google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

UJUMBE: UFALME WA MAJINI

Na Mch. Josephat Gwajima | GCTC; Dar es Salaam, Kawe. 01.09.2013

Mchungaji Kiongozi, Ufufuo na Uzima; Josephat Gwajima
UTANGULIZI:
Kwa kichwa cha somo hili, utakuwa umejiuliza maswali kuwa “namaanisha ufalme wa kwenye maji au namaanisha ufalme wa majini au pepo wachafu” lakini vyovyote vile utakavyotafsiri katika maana hizo mbili utakuwa upo sahihi kwa ujumbe huu.

Ufunuo 2:12-13 “..napajua ukaapo ndipo katika kiti cha enzi cha shetani…” ni muhimu kujua kuwa, huwezi kumshinda adui bila kujua mbinu na silaha zake anazozitumia. Maombi ya wakristo wengi yamejikita katika kujilinda dhidi ya shetani (Defensive Prayer) lakini kama unataka kumshinda shetani unatakiwa uwe na maombi ya kumshambilia (Offensive Prayers) na kuwa huwezi kumshinda adui bila kujua mbinu zake, ndio maana tunajifunza kuhusu ufalme wake.

MAANA YA AKAAPO SHETANI:
Kwa kawaida utawala wa shetani duniani, umeweka himaya yake katika maeneo tofauti tofauti, na ndio maana katika kila mkoa au wilaya kuna mtu au eneo ambalo linaogopewa na watu. Katika maeneo mengi utakuta mtu ambaye ama kwa nguvu zake za rohoni au mwilini amekuwa akiogopwa na watu. Mtu huyo au mahali hapo ndipo panaitwa pale akaapo shetani. Maeneo mengi ya vijijini huwa kunakuwa na mtu anayeogopewa na mara nyingi husababishwa na uchawi wake; mtu huyo ndiye anayeitwa kiti cha enzi cha shetani katika kijiji hiko.

Ili kuweza kuitawala dunia, shetani ameweka tawala zake sehemu tofauti; maeneo hayo sio kuzimu yenyewe bali ni ngome ya shetani katika eneo husika. Kimsingi, hata katika maisha, kazi, masomo au biashara za watu kuna maeneo ambayo shetani anakaa; hapo panaitwa kiti cha enzi cha shetani katika biashara, nyumba au katika mwili.

NENO MAJINI KATIKA BIBLIA:
Mambo ya walawi 17:7, ukiangalia kibiblia neno hili “Jini” kwa lugha ya kingeleza limetajwa kama “goat idols” Kimsingi katika agano la kale kulikuwa na aina nyingi za miungu; na mojawapo alikuwa mungu mbuzi-dume. Na ndio maana katika biblia wakristo hawafananishwi na mbuzi bali kondoo kwasababu mbuzi dume alikuwa moja ya miungu iliyokuwa inaabudiwa kama mashetani. 2Mambo ya Nyakati 11:15, hapa pia wanatajwa aina hiyo ya mashetani waliokuwa wanakaa ndani ya miungu-mbuzi “goat idols” Miungu mbuzi ilikuwa ni mashetani waliokuwa wakiabudiwa na watu katika agano la kale ambao kwasasa ndio walewale wanaofahamika kama majini.

UNDANI KUHUSU MAJINI:
Majini ni mashetani ambao wanafuatana na tamaduni za nchi za kiarabu, lakini pia, majini haya yalikuwa ni mashetani yanayofuatana na maji au mikusanyiko ya maji; kwasababu makao yao makuu yalikuwa majini ukisoma, Ezekieli 29:3-5. Na ndio maana mfalme wa Misri, Farao alikuwa anakwenda kuabudu katika maji, Ukisoma, Ezekieli 32:2-3 inaeleza jinsi Farao alivyotegemea miungu ya katika maji kiasi biblia inamwita joka wa majini.

Kwasababu ya mashetani hao wanaokaa majini, mara nyingi maji katika biblia yamekuwa yakitumika kuonyesha uharibifu, Zaburi 18:16. Ndio maana hata kipindi cha Musa alipokuwa anamfuata Farao ili kuomba ruhusa ya kutoka utumwani, maranyingi, alikuwa akimkuta anatoka au anakwenda majini, Kutoka 7:18; 8:20; Ilikuwa ni desturi ya farao kwenda kuabudu katika mikusanyiko ya maji. Maandiko yameonyesha sana kuhusu mashetani wa baharini, katika Ufunuo 14:31; 20:13, Isaya 27:1, Ayubu 3:8.

Ufunuo 12:1-16; Joka jekundu ni ishara ya shetani. Kama nilivyosema mwanzoni, majini ni mashetani yanayofuatana na desturi za kiarabu, na yanaitwa majini kwasababu yanatokea katika maji. Mashetani haya ndiyo ambayo yalikuwa yakiabudiwa na Mfalme wa Misri, Farao na ndio maana katika maeneo ambayo yametawaliwa sana na waarabu lazima utakuta kuna aina hii ya mashetani. Na mashambulizi mengi ya rohoni huanzia kwa majini hawa.

Hili ni kundi la mashetani, wanaofanya kazi zao ndani ya maji; pia, majini haya yanauwezo wa kukaa nchi kavu na kuishi kama watu, wakaongea na kupanda gari kama watu. Ndio maana matatizo yote ya rohoni katika maeneo ya pwani husababishwa na majini, kuanzia katika tawala za kiserikali mpaka katika nyumba za mtu mmoja mmoja. Asilimia kubwa ya matatizo ya watu yamesababishwa na majini, ambao hutenda kazi kumwakilisha shetani mahali husika. Majini ni aina ya mashetani yanayotumiwa kuvuruga makanisa, kuleta visasi, kufanya watu kuwa wazinzi, kuharibu amani, kuleta kutokuamini (ukiondoa majini kuna baadhi ya dini zinakufa) na magonjwa yote; kazi hizi zote hufanywa na majini.

DALILI ZA UWEPO WA MAJINI KATIKA MAISHA YA WATU:
  • Dalili zifuatazo ni za mtu ambaye ama ana majini au anafuatiliwa na majini:-
  • Unakuwa unaota ndoto upo ndani ya maji; ama unatembea ndani ya maji, unaingia majini au unatembea juu ya maji.
  • kila wakati unajikuta umeona au umeokota pete za dhahabu; mara nyingi majini wanaotaka kukutana kimwili na wanadamu hutegesha mikufu au pete ili kuunganishwa naye.
  • Mara nyingi unapotembea unakuwa unasikia harufu ya udi, ubani au marashi. Si lazima majini hayo yawe ndani yako lakini yanaweza kuwa yanakufuatilia ili kukudhuru.
  • Wakati wa usiku unasikia vitu vimepigwa kwenye bati au darini bila kujua chanzo na mwisho wake.
  • Kudondoka chooni ni dalili nyingine ya mtu anayefuatiliwa na majini.
  • Wewe ni mkristo lakini ukisikia adhana unajisikia kuipenda; na ndio maana watu wengi wakija kuombewa wanalipuka mapepo yanayopiga adhana.
  • Kukonda kupita kiasi.
  • Kupenda kuvaa nguo za nusu uchi.
2 Wathesalonike 2:8, alisema Mtume Paulo alikua amepakwa mafuta na Mungu kutenda mambo makubwa lakini pamoja na hayo shetani aliweza kumzuia kwenda Thesalonike kuifanya kazi ya Bwana. kumbe kupitia majini shetani aweza kutenda kazi ama ndani au nje ya watu ili kufanikisha azma yake ya kutesa maisha ya watu.


USHINDI DHIDI YA MAJINI:
Ili kupashinda na kupaondoa pale akaapo shetani ni lazima kuwashambulia majini ambao ndio wanaotenda kazi katika maisha ya watu. Huwezi kutatua tatizo bila kushughulika na chanzo chake, na kama tulivyoona hapo juu kuwa majini ndio wanaosababisha matatizo ya watu wengi, hivyo ukishambulia majini kwa Jina la Yesu Kristo unajiondoa mwenyewe katika tatizo ambalo limeletwa na shetani katika maisha yako.


Ukiokoka unapokea mamlaka ya kuteketeza kazi za shetani, tumia mamlaka hiyo kuharibu kazi zote za majini katika maisha yako.

For More Information Visit Our Facebook Page

Post a Comment

1 Comments

  1. UTAJIRI AU FEDHA ZA NDAGU AU MAJINI KWA MUDA MFUPI

    (Kwanza kabisa nataka kukwambia kwamba hakika utajili ni azina kutoka kwa mwenyezi mungu na pia kuna viumbe alio wapa mamlaka na nguvu ya kumiliki mali)


    MPAKA MASAA 72(SIKU3) PAPO HAPO KWA MASHARTI MAALUM KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

    KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA

    kwa maelezo kamili piga namba +255742162843

    (KWANINI USUMBUKE,HACHA KUTANGATANGA, NA MAISHA NI MAFUPI PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI (Tumia ufahamu kujinasuaUTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

    NAITWA DR, MDIRO piga 0742162843. KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU ULINZI KWA MALI YAKO
    (HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)
    MATIBABU MENGINEYO NI KAMA UTULIVU KATIKA NDOA, AU KUMVUTA UMPENDAE, KUONDOA MIKOSI, MABALAA, KUOSHA NYOTA, KUITAMBUA NYOTA YAKO NA ASILI YA KAZI YAKE, KAMA UNASUMBULIWA NA MAJINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI.

    NIPIGIE 0742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA NA KUFATA MASHARTI. ANGALIZO USITUME SMS PIGA NA UWE NA NIA.

    (kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
    KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO AMBAYO SIJATAJA INSHAALAH ITATATULIWA IKIWA NDANI YA UWEZO WANGU.

    ReplyDelete