JUMAPILI
YA TAREHE 23/11/2014
SOMO:
MADHABAHU YA LAANA YA KICHAWI
Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima |
Neno mchawi
limeandikwa mara nane kwenye Biblia tena kwa mkazo; neno wachawi limeandikwa
mara ishirini, uchawi mara kumi na nne, uganga mara kumi na nane, waganga mara ishirini
na moja na mapepo mara mia moja na arobaini na moja. Ni muhimu na lazima mambo
haya yahubiriwe ili watu waweze kuyaelewa na waweze kuwa huru.
“Tena mtu mume au mtu
mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa; watawapiga kwa mawe; damu
yao itakuwa juu yao.” Walawi 20:27
Maana ya Laana
Laana ni zaidi ya
kuwa mgonjwa. Ni pale ambapo maisha ya mtu yanakosa muelekeo; kila unalolianza
hulimalizi, ikiwa asubuhi unatamani iwe mchana na mchana unatamani iwe usiku.
Ukiwa huna watoto unawatamani ukiwapata unatamani usingekuwa nao. Hayo ndio
maisha ya laana. Yaliyojaa misukosuko, kukosa amani na furaha kutoweka kabisa.
Laana inaweza kumpata
mtu kutoka kwa mchawi au mshirikina ambaye anakuwa na wivu juu ya maisha yako.
Ni vizuri ujue kuwa katika kila familia lazima kunakuwa na mtu mshirikina au
mchawi. Na siku zote kamba za kufungwa na mtu anayekujua zinatenda kazi vizuri
kuliko kamba za mtu asiyekujua.
Lakini laana pia
yaweza kumpata mtu anapoacha kuisikiliza sauti ya Mungu. Biblia inaeleza kwa
kirefu namna maisha ya mtu mwenye laana yalivyo.
“Lakini itakuwa
usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo
yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi
zote na kukupata. Utalaaniwa
mjini, utalaaniwa na mashambani. Litalaaniwa kapu lako na chombo chako
cha kukandia. Utalaaniwa
uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa
kondoo zako. Utalaaniwa
uingiapo, utalaaniwa na utokapo, Bwana atakuletea laana na mashaka, na
kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea
kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo. Bwana atakuambatanisha na tauni, hata
atakapokwisha kukuondoa katika nchi uingiayo kwa kuimiliki. Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa
homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na
kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie. Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako
zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma. Bwana atafanya mvua ya nchi yako iwe
vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie. Bwana atakufanya
upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia
mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za
duniani. Na
mzoga wako utakuwa chakula cha ndege wote wa angani, na wanyama wote wa
duniani, pasiwe na mtu wa kuwafukuza. Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri, na
kwa bawasiri, na kwa pele, na kwa kujikuna, ambayo hupati kupoa. Bwana atakupiga kwa
wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni; utakwenda kwa kupapasa-papasa mchana,
kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote
utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa. Utaposa mke na mume
mwingine atalala naye; utajenga nyumba usiikae; utapanda mizabibu usitumie
matunda yake. Ng'ombe
wako atachinjwa mbele ya macho yako, usile nyama yake; utanyang'anywa punda
wako mbele ya uso wako kwa jeuri, usirudishiwe; kondoo zako watapewa adui zako,
usipate mtu wa kukuokoa. Wanao na binti zako litapewa taifa
lingine, na macho yako yataangalia, na kuzimia kwa kuwatamani mchana kutwa;
wala hapatakuwa na kitu katika uwezo wa mkono wako. Matunda ya nchi yako, na taabu yako
yote, vitaliwa na taifa usilolijua; utaonewa tu, na kupondwa chini daima; hata uwe mwenye
wazimu kwa yaonwayo na macho yako, utakayoyaona. Bwana atakupiga magoti na miguu kwa
jipu lililo zito, usilopata kupozwa, tokea wayo wa mguu mpaka utosi wa kichwa. Bwana atakupeleka
wewe, na mfalme wako utakayemweka juu yako, kwa taifa usilolijua wewe wala baba
zako; nawe huko utatumikia miungu mingine ya miti na mawe. Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na
dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza Bwana. Mbegu nyingi utazichukua nje shambani,
lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala
hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu. Utakuwa na mizeituni
katika mipaka yako yote usijipake mafuta yake; kwa kuwa mzeituni wako
utapukutika. Utazaa
wana na binti, lakini hawatakuwa wako wewe; kwa sababu watakwenda utumwani. Miti yako yote, na
mazao ya nchi yako, nzige watakuwa nayo. Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu
yako; nawe utazidi kushuka chini. Yeye atakukopesha, wala wewe
usimkopeshe; yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia. Na laana hizi zote zitakujilia juu
yako, zitakuandama na kukupata, hata uangamizwe, kwa kuwa hukuisikiza sauti ya
Bwana, Mungu wako, kushika maagizo yake na amri zake alizokuagiza; nazo zitakuwa juu
yako kwa ishara na ajabu, na juu ya uzao wako milele; kwa kuwa hukumtumikia Bwana, Mungu
wako, kwa furaha na moyo wa kushukuru, kwa ajili ya ule wingi wa vitu vyote; kwa hiyo utawatumikia
adui zako atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na
kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata
atakapokwisha kukuangamiza. Bwana atakuletea taifa juu yako kutoka
mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usilolifahamu ulimi wake;
taifa lenye uso
mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana; naye atakula uzao wa
ng'ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa;
wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng'ombe wako,
wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza. Naye atakuhusuru katika malango yako
yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika
nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila
upande, katika nchi yako yote aliyokupa Bwana, Mungu wako. Nawe utakula uzao wa tumbo lako
mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa Bwana, Mungu wako; katika
mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako. Mtu mume kati yenu aliye mwororo na
laini sana, jicho lake litakuwa ovu juu ya nduguye, na juu ya mke wa kifuani
mwake, na juu ya masalio ya wanawe waliosalia naye; hata asitake wao mmojawapo apewe katika
nyama ya wanawe atakaowala, kwa kuwa hana kitu kilichomsalia kwake; katika
mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika malango yako yote. Mwanamke kati yenu
aliye mwororo na laini, ambaye hangehatirisha kuweka wayo wa mguu wake nchi kwa
umalidadi na ulaini, jicho lake huyu litakuwa ovu juu ya mume wa kifuani mwake,
na juu ya mwanawe, na juu ya binti yake, na juu ya mchanga wake atokaye katikati
ya miguu yake, na juu ya wanawe atakaowazaa; kwa kuwa atawala kwa siri, kwa
uhitaji wa vitu vyote; katika mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako
katika malango yako. Kama
hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu
hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, Bwana Mungu wako;
ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana. Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa. Nanyi mtasalia wachache kwa hesabu, ninyi mliokuwa mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi; kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako. Tena itakuwa, kama vile alivyokuwa akifurahi Bwana juu yenu kwa kuwatendea mema na kuwafanya kuwa wengi, ndivyo atakavyofurahi Bwana juu yenu kwa kuwapoteza na kuwaangamiza; nanyi mtanyakuliwa katika hiyo nchi mwingiayo kuimiliki. Bwana atakutawanya katika mataifa yote, tokea ncha hii ya dunia hata ncha hii ya dunia; nawe huko utatumikia miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako, nayo ni miti na mawe. Wala katika mataifa hayo hutapata raha iwayo yote, wala hutakuwa na kituo cha wayo wa mguu wako; lakini Bwana atakupa huko moyo wa kutetema, na macho ya kuzimia, na roho ya kudhoofika; na uzima wako utakuwa na wasiwasi mbele yako; nawe utakuwa na woga usiku na mchana, wala hutaamini kamwe maisha yako; asubuhi utasema, Laiti ingekuwa jioni! Na jioni utasema, Laiti ingekuwa asubuhi! Kwa kicho cha moyo wako utakavyokucha, na kuona kwa macho yako utakavyoona.” Kumbukumbu 28: 15-67
ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana. Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa. Nanyi mtasalia wachache kwa hesabu, ninyi mliokuwa mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi; kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako. Tena itakuwa, kama vile alivyokuwa akifurahi Bwana juu yenu kwa kuwatendea mema na kuwafanya kuwa wengi, ndivyo atakavyofurahi Bwana juu yenu kwa kuwapoteza na kuwaangamiza; nanyi mtanyakuliwa katika hiyo nchi mwingiayo kuimiliki. Bwana atakutawanya katika mataifa yote, tokea ncha hii ya dunia hata ncha hii ya dunia; nawe huko utatumikia miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako, nayo ni miti na mawe. Wala katika mataifa hayo hutapata raha iwayo yote, wala hutakuwa na kituo cha wayo wa mguu wako; lakini Bwana atakupa huko moyo wa kutetema, na macho ya kuzimia, na roho ya kudhoofika; na uzima wako utakuwa na wasiwasi mbele yako; nawe utakuwa na woga usiku na mchana, wala hutaamini kamwe maisha yako; asubuhi utasema, Laiti ingekuwa jioni! Na jioni utasema, Laiti ingekuwa asubuhi! Kwa kicho cha moyo wako utakavyokucha, na kuona kwa macho yako utakavyoona.” Kumbukumbu 28: 15-67
Unakuta unazaa watoto
hata uwafundishe vipi hawaelewi, umekuwa mtu wa mashaka na kuonewa, kila ukianza
biashara unakuwa unaishia na madeni na kufilisika. Chanzo ni laana hiyo, tauni inayoongelewa
kwenye biblia ni magonjwa kama kifua, mgongo, homa zinakuwa haziishi, bumbuazi
la moyoi unakuwa umeeduwaa tu; unaposa mchumba lakini mwingine anakuja kumwoa, unaanza
mradi haufanikiwi, ngombe wako anachinjwa mbele ya macho yako maana yake
unapigwa roba au kabari na kuibiwa huku unajiona,
Shida hizi zinaweza
kuwa zinakupata na hujui kwa nini au nini chanzo chake. Chanzo cha yote haya
chaweza kuwa ni laana ya wachawi.
Laana ya Kichawi
“Kisha wana wa
Israeli wakasafiri na kupanga katika nchi tambarare za Moabu ng'ambo ya pili ya
Yordani karibu ya Yeriko. Na Balaki mwana wa Sipori akaona mambo
yote ambayo Israeli wamewatendea Waamori. Moabu akawaogopa hao watu sana, kwa
kuwa walikuwa wengi; Moabu akafadhaika kwa sababu ya wana wa Israeli. Moabu akawaambia
wazee wa Midiani, Sasa jeshi hili la watu litaramba vitu vyote vinavyotuzunguka,
kama vile ng'ombe arambavyo majani ya mashamba. Na Balaki, mwana wa Sipori,
alikuwa mfalme wa Moabu zamani zile. Basi akatuma wajumbe kwa Balaamu mwana
wa Beori, hata Pethori, ulio kando ya Mto, mpaka nchi ya wana wa watu wake,
kwenda kumwita, akisema, Tazama, kuna watu waliotoka Misri; tazama, wanaufunika
uso wa nchi, tena wanakaa kunikabili mimi. Basi, njoo wewe, nakusihi unilaanie
watu hawa; maana wana nguvu kunishinda mimi. Labda nitawaweza, tupate kuwapiga,
niwafukuze watoke katika nchi yangu, kwa maana najua ya kuwa yeye umbarikiye
hubarikiwa, na yeye umlaaniye hulaaniwa. Wazee wa Moabu, na wazee wa Midiani,
wakaenda, wakichukua ujira wa uganga mikononi mwao; wakamfikilia Balaamu,
wakamwambia maneno ya Balaki. Akawaambia, Kaeni hapa usiku huu, nami
nitawaletea jawabu kama Bwana atakavyoniambia; wakuu wa Moabu wakakaa na
Balaamu. Mungu
akamjia Balaamu, akasema, Ni watu gani hawa ulio nao pamoja nawe? Balaamu akamwambia
Mungu, Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, amewatuma kwangu, akisema, Tazama, kuna watu
waliotoka Misri, wanaufunika uso wa nchi; basi njoo unilaanie watu hawa; labda
nitaweza kupigana nao, na kuwafukuza.” Hesabu 22:1-11
Kumbe unaweza kuwa
una nguvu ya kumshinda mtu lakini unapolaaniwa unakuwa hauna kitu tena. Unaweza
kuwa una elimu lakini ukilaaniwa elimu yako haiwezi kukusaidia kuishi maisha
mazuri. Wana wa Israeli walisafiri jangwani wakapata njaa Mungu akawapa mana
kutoka mbinguni na mavazi yao hayakuchakaa kwa muda wa mika arobaini , wakapata
kiu mwamba ukatoa maji jangwani, wakaugua naye yule nyoka wa moto akawatokea wakaponywa.
Walipofika kwenye bahari ya Shamu, ikagawnyika wakavuka huku farasi na wapanda
farasi wa majeshi ya Farao akatupwa baharini.
Balaki mwana wa Moabu alipoona wana wa Israeli wanaelekea kwenye nchi yao ya
ahadi akamkodisha mchawi aje kuwalaani. Hata wewe leo wapo kina Balaki wa
maisha yako ambao wameona umepita vikwazo na magumu mengi na sasa unakaribia
kulifikia lile kusudi la Mungu katika maisha yako; wameazimia kuona
unaharibikiwa hivyo wanakulaani kama wachawi au kama sio wanakodisha mchawi
akulaani kwa niaba yao kama Balaki alivyomtumia Balamu kuwalaani wana wa
Israeli..
Kwenye ulimwengu wa
rohoni kuna viashiria vinavyoonyesha mtu atakuwaje siku zijazo na watu ambao
hawakupendi wanapoona unaelekea kwenye mafanikio wanamkodisha mtu mchawi ili
akulaani. Lakini sisi tuliookolewa kwa damu ya mwanakondoo Yesu Kristo tuna
nguvu ya kuwashinda wao maana wao wanategemea hirizi, na kafara zao lakini sisi
tunamtegemea Bwana wa majeshi.
Laana inapotumwa
huruka na kwenda kuingia sehemu husika na inajua ingie kwa nani na isingie kwa
nani.
“Balaamu akamwambia
Balaki, Nijengee hapa madhabahu saba, ukaniandalie hapa ng'ombe waume saba, na
kondoo waume saba. Balaki
akafanya kama Balaamu alivyonena. Balaki na Balaamu wakatoa sadaka, ng'ombe
mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu. Balaamu akamwambia Balaki, Simama
karibu na sadaka yako, nami nitakwenda, labda Bwana atakuja kuonana nami; na lo
lote atakalonionyesha nitakuambia. Akaenda hata mahali peupe juu ya kilima. Mungu akakutana na
Balaamu; naye Balaamu akamwambia, Nimetengeneza madhabahu saba, nami nimetoa
sadaka ng'ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu. Bwana akatia neno
katika kinywa chake Balaamu, akasema, Umrudie Balaki; ukaseme maneno haya. Akarudi kwake, na
tazama, amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, yeye na wakuu wote wa
Moabu pamoja naye. Akatunga
mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka
milima ya mashariki, Njoo! Unilaanie Yakobo, Njoo! Unishutumie Israeli. Nimlaanije, yeye
ambaye Mungu hakumlaani? Nimshutumuje, yeye ambaye Bwana hakumshutumu?” Hesabu 23:
1- 8
Mchawi Balaam alitataka
madhabahu saba ili awalaani wana wa Israeli siku saba za wiki. Laana ya mchawi
haina jumapili wala jumatatu bali ni siku zote. Pia tumeona amewatoa kondoo na
ngombe kama kafara juu ya kila madhabahu. Katika wanyama watolewao kafara juu
ya madhabahu ng’ombe ndiye mkubwa kuliko wote na kondoo mdogo kuliko wote. Hii
inamaanisha kuwa kwenye mambo makubwa wanakulaani na kwenye mambo madogo pia.
Kwa hiyo yule mtu ambaye
hakupendi anamwendea mchawi halafu wanaandaa madhabahu na kuchinja mnyama ili
damu ambayo ni uhai imwagike kwenye madhabahu. Mashetani huja kwenye ile
madhabahu na kunywa ile damu inayomwagika na baadaye huelekezwa kwako ili waje kukuwekea hiyo laana.
“lakini,
kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia,
(Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata
mafumbo ya Mungu. Maana
ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo
ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.”
1 Wakorintho 2:9-11
Yapo mambo makubwa
ambayo Mungu ameandaa kwa ajili ya maisha yako. Pale ulipo leo si kitu kabisa
ipo sehemu njema unayoelekea kesho. Mahali ambapo hutatikisika tena na utasahau
taabu yako. Wewe ambaye ni mbilikimo leo kesho utakuwa baunsa. Mungu tunaye
mtumikia ni Mungu anayejua tutokako na tuendako. Ukikubali kumsikiliza Mungu
hakika atasema na Balaam wa maisha yako kama alivyosema kipindi kile cha wana
wa Israeli; kwamba “huweezi kumlaani aliyebarikiwa.” Kama Mungu ndiye aliyekubariki sio mchawi
wala mshirikina atakayeweza kukulaani. Lakini uwe na baraka kutoka kwa Mungu
ambayo hupatikana kwa kuisikiliza sauti yake. Utakapolaaniwa na Mungu pia,
hakuna atakayekubariki ukabarikiwa.
Balaam Alikuwa ni
Mchawi si Nabii wa Bwana.
Kwa nini mchawi huyu
Balaam anasikia sauti ya Bwana kama sio nabii wa Bwana? Ni kwa sababu mtu anapoingia
kwenye ulimwengu wa rohoni anakuwa anawaona wote Mungu na malaika zake pamoja
na shetani na mapepo yake. Hivyo Mungu aliingilia mawasiliano ya Balaam na
shetani na kumpa maelekezo yake kwa kuwa alikuwa anawalinda wana wa Israeli.
Balaam yeye atakuwa alidhani kuwa Mungu ni ngazi fulani ya juu katika utawala
wa shetani ambao yeye hajafikia.
Baadaye huyu mchawi
Balaam alikuja kufia mikononi mwa wana wa Israeli.
“Balaamu
naye, huyo mwana wa Beori, huyo mchawi, wana wa Israeli walimwua kwa upanga
kati ya hao wengine waliowaua.” Yoshua 13:22
Madhabahu za Laana za
Kichawi.
Wachawi hawawezi
kuloga bila madhabahu. Ili waweze kuyatuma mashetani yafanyike laana kwenye
maisha yako ni lazima madhabahu ijenge kwanza. Kisha lazima kafara itolewe juu
ya madhabahu hiyo ili ule uhai ambao umo katika damu uyahuishe yale mashetani
ambayo hufanyika laana. Pasipo hiyo madhabahu laana haiwezi kufanyika kwako.
Hivyo ni muhimu kuzishughulikia madhabahu zilizoinuliwa ili wewe ulaanike.
Zinapobomoka zile, wewe unarudi kwenye kusudi la Mungu juu ya maisha yako.
UKIRI:
Ninazivunja laana za
wachawi na waganga wa kienyeji kwa damu
ya mwaanakondoo. Madhabahu saba zenye kafara saba zilizo juu yangu
ninazivunja kwa damu ya Yesu. Kuanzia leo kila madhabahu ya kuzimu ya Lucifer, nabii wa uongo ninaifyeka kwa
damu ya Yesu, maaskari wa kishetani ninawafyeka na madhabahu zao kwa jina la
Yesu Kristo. Ninasimama kinyume na kuzimu, ninateketeza nia ya kuzimu kwa jina
la Yesu. Imeandikwa; “laana isiyo na sababu haimpati mtu” Ninaibomoa madhabahu ya kila laana iliyo juu
ya maisha yangu kwa jina la Yesu.
Kwa jina la Yesu
ninabomoa madhabahu za laana za kichawi. Madhabahu za kushindwa, madhabahu za
kuzimu zilizojengwa juu yangu, madhabahu za laana ya ukoo wangu; ninazivunja
kwa jina la Yesu! Ninavaa silaha za vita, ninawafyeka wasimamizi wote wa laana
za kichawi kwa jina la Yesu, ninawateketeza kwa damu ya mwanakondoo. Ewe laana uliy
kwenye maisha yangu ninakufuta kwa jina la Yesu, ninateketeza laana za kishetani
zilizotumwa kwangu na familia yangu kwa damu ya Yesu. Ninazivunja laana zote za
kishetani zilizotumwa kwangu kwa jina la Yesu.
Ewe laana ya nchi
uliyoishikilia nchi yangu ninakuamuru achia nchi yangu kwa jina la Yesu. Madhabahu
za laana ya kushindwa, laana ya kukataliwa, laana ya kukosa mke/mume; ninaibomoa kwa jina la Yesu. Ninazibomoa
madhabahu zote za kichawi kwa jina la Yesu. Madhabahu za laana juu ya familia
yangu ninazivunja kwa damu ya mwanakondoo. Kwa jina la Yesu ninavunja laana juu
ya ndoa yangu kwa, ninavunja laana juu ya masomo yangu, ninazivunja madhabahu
za kishetani zilizoshikilia laana juu ya biashara yangu kwa jina la Yesu. Kwa damu
ya mwanakondoo, maneno ya laana yaliyotamka na wanadamu juu yangu na familia
yangu ninayavunja kwa jina la Yesu. Imeandikwa; “ni nani asemaye neno ikiwa Bwana
hakuliagiza likatendeka?” Hii laana haijaagizwa na Bwana,
ninaibatilisha kwa damu ya mwanakondoo.
Ninawateketeza majini
na mashetani wote mlioshikilia laana juu ya nchi na familia yangu kwa jina la
Yesu. Ninavunja laana za majeshi ya pepo wabaya kwenye maisha yangu kwa jina la
Yesu. Ninavunja madhabahu za wachawi zilizomwagiwa damu ya kafara inenayo laana
juu ya maisha yangu; ninazivunja kwa damu ya mwanakondoo, katika jina la Yesu Kristo.
AMEN!
0 Comments