google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUNA MTU NYUMA YA TATIZO LAKO

JUMAPILI, 23.08.2020
BISHOP DR. JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: KUNA NGUVU NYUMA YA TATIZO LAKO

Dunia yote inafahamu kuwa matatizo ni asili, tatizo unaloliona kuna nguvu nyuma yake unapo kuwa unaishi kuna nguvu inang’ang’ana kukuongoza katika vitu unavyo vifanya. Kila mtu unaemuona duniani anawakilisha nguvu fulani ya ki Roho au ya shetani kila mtu unamuona anatembea kuna mamlaka nyuma yake inayo msukuma kufanya jambo fulani au mambo fulani ukimuona mtu amesima ujue kunanguvu iliyo msimamisha ikiwa nguvu ya Mungu itamuongoza katika njiailiyo sahihi kuipita lakini kama ni nguvu ya kishetani ipo nyuma yake basi itamshusha chini

Kuna watu wamepewa macho yakuona biashara na macho yakuona nguvu iliyo nyuma ya biashara kuna watu wanajua umekiribia kupata lakini kuna watu wakaanza kukutumia vitu vya kukukwamisha. Mungu anaweza kukuvusha katika matatizo yako yote unayo pita mchawi ukimtambua hana uwezo tena wakukumaliza wala kukujalibu.

Biblia inasema mtu mwenye akili nyingi ndio mtawala shetani anapenda  mtu anayesema hakuna uchawi iliapate kumroga vizuri,  wachawi wakiona jambo limenyooka wanataka kulipindisha, mafanikio ya mtu haya andaliwi na urefu wa mtu au ufupi wa mtu. Kuna watu walijenga  vibanda  ili waanze biashara lakini hawakufanikiwa na wao wakaona  kama ni kitu cha kawaida ulianza kwa huzuni utamaliza kwa heshima kuliko ndugu zako wote. kuna mambo mengine mtu anayaona ya kawaida  lakini mtu mwingine kwake haoni kama ni mambo ya kawaida.

Matatizo hayaja ruhusiwa na Mungu ili ya kumalize ila matatizo ya ruhusiwa na Mungu ili ya kunoe kwaajili ya kesho yako. Dunia haikupi kile unacho kitaka ila inakupa kile unacho kipigania, Mungu anajua kile unachotaka lakini hawezi kukupa mpaka useme. Kuanguka kupo lakini tatizo ni kubaki pale ulipo angukia ukianguka simama upambane kupiga hatua nyingine .Vita ya maisha lazima upigane hadi  mwisho Mungu anaweza kukutoa chini na  kukuweka juu lipo jambo Mungu anakuwekea ili uje kulitenda shetani alikuwa mpendwa wa Mungu kila mtu aliye kusaliti atapigwa mpaka pande za mwisho kuzimu kama alivyo pigwa shetani mpaka pande za mwisho kuzimu  sio kila wanaoitwa na Mungu hawana makosa Mungu awapa sifa wale wasiokuwa na sifa.

 KANUNI YA USALITI:

1/ Kila unalolipanga kwaajili ya mtu unajipangia mwenyewe

2/ Wasaliti hufa wao kabla ya kukuuwa wewe

3/ Kila unayemuonea wivu unamkatia leseni ya kwenda juu, wivu ni namna ya ndani ya ukili

4/ Kila wenye wivu uishi muda mfupi

Huwezi kusikia kama unausaliti au  wivu ndani yako maana maumivu yanaweza kugeuka  kuwa majeraha ndani yako kila mtu aliye na maumivu hawezi kuishi muda mrefu nyuma ya unaye mpenda kun amipango ya kukuteketeza.

1 Samweli 18:20-27

 “Walakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi; watu wakamwambia Sauli, na neno hilo likampendeza. Naye Sauli akasema moyoni, Mimi nitamwoza huyu, awe mtego kwake, tena kwamba mkono wa Wafilisti uwe juu yake. Basi Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, Leo utakuwa mkwe wangu. Naye Sauli akawaagiza watumishi wake, Zungumzeni na Daudi kwa siri, na kusema, Angalia, mfalme anakuridhia, na watumishi wake wote wanakupenda; haya basi! Na uwe mkwewe mfalme. Nao watumishi wa Sauli wakanena maneno hayo masikioni mwa Daudi. Daudi akasema, Je! Ninyi mwaona kuwa ni shani mimi kuwa mkwewe mfalme, nami ni maskini, tena sina cheo? Na hao watumishi wa Sauli wakampasha habari, wakisema, Ndivyo hivyo alivyosema Daudi. Naye Sauli akasema, Mwambieni Daudi hivi, Mfalme hataki mahari yo yote, ila anataka govi mia za Wafilisti, ili ajilipize kisasi adui za mfalme. Basi Sauli alidhani kumwangamiza Daudi kwa mkono wa Wafilisti. Na watumishi wake walipomwambia Daudi; maneno hayo, ilimpendeza Daudi sana kuwa mkwewe mfalme. Na siku zilikuwa hazijaisha bado; basi Daudi akainuka, akaenda yeye na watu wake, akaua katika Wafilisti watu mia mbili; na Daudi akazileta govi zao, wakampa mfalme hesabu kamili, ili awe mkwewe mfalme. Naye Sauli akamwoza Mikali, binti yake.”

Kuna watu wanatakiwa kufika mahali pazuri lakini wanakutana na miiba njiani kila njia unapita hata kama kuna magumu kiasi gani simama  chomoa  mwiba ili ufikie mafanikio yako,  Mafanikio hayaletwi kwenye sahani ya fedha ukitaka kuwapeleka watu mahali lazima uwe na ujasiri vitu huja kwa kusema unaposema wewe ni tajiri kweli utakuwa tajiri hatatokea mtu kukupenda mpaka kufa. Kuna wanaume hawawezi kuondoka kwao mpaka wagombane. Usijaribu kushindana na mtu maana kila nyuma ya mtu kuna nguvu inayo mlinda usijaribu kumtoa mtu mahali alipo kuwa maana ujui nani kamuweka hapo alipo yupo shetani anaye kufatilia ili ushindwe katika mambo unayoyafanya.


BONYEZA HAPA👇👇 KUANGALIA IBAADA NZIMA YA JUMAPILI


BONYEZA LINK HAPA CHINI ðŸ‘‡ðŸ‘‡ KUSIKILIZA LIVE IBAADA ZETU

UFUFUONAUZIMA RADIO is on Mixlr https://mixlr.com/ufufuonauzima-radio

Post a Comment

0 Comments