wakati mwingine mtu anaweza kutafuta njia za kufanikiwa kwa
kutumia nguvu nyingi, lakini mafanikio na Baraka za Mungu zinakuja pale
unapoaamua kujitoa kusaidia wengine na kuwaweka huru.
Kama kuna kitu cha muhimu hapa duniani basi ni mwanadamu, na
kila kitu unachokiona leo ni kwaajili ya mwanadamu, na kila kitu unachokiona
pasipo mwanadamu hakina thamani. Watu wanakua madaktari kwaajili ya wanadamu,
wanakua waandisi kwaajili wa wanadamu, magari, majumba hata spika hazina
thamani bila uwepo wa binadamu.
Jaribu kuwaza leo duniani hakuna mtu spika ni
ya nini?
Kwahiyo watu ni wathamani na ni vizuri kuuthamini utu wa mtu
wakati angali bado anaishi, kwasababu hatuwezi kufanya chochote kwa mtu
anapokufa na ndio sababu unaona mtu anapokufa watu wanatoa hotuba nzuri kwenye
misiba, hotuba inayotolewa msibani hata kama ni nzuri kiasi gani inakua haina
thamani kwa aliyekufa ni kwaajili ya wale waliohudhuria msiba, hii ndio sababu tunatakiwa
kuuthamini utu wa watu wakati bado wako hai.
Jaribu kuwaza mtu alikua na matatizo na yuko nyumbani na
alikua hajawahi kuwaza kwamba masaada wake anaweza kuupata kanisani, na wewe
ulipomualika kuja kanisani mtu huyo anapokea muujiza wake, hakuna jamnbo ambalo
mtu huyo anaweza kukulipa ndio sababu Mungu huwa anayo Baraka maalumu
unapowasaidia wengine na kuwafungua wengine.
BARAKA ZA KORESHI
a) Koreshi ameshikwa mkono wa kuume na Mungu.
Isaya 45:1
Mmoja wa watu waliofunguliwa kutoka katika vifungo vya Ibirisi |
Unaposema mtu ameshikwa mkono na
Mungu inamaanisha huyo mtu hana Baraka zinazotokana nay eye bali zimetoka kwa
Bwana. Kila anachofanya ni Mungu amefanya kila anachogusa ni Mungu amegusa,
akikuonya ni Mungu amekuonya, nguvu za mtu huyo zinakua ni nguvu za Mungu.
Kwa kadiri mtu anavyojihusisha na
kufungua watu ndivyo Mungu anavyojihusisha na kukubariki katika maeneo mabli
mbali.
wakati mwingi inapofika wakati wa
kuwasaidia watu mara nyingi watu wa Mungu wanakuwa wabaguzi, wanachagua wa
kuwasaidia, lakini kama unataka Baraka za Mungu wafanye watu wote kuwa na thamani
sawa, mwenye kazi sawa na asiye na kazi, meneja au asiye na kipato wafanye wote
kuwa sawa, awe ni waziri, mbunge, au mtoto mdogo wote wahudumie sawa.
Na unapokutana na mtu msaidie kana
kwamba utamuhitaji kesho, ongea nao kana kwamba kesho yako inawategemea hao na
kwa kufanya hivyo Mungu anaachilia Baraka zake katika maisha yako.
“Ni maombi yangu Mungu akuishike
kwa mkono wake wa kuume unapowaheshimu na kujihusisha na maisha ya watu wake
kwa jina la Yesu”
b) Ili kutiisha mataifa mbele yake. Isaya 45:1
Jambo hili kwa ulimwengu wetu si
wazi sana, unawaza utayatiishaje mataifa.
Mwanzo 1:26..Akawaambia zaeni
mkaongeke mkaijaze nchi nz kuitiisha.
Kutiisha maana yake kuwafanya
wafuate unachosema, ni mamlaka ya kusema na kikafuata kile ulichokisema na
kutii.
Unapojihusisha na kuwafangu awatu
wa Mungu kuna wakati unapata usumbufu kutoka kwa hao watu kwasababu inahusisha
maisha yao, lakini iko Baraka ya kutiisha mataifa inayotokana na kuwasaidia
watu wa Mungu.
Mungu anakawaida ya kuwageuza watu
wanaomtumikia kutoka kwenye yale maisha ya hali ya chini na ya dharau na
kukugeuza kuwa kitu bora, ubora ule ambao ulikua umefunikwa kutokana na shida
na misongo mbali mbali ya maisha.
Kile ambacho elimu haiwezi kutoa
Mungu anaweza kutoa. Kuna watu ambao wanawaza kuwa hawawezi kufikia mafanikiofulani
katika maisha kutokana na kiwango chao cha elimu walichonacho, lakini ni vizuri
kugundua elimu ni jambo moja na mafanikio ni jambo linguine, yako maarifa ya
kufanikiwa kutoka kwa Mungu, utajiri kutoka kwa Mungu na upenyo utokao kwa
MUngu ndio sababu unaweza ukakuta profesa lakini hajafanikiwa katika maisha
yake.
Ndio sababu ni vizuri kila mtu
akaingia kwenye kazi ya kuwafungua watu wa Mungu, kufungua taifa, kufungua ndoa
zilizofungwa ili Baraka za Koreshi ziambatane na maisha yako kwa Jina la Yesu.
Siku moja nilikua na mkutano
karibu ulaya yote, nikafanikiwa kufika mpaka kisiwa cha PPatmo ndani kabisa.
Nilipofika kule nikakuta watu wa aina yangu hawapo kabisa kule, watu wa kule
wakaanza kushanga mbona hamna watu kama wewe huku, nikawaambia yuuko
aliyenifikisha huku, nyie mmetumia njia zenu za kawaida na utaratibu wa
kibinadamu kufika huku lakini mimi nimekuja kuweka mateka huru, nilijua kuna
magereza ya kiroho, magereza ya magonjwa, magereza ya dhambi na shida na
wanatakiwa kuwekwa huru kwa jina la Yesu.
Kipindi ambapo unaona maisha ni
magumu na huoni pa kwenda fahamu jambo moja, uko ufunguo, neon la Mungu ndio
ufunguo.
Mungu anaweza kuyafanya mambo yote
yaliyoshinmdikana yakawa sawa, Mungu anaweza kuifanya huzuni yako kugeuka na kuwa
furaha, Mungu anaweza kugeuza msiba wako na ukawa shangwe, Mungu anaweza
kugeuza mauti yako na kuwa uzima. IKIWA MUNGU YUKO UPANDE WETU NI NANI ALIYE
JUU YETU?
Iko mamlaka ya ya kawaida ya
kibinadamu na iko mamlaka ya rohoni pia. Na mamlaka ya rohoni iko ya upande wa
Mungu nay a upande wa shetani.
Ndio sababu wako viongozi ambao
wanamtumikia shetani anawapa mamlaka ya kishetani na anaposema jambo kila mtu
analitii hata kama ni jambo baya na anakua hana mtu anayeweza kumjibu.
Na pia kuna mamlaka ya roho upande
wa Mungu ambayo mamlaka hiyo alipewa Adamu, Mungu alimwambia nimekupa mamlaka
utawale vitu vyote, na shetani akaja akamnyang’anya mamlaka hiyo.
Kwakua
Mungu anakua anaishi ndani yetu tunakua na sehemu ya uungu ndani yetu na ile
mamlaka ya kutiisha na kutawala inakua ndani yetu.
mfano
ukichukua jiwe ukalifunga ndani ya gazeti hakulifanyi lisiitwe jiwe au uweza
wake wa kuumiza hautaweza kudhihihika kwasababu tu limefungwa ndani ya
karatasi, hapana. ndivyo ilivyo kwetu Mungu yule aliyeumba mbingu na nchi na
vyote anakaa ndani yetu na uweza wake ule ule uko ndani yetu bila kupungua kwa
namna yoyote.
Adam
baada ya kutenda dhambi ule uweza wake shetani akauchukua na kuanza kuutumia,
ndio sababu Yesu alipokuja akamnyang'anya shetani ule uweza na kulikabidhi
kanisa.
Lakini
leo Yesu anashangaa ametupa nguvu lakini hatujui kama tunazo, ametupa nguvu
lakini hatujui kama tunazo. ndio sababu wakati huu wa mwisho tutaenda kuona
udhihirisho wa nguvu usiokua wa kawaida kwasababu kwanjia ya roho mtakatifu
tataona udhihirisho wa nguvu hizi wa namna isiyokua ya kawaida.
Ndio
sababu baadhi ya watu huwa wanauliza mbona nyie mnaongea kwa kujiamini? ni
kwasababu ule uweza wa kutiisha uko ndani yetu na unatenda kazi kwa jina la
Yesu.
wakati
niko japani niliona maono ya ajabu wakati nimelala usiku.
nilikua
nimelala usiku kitandani ghafla nikajiona nimefika kwenye kikao kimoja kimejaa
wazee wa kijapani, lakini katika maono hayo nikajiona na mimi nimekaa hapo
katika hicho kikao.
wakaaanza
kujadili wakisemezana kuwa Budha ameanza kuishiwa nguvu, wazee wale
wakatengeneza sanamu yenye mfano wa Tembo na wakaanza kuiongelesha kijapani
wanaiambia ile sanamu amka Budha amka utiwe nguvu amka tunataka kushindwa,
ghafla yule mnyama akaamka na akaanza kukimbia kwenye ule uwanja kwa maringo huku
akiruka juu, wale wazee wajapani wakaanza kufurahi na kushangilia maana Budha
ametiwa nguvu.
Gafla
nikajiona nimetokea katika ule uwanja nikamuamuru yule mnyama huku nikisema kwa
jina la Yesu. Yule mnayma aliponiona akaanz akunifuata sehemu nilipokua, wakati
huo mimi nikiendelea kusema kwa jina la Yesu, huku akizidi kuja. Moyoni mwangu
nikasikia sauti inaniambia huyo mnyama anaendelkea kuja kwasababu anajua
akikaribia karibu na kabla kitu chochote hakijatokea wewe utakimbia.
Akanikaribia kabisa nikamshika pembe na kumuamuru kwa jina la Yesu tii, baada
ya kumuamuru atii akageuka n kuwa mwanaume wa kijapani akageuka na kuanza
kukimbia, na mimi nikaanza kumkimbiza, na wale wazee wengine walipoona hivyo
wakaanza kukimbia.
Ndipo
Mungu akaanza kunifundisha kumbe kuna
mapepo ambayo yamepokea kafara na kufikia hatua ya kuwa kama miungu na
kama binadamu, na hao wanatakiwa kutiishwa. na hii ndio baraka aliyopewa
Koreshi ili kutiisha mataifa kwa jina la Yesu
Dada aliyekua hawezi kutembea kabla akifurahi baada ya uponyaji |
ITAENDELEA
2 Comments
mungu yuko upande wako
ReplyDeletegwajima ulipo kuja tanga uli tuponya watu wa tanga
Inapendeza ninapoyaona mambo haya hakika Mungu wetu ni mkuu sana.Inabariki sana.
ReplyDelete