google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUSUDI LA KUCHAGUA LITASIMAMA

UFUFUO NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL 
IBADA YA JUMAPILI 16 APRILI 2023 
ASKOFU JOSEPHAT GWAJIMA 
SOMO: KUSUDI LA KUCHAGUA LITASIMAMA


Swali; Kwanini mimi nipo hapa? kwanini mimi ni mtu na sio mnyama? Kwanini mimi niko kama nilivyo?

Jibu; Ni kwa sababu Mungu amekuchagua kutimiza kusudi fulani hivyo ulivyo ili siku moja utoe hesabu ya kusudi lako hapa duniani.

“Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba. Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA. BWANA akamwambia,Mataifa mawili yako tumboni mwako,Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo.Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake.Wa kwanza akatoka, naye alikuwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau. Baadaye ndugu yake akatoka, na mkono wake unamshika Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa.” Mwanzo 25:21-26

“(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye), aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo. Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia. Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha! Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu. Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote. Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.” Warumi 9:11-18.

Mungu anampatia mtu kusudi sio kwa sababu kuna jambo zuri amelifanya ila ni kwa mapenzi yake yeye achaguaye. Mafanikio hayapo katika yeye apigaye mbio, ila ni kwa uwezo wake Mungu mwenyewe. Uwezo wako wa kuamua umesukwa na Mungu, ndiye anayekuongoza katika kufanya maamuzi. Esau na Yakobo hawakutenda baya wala jema ila ili kusudi la Mungu la kuchugua lisimame alimchagua Yakobo.

Duniani watu wanatabia ya kuhukumu mtu anayepitia shida au mabaya kuwa ni muovu. Kusudi la Mungu la kuchagua halijalishi umetenda ubaya au uzuri, japo kufanya matendo mema ni muhimu na mabaya sio yakufanya. Unakwenda mahali na utafika salama, ili kusudi la Mungu la kuchagua lisimame. Mpango na nia ya Mungu haiwezi kueleweka na mwanadamu.

Sasa kuna watu wanakupiga vita maana wanaona ulichonacho hukustahili bila kufahamu ni kusudi la Mungu kukuchagua sio kwa uweza wako bali ni kwa sababu kusudi la Mungu la kuchagua lisimame.

Hakuna sababu ya kusema jambo hili siliwezi au sina uwezo wa kutimiza jambo hili, yeye aliyekuchagua atakupata uwezo wa kulitimiza. Kabla kusudi lako halijatimia hakuna kitu wala mtu anayeweza kukuondoa duniani. Unapotoka mbinguni kuna kusudi umepewa na Mungu, na lazima hilo kusudi litimie kabla hujarudi.

Unaweza kumuona mtu anatabia mbaya ukamkataa kumbe ndio Mungu aliyemchagua na kumuita. Rahabu alikuja duniani kwa kusudi la kuficha wapelelezi wa Israeli ndani ya Yeriko na kupitia Salmoni aingie kwenye ukoo wa Mfalme Daudi mpaka Yesu, japo alikuwa kahaba.

“Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko. Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi. Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi. Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka; ikawa kama wakati wa kufungwa lango la mji, kulipokuwa giza, watu wale wakatoka, wala sijui walikokwenda; wafuateni upesi, maana mtawapata. Lakini yeye alikuwa amewapandisha darini, akawaficha kwa mabua ya kitani, aliyokuwa ameyatandika juu ya dari.” Yoshua 2:1-6

Yesu aliwekwa kwa ajili ya kuinuka kwa wengi na kuanguka kwa wengi. Safari yako inaanza ikiwa imemalizika, ndio maana Mungu anaitwa Mungu wa miisho kabla ya mianzo. Maisha yako yalishaamuliwa kabla hujazaliwa.

“kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.” Isaya 46:9-10.

Mambo yote hayapo kwenye uwezo wake atakaye, umesoma, hujasoma, hapo ulipo kuna jambo umechaguliwa, wale wanaozuia wanakuwaisha. Umepewa uwezo wa kugonga kila anayekuzuia na asikuzuie. Kesho yako imeshaamuliwa na Mungu.

Ukikosea na kutenda uovu, amka omba msamaha endelea, safari yake iko pale pale.

“Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari. Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.” Zaburi 46:9-11.

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA NZIMA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments