google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

WAMEIONA NYOTA YAKO.

UFUFUO NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL.
IBADA YA JUMAPILI 30TH APRIL,2023.
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE.
SOMO: WAMEIONA NYOTA YAKO.



Hii ni habari njema pia ni habari mbaya,nyota ya mtu inapoonekana ni habari njema lakini pia  mbaya lakini kwako ni habari njema.

“Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia. Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye”. Mathayo2: 1-3

“Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota. Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie. Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto. Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno. Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane”. Mathayo 7-11

Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”. Isaya 9:6

Biblia ni kitabu cha kiroho na ukiweza kuamini tu biblia ile mwanzo 1:1 basi mambo mengine yote baada yahapo unaweza kuamini. “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”. Mwanzo 1:1  ina maana kuna Mungu ukiona mbingu na nchi kuna aliyeziumba unaanza kuona kuna aliyeziumba yeye asiyeonekana ndiye anaitwa hapo mwanzo aliyeziumba mbingu na nchi, na ilikuwa ukiwa tupu na giza ndipo Roho wa Mungu akatulia juu ya maji, Mungu akasema iwe nuru ikawa nuru,  kuanzia hapo Mungu anasema vitu na vikawa vinatokea,biblia sio kitabu cha mantiki au logic ,ni kitabu ambacho haonekani anasema na vinatokea , ni kitabu ambacho nyoka anaongea na mtu, Mungu asiyeonekana anasema wanyama watokee na wanatokea, ardhi ilikuwepo imefunikwa na maji Mungu anasema pakavu paonekane na pakavu pakaoneka a, Mungu akasema iwe na angaa  maji yagawanyike ,angaa likagawa maji sio kwa mujibu wa sayansi bali kwa neno la Bwana , kwahiyo dunia hii kuna maji ya juu na ya chini, maji yaliyo chini yakusanyike pamoja ,na akaongea na pakavu paonekane sehemu moja, na maji yale yatoe ssmaki na yakatoa. Utakuwa na maisha yaliyojaa msongo wa mawazo, uwe kanisani au usiwe kanisani kama huamini biblia utakuwa na msongo wa mawazo, kama huamini biblia utajaa msongo wa mawazo kuna mambo yatakupata utachanganua kwa degree yako na usipate majibu ila kwenye neno la Mungu kuna majibu.

Watu wengi wenye akili nyngi ila hana Mungu ana changanyikiwa, dunia imejaa watu waliochaganyikiwa hata wakivaa suti wana msongo wa mawazo, ana degree ila ana msongo wa mawazo, kuna mtu mmoja hana degree wala cheo ila anamuamini Mungu. Mtu mwenye Mungu hatakama hana akili nyingi hana msongo wa mawazo, wewe unawaza vitu vingi kama mabadiliko ya tabia ya nchi, elimu imekufundisha na haina majibu, kadri unavyotafuta elimu dunia ndio unazidi kuchanganyikiwa, nakushauri baki hapo hapo. Anasem mfalme Sulemani wenye hekima nyingi kuna huzuni sana kuna mtu hafahamu kule Ukraine kuna vita ,vita pekee anayoifahamu ni ya rohoni,wana amani kama nini waipendao sheria ya Bwana hakuna kitu cha kuwakwaza, ameolewa au hajaolewa ila ana amani kama nini, amekula haja, hakuna kitu cha kumkwaza.

Kila ukiwaza hupati jibu msongo wa mawazo unakuja ila pesa unayo na elimu unayo, unapokuwa na vitu na havina msaada hapo ndipo msongo wa mawazo, pressa, kisukari vinaanza , hasa kugundua  havina uwezo kukuletea furaha , furaha ya kweli ipo kwa njooni ninyi nyote msumbukao na nakuelemewa na mizigo na mimi nitawapumzisha, jitieni  nira jifunzeni kwangu nanyi mtapata raha nafsini kwenu.

Kama kweli amesema njooni kwangu, kuna raha basi watu wa dunia wanadhania tunajifanya wala hatujifanyi, walihisi ulivyoachika nitakonda, nitakuwa wakulia, hapana kwake kuna furaha. Mumgu anamwambia Musa uso wangu utaenda na wewe nami nitakupa raha.

Wanao ongoza kujiua sio maskini, kuacha wake sio maskini ni matajiri ulidhania alipolewa na tajiri atakuwa na furaha maana kuna pesa ila ameachika. Billionea ndio wanaongoza kwakuacha mke, pesa zake hazia uwezo kukupa furaha, furaha ya kweli inapatikana kwa Mungu wana amani kama nini wapendao sheria ya Mungu. Maisha kwa asili ni ya rohoni ukIjaribu kuleta mantiki utachanganyikiwa ila kama unaamini mwanzo 1 utaamini hayo mengine.

Yesu alipozaliwa mamajusi wa mashariki waliona nyota wakasafiri. Mpaka wamesafiri ina maana wana uhakiki hawaja pigiwa simu wala kusoma vitabu ila kuna kitu cha rohoni waliona wakiwa mbali, biblia ni kitabu cha rohoni na wewe ni wa rohoni, Maisha ukiyakabili kimwili utaumia.

Mamajusi walipelewa kwa mfalme Herodi, zamani mfalme anazaliwa na mfalme na kuwa mfalme lazima atokee kwenye familia ya kifalme. Ni mtoto mmojawapo wa mfalme baada atakuwa mfalme hakuna uchaguzi. Mamajusi waliona nyota taifa la Israel kuna mfalme amezaliwa, wakachukua uvumba na manemane kwenda kumuona, wakasafiri wamebebea dhahabu pia kumpelekea yule mwenye nyota ya mfalme, wakafika Israel nyota ikapotea. Kuna jambo limetokea kwenye ulimwengu wa roho nyota ikapotea, wakaanza kuuliza watu hii nchi mfalme anakaa wapi maana bila shaka kwenye familia yake mtoto amezaliwa, Lakin Herodi akasema hakuna mtoto kwake aliyezaliwa, mamajusi wakamwambia kuna mtoto amezaliwa mfalme wa wayahudi, Herodi akawauliza viongozi wa wayahudi kuwa anazaliwa wapi mfalme? Wakamjibu Herodi kuwa mfalme atazaliwa Bethlehemu, kwa mujibu wa vitabu. Walipotoka pale ile nyota ikaonekana, nyota yamtoto ikiwaongoza watu wazima mpaka kwenye nyumba aliyekuwepo mtoto, Bethlehemu bila kuuliza walipomuona mtoto wakasujudu wakatoa uvumba na manemane mbele ya mtoto.

Haya mambo kwenye sayansi hayapo na haitumika hapa hatutumii elimu. Kanisani unakuja kumsikia Mungu aliye roho, Isaya inasema kwa ajili yetu mtoto mwanaume amezaliwa na uweza wakifalme utakuwa begani mwake, Isaya alimuona kabla na akamtaja kabla hajazaliwa miaka 600 alitoa unabii atazaliwa na manamke aliye bikira na akaona juu yake kuna nyota yakifalme inaitwa uweza wa kifalme. Kila mtu aliyezaliwa juu ya uso wanchi ni roho , kila mtu ametoka kwa Mungu, na kila mtu amepewa zawadi alipokuwa anakuja alipewa zawadi au kamara,kila mtu ana asili ya kiuungu ndani yake kila mtu sio aliyeokoka tu bali kila mtu ana Uweza wa kiungu wa kufanya mambo fulani maana Mungu anaweza mambo yote ameweka uwezo kidogo kidogo kwa kila mtu, kila mtu ana uwezo  wa kiungu ndani yake na kwenye eneo hilo unafanya kama Mungu yaani unafanya mambo ambayo Mungu angekuwa mtu angefanya hivyo hivyo.

Ukiwaleta watu wengi kwa karibu utagundua wana uwezo wakiungu, ndani ya mtu kuna uwezesho wa mtu kufanya mambo ya kiungu hiyo ndio inaitwa zawadi, unaweza kufanya mambo tofauti. Umezaliwa nayo nahii ndio inaitwa nyota ndio sababu ya mtu kufanikiwa, nyota inapooneka kuna watu wanawezo wakuja kwa nia mbaya ua nzuri. Uweza wakiungu kifalme upo begani mwake wachawi wa mashariki wakale wakaona ni nyota ya kifamle.

“Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;
Kila kigeukapo hufanikiwa”.
Mithali 17:8

Kito cha thamani ni kama zilivyo almasi au dhahabu, Karama ni kito cha thamani. Kuna dhahabu, almasi na rubi hivyi ni vito vya thamani, kipawa ni kito cha thamani kwake yeye aliye nacho kila kigeukapo yeye hufanikiwa. Inaonyesha mafanikio haya ni kwa kipawa sio elimu na watu wanaofanikiwa ni watu wenye kipawa sio elimu, kipawa cha kuongea au kuingiza sauti ya mtu,kuna mtu  akikusikia ndani ya dakika chache anaongea kama wewe, hata uende shule huwezi fanya kama yeye, Ronaldo ana kipawa cha kucheza mpira ndio maana anafahamika sana hata wewe unacho kipawa kikafahamika na wewe utafaamika sana tu.

“Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu”. Mithali 18:16

Lugha nyingine ya kipawa ni zawadi, unaweza ukawa hujasoma shule ila uko karibu na watu wakuu ili ufanikiwe lazima watu wakuu wakufahamu ndio ufanikiwe. Nyota yako inakupatia nafasi sio elimu itakupatia nafasi na kipawa  unacho kikionekana nafasi yako itaonekana tu hata kama ni kampuni hakuna nafasi yako itabidi watengeneze nafasi kwa ajili yako. Kijana mdogo anachunga kondoo kule Bethlehemu  hana maana hata kwa ndugu zake wa babaye, akiwa kule anatumia kipawa chake ila hawamlipi fedha, endelea kutumia kipawa chako, kijana anapiga kinanda pale Bethlehemu ila hafahamiki na wakuu.

Basi Sauli akawaambia, Vema, nitafutieni mtu aliye stadi wa kupiga kinubi, mkaniletee. Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, aliye stadi wa kupiga kinubi, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye BWANA yu pamoja naye. Basi Sauli akampelekea Yese wajumbe, akasema, Nipelekee Daudi mwanao, aliye pamoja na kondoo. Yese akatwaa punda, wa kuchukua mikate, na kiriba cha divai, na mwana-mbuzi, akampelekea Sauli kwa mkono wa Daudi mwanawe. Basi Daudi akamwendea Sauli, akasimama mbele yake, naye akampenda sana; naye akapata kuwa mtu wa kumchukulia silaha zake. Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, mwache Daudi asimame mbele yangu; maana ameona kibali machoni pangu. Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”. 1Samweli 16:17-23

Huyu ni mfalme wa nchi anasema atafutiwe mtu anaye juu kupiga kinanda. Mtu mmoja anakaa na wakuu na kuna mahitaji ya mkuu yamesema nayeye ana mfahamu mtu ambaye si mkuu. Hapa unaona kipawa cha mtu na tabia ya mtu huyu, mpaka mtu anaweka dhamana maisha yake ili huyu mtu akiharibu, mpaka mtu akutaje kwa wakuu tabia zako ni muhimu ili zisiharibu mambo, asema mtu huyu ana Mungu na ananena kwa busara,.

Kijana mdogo anakaa na kondoo hajasoma shule ila ana nyota, mfalme ameongea na watu wake wa karibu wamtafutue mtu, kuna baadhi ya mambo hutayatafuta kwa sababu nyota yako imeonekana, nyota yako ikaonekane wakutafuta. Hii ili mfanya Daudi kwa mara ya kwanza kwenda ikulu kwa mfalme, ni kipi kina mpeleka ikulu? Ila ni nyota yake. Kuna watu wanaona yeye na mungu inatosha hapana haitoshi, kuna watu wana ukaribu  na watu wakuu. Kuna watu wa kawaida wana fahamia na watu wasio wa kawaida na hao watu wa kawaida wanahitaji kukusema kwa wakuu. Chunga tabia zako zinaweza kukwamisha nyota yako kufanikiwa.

Kuna watu wanaamini kuwa wanachukiwa hata kwenye familia anaamini baba ama mama yake hawampendi ,husema tangu nizaliwe sijawahi kupumzika kazi zote ni zake hata akisemeshwa kidogo basi anachukiwa, sisi hatumpendi shetani kwani wewe ni shetani? Kuna watu wanapenda amani anapokuona wewe ni mtu wa shari, unakaa kwa mtu na anakusaidia ila unaishia kulalamika tu inabidi ushukuru sana kwa kuweza kukupatia mahali pakukaa na hakuna bili yoyote unadaiwa unakuta una nyota  na mtu ameona akusaidie ila kwa tabia yako ina haribu nyota.  Niliwahi kudhamiria kumchukua kijana mmoja akae kwangu nimsomeshe maana nina uwezo wakumlipia kidato cha kwanza hadi cha nne ila yeye tabia zake ni kaona ni za ugombanishi, nikamwacha akae  kanisani na malaika wa kanisa la Ufufuo na Uzima.

Kipawa chenyewe kina kutengenezea nafasi kwenye moyo wa mtu na itamtaka akusaidie. Tumeona nyota yake na imetuvuta kwake, kuna mtu nyota yake inakuvutia kumchumbia, wakati mwingine hakuna anayekupiga vita unajipiga vita mwenyewe. Unaweza kukaa kwenye dhiki kwa muda fulani ila Mungu atakutoa kwa wakati wake. Naongelea nyota na nafasi, zawadi ya mtu humfanyia nafasi mbele ya wakuu. Wakuu wanaongea na wachache wa karibu yao wamletee mtu fulani. Watu wote wanao msaidia mkuu wa nchi wanakaa alipokuwa mkuu wa nchi sio kwa sababu ya elimu ila waliona nyota yake.

Kuna siku nilimuona mtu anayemnyoa raisi nywele nikaambiwa anakaa ikulu na sio kwamba kila siku anamnyoa ila anakaa karibu tu kusubiria ziote nywele amnyoe, hii ni kwa sababu ya kiusalama. Waione nyota yako, Sauli aliandika barua kwa Yese babaye Daudi, kuwa Daudi abaki ikulu maana amepata kibali machoni pa Sauli, nyota yako ya biashara ionekane.

Siku ya kwanza baba alimuona Pastor Paul kule Maragalasi, Pator Paul ni mchungaji kwelikweli maana amewahi kuchunga kondoo, mbuzi hata mbwa, baba alipomuona akaniambi kuna kijana nimemuona. Siku moja nikaenda Kigoma nilipomuona Pastor Paul, ila sikujua ndio baba alimzungumzia nikasema nitaongea nae muda wa chakula cha mchana, nilipewa wali na migebuka, nikamuuliza una mipango gani ya maisha akasema nataka kusoma sheria, nikamwambia mbona wewe ni mchungaji, maana alikuwa SNP wa Maragalasi ila anachapa gombo kama wale wa cathedral Ubungo. Baba akasema tupeleke mwangalizi Maragalasi. Kwa mara ya kwanza akapokea wito akaja Ubungo, fanya kazi ya Mungu kwa bidii hata kama uko porini wataiona nyota yako. Baba akasema aitwe mara moja na baba akikuita ujue kuna vitu vitakusindikiza. Alikuja akafikia pale Hai moshi akawa muhubiri mjini, wilaya ya Kilimanjaro karibu na  Moshi, nyota ikaonekana. Fanya kwa bidii hata kama ni fundi viatu au muimbaji hata ikulu wapo hawakai Msewe. Mtu anapokupa kazi fanya kwa biddi watakutaja mahali hata kama huwafahamu wakuu, mtu atakutaja kwa wakuu.

Siku moja nikaongea na baba, yule kijana anapiga gombo mpaka moshi mjini alikuwa analala kanisani, na wengine watu wa kanisani  wakamwambia hawa kutunzi, unalala kanisani kama wana thamini huduma yako wakupangie nyumba, wewe una moto ila hawa kutunzi ungepangiwa chumba chenye AC , nikamuonyesha baba clip yake , baba kasema huyu sio wa Moshi aje mzimuni, wewe pia una nyota yako inaweza isiwe kuomba,kusalisha,ila una nyota, huhitaji kujitangaza. Nyota yeyewe itakupatia nafsi, ni kito cha thamani ni zaidi ya dhahabu. Kuna kitu unacho ni cha ki-Mungu hata kama hulipi kuna siku utatajwa mahali.

Yusuph mwana wa Yakobo alikuwa gerezani ana tafsiri ndoto na halipi, nyota  ikifika mahali itajilipa yenyewe nachukia mtu anayefanya mambo mpaka alipwe. Kuna mabo unayaona kawaida ila ni mabaya, unawaombea watu na kuwaomba pesa ndio una nyota ya kuombea watu. Juzi niliambiwa ni peleke watu watano nyumbani kwa mtu mkubwa wakae siku 5 wamuombee, je nikikupeleka ukaanza kuomba pesa si utaniambisha, kuna watu ni wakuu hawahitaji uwaombe pesa ila wao watakupatia kuliko uliyofikiri kuomba, usiwe na tabia yakuenda pesa na kuweka pesa mbele kwa kila jambo.

Nimeshuhudia hapa kanisani baba anaombwa apeleke watu mahali kuomba ila wanaenda kuharibu ni kwasababu kuna mambo wameyaozea , utaeda kwa mtu mkubwa na baada ya maombi unaomba elfu 50,kumbe yeye alitaka kukupa 3m anaona una njaa sana na kuhisi unaweza muibia tv, kipawa cha mtu kina kupatia nafasi kwa watu kwa kutumia kipawa alichokupatia kama zawadi, tabia sasa. Nyota ya Yesu ilipotea maana yake kuna vitu ulitakiwa uletewe ila vikapotea, shetani hawezi kumuibia nyota aliyeokoka ila anaifunika haiwezi kuonekana kwa wakuu wakaona, na kifuniko kikubwa kwa nyota ni tabia, wanaogopa kukaa karibu na wewe kwa sababu ya tabia. Na hizi tabia ambazo ni kifuniko cha nyota ni tabia zenye uvuvio wa shetani, siongelei tabia za mwilini ila za rohoni, mtu ni muimbaji mzuri ila tabia sasa, kila mtu mwenye mapepo akipagawa kuna tabia ataonyesha ambayo sio yake anaweza kuanza kupiga kareti au kutukana, unakuta ni mdada tena ila unagundua sio yeye. Shetani hahitaji udhihirishe tabia mbaya muda wote, ni mpaka ufike kwenye fursa ndio ana jidhihirisha.

Unaweza muona binti, ukatamani upeleke jina kwa Pastor Msimbe unataka kuoa binti, sasa jumapili unamkuta amekaa mbele madhabahuni na sio mahali pake pakukaa, anaomba mara anaambiwa na kiongozi asikae madhabahuni, anaanza kumfokea kiongozi, unaenda kwa mzee Msimbe anakuambia yule mbona ni kichaa, umesema unataka mke au umsaidie kumpeleka milembe.

Kila jambo la ki-Mungu lina wakati wake, ikifika muda wake shetani anakupanda kichwani unakuta mtu muda wake umefika, ukiwa kiongozi ina bidii uwa hurumie watu kuna mtu ni jeuri na kiburi ni kwa sababu ana nyota na muda wake umefika, Stephano anasema ili pokaribia wakati wa Mungu , ndipo Farao akazidi kuwatesa wana wa Israel, kuna wakati unafikia ndio mashetani yanaibuka kifuniko kikubwa cha nyota ni tabia zenye uvuvio wa shetani, nyota ni kitu cha rohoni na kuna tabia ni matokeo ya tabia za rohoni, kama iIlivyo Roho Mtakatifu akiwa ndani ya mtu ana matunda au matendo. Tunda la roho ni upendo, furaha, utu wema, amani, fadhili, uaminifu ni tabia mambo sio asili ya mtu. Kuna mtu ni mkorofi ila akijaa Roho anakuwa mpole ,mkaribu nini hiki ni kwakuwa Roho ameingia ndani yake na kumpa tabia nzuri. Likewise shetani anaweza kufanya kazi akiwa ndani ya mtu au nje anamvuvia maana yake anampa hisia mawazo juu ya tabia fulani ukorofi, uasi na matusi.

Mtu ni mkorofi mbishi, ila ukimkuta anaabudu na kusifu unaweza muona mke bora ila akiweka mic chini ni mkorofi kama ibilisi. Ila sio yeye kuna tabia watu wanazo ila sio tabia zao za asili ni wakati umefika shetani anamfunika na tabia ili asionekane, mtu ana tabia ya mahusiano, biashara na inaonekana ila tabia japokuwa nyota ipo hapa nyota haijaibia ila imefunikwa.

Yesu nyota ilipotea na kama isingeonekana wangerudi kwao na uvumba, dhahabu na manemane, kuna mtu wakati umefika uanze biashara, familia ila shetani anakuletea tabia hata kama unanena ila hawakutaki tena. Binafsi mtu asiyeheshimu mamlaka simtaki hata aweje itabidii nitumie neno. Mtu kumvunjia heshima mtu mzima hata kama amekukosea. Paulo anamwambia Timotheo usiana na wazee kama baba zako ama mama zako muheshimu mzee. Kuna mambo hutakiwi kumfanyia mtu aliyekuzidi umri hata kama una mzidi vipawa ule utu uzima wake unahitaji kuheshimiwa sio ishu ya cheo chake.

Kuna nabii nilimuona anachapa wazee Pastor Mwagela ukienda pale utachapwa viboko, hata kama una mafunuo ndio mpaka wazee una wachapa.

Ni kama lile neno nzuri Mungu alisema nimependa Yakobo nimemchukia Esau, kwasababu alidharua kitu cha Kiungu, mamlaka ni kitu cha Kiungu Mungu aliweka badala yake, itabdi nisome neno na kuomba Mungu anisaidie nikupende huheshimu watu wazima. Watu wengi waovu, waasi, kudharau mamlaka sio wao ni shetani anawavuvia. Shetani anafanya kazi na wewe, ile kudharau mamlaka ni kifuniko shetani anaweka ili nyota yako isionekane.

Nakuahidi kuwa muda niliopo hapana usipo heshimu mamlaka nitahakikisha haustawi nitakumwagia chumvi, sipendi mtu astawi kama haheshimu mamlaka maana atanisumbua ni heri afe na ina ruhushiwa ili wengine wapone. Nyota imeonekana ila tabia nyingine za watu ni zile zenye uvuvio wa kishetani. Shetani anaona na anakutumia wachawi wanaingia ndani yako au anakuvuvia  unaanza jiona wewe ni  maalumu sana au wakipeeke wa aina yako ni wewe tu. Kanisa lazima liheshimiwe kuwa na adabu wazee waheshimiwe. Kama huwezi hama kanisa.

“Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda. Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe. Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia; akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese. Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.  Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni,
kwa kuwa tu wengi. Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha.
Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao. Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini. Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea.
Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa. Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza ni mambo gani yaliyompata yule mwenye pepo, na habari za nguruwe. Wakaanza kumsihi aondoke mipakani mwao. Naye alipokuwa akipanda chomboni, yule aliyekuwa na pepo akamsihi kwamba awe pamoja naye; lakini hakumruhusu, bali alimwambia, Enenda zako nyumbani kwako, kwa watu wa kwenu, kawahubiri ni mambo gani makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokurehemu. Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu Yesu aliyomtendea; watu wote wakastaajabu”.
Marko 5:1-20 

Huyu ni mwenye pepo ni muhubiri na Yesu hawezi kumwambia mtu akahubiri kama hana kipawa, sasa ameingiwa na mashetani baada ya mapepo kutoka akaenda kuhuburi na baadae alikuja kuwa na makanisa 10 Dekapori alikuwa askofu. Mtu mkorofi asikilizi watu wafahamu shetani anakifunika kwa kumvuvia na tabia au anaingia ndani yako, huyu ni  muhibiri mwenyewe uwezo wakuhubiri ila anakaa makaburini anajeshi la mapepo ndani yake ,amefungwa minyororo. Unakuwa na mtoto ana tabia mbaya ya wanaume umechapa na ukachapa akasema hatarudia na kuapa ameapa na kusema nikifanya uzinzi ardhi ipasuke niingie kama Kora ila ukiingia ndani tu unakuta anaongea na mwanaume atume nauli ataenda tena. Utagundua huyu sio wakuchapa ila anahitaji maombi maana hiyo ni tabia ya shetani amepanda Roho iwe tabia anasema nitawaingia washauriwa Rahabu waongee uongo. Ni uvuvio wa kishetani ulipovunjika wakamuona ana akili timamu amevaa nguo anahubiri kotekote Dekapori na watu wakashangaa. Mtu anaye hasi mamlaka ana uvuvio wa kishetani yuko nje au ndani,

“Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye, Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye, na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao”Luka 8:1-3   

Mariam Magdalena alikuwa na nyota ya fedha, pia alikuwa na mapepo saba alipofunguliwa akaanza biashara na kutoa fedha kwenye huduma ya Yesu ina maana asingetokwa na pepo asingeweza kufanya biashara, kuna mtu hapa anatakiwa kufanya baishara apate pesa awezeshe kanisa, kuwa na pepo saba ni sawa na kuwa na watu saba wasio na miili ndani yako. Mungu anataka waione nyota yako ili akuketishe na wakuu.

Kuna mtu ni muongo hata kwenye mambo yasiyo ya kudanganya anadanganya, ni muongo tu ili kipawa kifunikwe asionekane kuna mtu anatakiwa akupetenda. Kuna mambo usidanganye unakaa wapi, umri au kabila lako, kuna kitu mtu anataka akupatie ila anajiuliza kama kanisani umemdanganya je akikupa tenda ya kumjengea si utaiba hadi tofali. Uvuvio wa shetani unampatia mtu tabia na kuna uvuvio wa ki-Mungu humpatia mtu tabia. Tabia za ki-Mungu ambazo roho akikaa ndani analeta matunda ambayo ni upendo, kuvumilia, kufadhili, utu wema, upole kiasi. Kuna roho zikikaa ndani ya mtu ni mkorofi anatukana.  Tabia mbaya watu ambazo adui amewavuvia ili nyota isionekane watu wakulete. Leo vunja kwa Jina la Yesu ili nyota yako ionekane ,wakuletee yale Mungu amepanga uyapate. AMEN.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments