UFUFUO NA UZIMA UBUNGO
CATHEDRAL.
IBADA YA JUMAPILI 21 MAY, 2023.
ASKOFU BARAKA THOMAS
TEGGGE.
SOMO: ROHO YA
UDANGANYIFU.
Silaha
kubwa ya shetani ni udanganyifu ili shetani akupate lazima akudanganye, shetani
ni muongo, mlaghai, yeye alikuwa wakwanza kudanganywa, silaha kubwa shetani
utumia kuharibu watu, kuharibu maisha watu ni kwa kuwadangnya. Imeandikwa vaeni
silaha za Mungu ili mpate kuzishinda hila za shetani, silaha yetu ina nguvu ili
tuweze kushinda ulaghai wa shetani. Shetani nisawa na mwanaume muhuni ili
ampate binti lazima amdanganye maana akija kama alivyo hakuna atakaye mpata
anajigeuza na kuwa malaika wa nuru,
akija na mapembe hakuna atakaye mkubalia, ni sawa na muuza chuma lazima
akudanganye anakuambia zimedondoshwa na wazungu sijui ni dhababu, na unaamini
na unaenda atm kutoa pesa na kununua ukidhania ni dhahabu kumbe ni chuma
ametumia udanganyifu kukuaminisha, ili kuolewa na mwanaume mdanganyifu lazima
akulaghai, je angekuambia anataka kukuoa na kukuacha baada ya miaka miwili
utamkubalia, hapana lazima akulaghai. Anakudanganya kuwa amesafiri dunia nzima
hajaona mwanamke kama wewe, kumbe ni kwenye ulimwengu wake huu wote ni
udanganyifu, maisha ya mwanadamu yalikuwa sawa kuna mahali Mungu alitaka
mwanadamu awe, ila amedanganywa mpaka maisha yakawa magumu, hatukosi kuzijua
fikra zake ili asipate kutushinda.
Huwezi
mshinda shetani kama hujui njia zake za udanganyifu, kuna watu ni waongo na
uongo wake unafanya kazi katika eneo analokaa kama anaishi kijijini anaweza
kudanganya wa kijijini ila wa mjini asiweze, akivuka nje ya nchi hawezi
danganya ila shetani anaweza kudanganya watu wote wa mjini na kijijini, wasomi
na ambao hawajasoma.
“Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi
kuzijua fikira zake”. 2 Wakorinthro2:11
Shetani
anaitwa nyoka wa zamani mbinu zake ni zile zile. Watu wa zamani wanaweza
kubashiri baadae yako maana wameishaona unayopitia mwisho wake utakuwa je maana
yeye aliwahi kuishia pale ambako anakuambia utaishia. Anaweza kuwa mshauri
nzuri wa ndoa maana yeye ndoa yake ilimshindaga kwa hiyo ni mshauri mzuri. “Iko
njia ionekanayo sawa machoni pa mtu lakini mwisho wake ni njia ya mauti “. Mithali
16:25. Ni vizuri kuwasikiliza watu wazamani maana ile kukaa muda mrefu
imempa hekima. Ni sawa na mtu aliyewahi kuibiwa hawezi kuibiwa tena maana
anajua hizo mbinu. Wasikilize watu wazamani maana wana siri ambazo zitachukua
muda kuzijua maana hazijaandikwa kitabuni wala popote.
Shetani
ni wazamani na mbinu zake ni za zamani kwanini zinafanya kazi, sio kwa sababu
umesoma kitabu cha kuwa na ndoa nzuri kitakusaidia maana aliyeandika ameandika
kwa uzoefu wake na maisha aliyopitia yeye haimanishi wewe kitakufaa kwenye ndoa
yako uliyonayo au utaishi maisha kama yake. Wewe unahitaji hekima kutoka kwa
wazee wa kwenu. Ayubu anasema waulize kizazi cha zamani watakuambia. Shetani
anaitwa nyoka wa zamani audanganye ulimwengu wote ili uwe salama inabidi uijue
kweli ya neno la Mungu, mambo hayako kama yanavyoonekana waweza kuona mazuri
kumbe nyuma yale kuna ubaya, Mungu akisema kweli ndio inakuwa hivyo. “ Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu
aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema
Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani? Mwanamke akamwambia nyoka,
Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; lakini matunda ya mti ulio
katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. Nyoka
akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba
siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu,
mkijua mema na mabaya. Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa
chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa
katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala, Wakafumbuliwa macho
wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia
nguo. Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati
wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu
asiwaone. Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi? Akasema,
Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha.
Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya
mti niliyokuagiza usiyale? Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja
nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala. Bwana Mungu akamwambia
mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala”.
Mwanzo 3: 1-13
Huu
mti sio mti mgeni maana anauona siku zote na anajua akila matunda yake hapo
atakufa kwa hiyo kila akiuona anaona ni mauti ila aliongea na mtu akamwambia unafaa
na mwanamke akaona kinatamanisha. Zamani ilikujua upo uchi lazima uambiwe na Mungu
ndiye atakayekuambia, maisha yangekuwa raha sana maana sasa hivi kuna kununua
nguo ni gharama. Kwahiyo Mungu pekee ndiye anayeweza kukuambia upo uchi au ule
kitu ambacho Mungu amekuzia kula.
Kuna
mambo Mungu hajakuambia ili uwe na amani, ajakuambia kuwa wanataka roho yako
kesho ili uwe na amani. Kabla ya udanganyifu
Adamu alipomuona Eva alisema wewe ni nyama katika nyama zangu wewe ni mfupa
katika mfupa wangu ila baada ya udanganyifu akasema ni huyu mwanamke uliyenipa.
Kila mwanamke mwenye miaka 25 kwenda juu aliishawahi kuambiwa maneno mazuri
sana ila kuna siku mambo yalibadilika akasema ni huyu mwanamke niliyepewa na Pastor
Baraka. Kuna mtu aliniambia nyuma ya mwanamke mwenye majonzi au msongo wa
mawazo sio kwamba ni biashara ina mchanganya wala masomo hapana ila ni mwanaume
aliyewahi kumpenda akamseme maneno makali. Imeandikwa enyi wanaume wapendeni
wake zenu, ghafla siku moja akaja mgeni na kumkuta mwanamke na kuanza kuuliza
maswali, shetani anajua ukweli ila hawezi kusema ukweli, anaitwa baba wa uongo
anapoulizwa maswali sio kama hajui ila anataka kukuuliza ili akudanganye, mwanamke
alipoulizwa habari ya kula matunda akasema Mungu amewakataza wasile matunda ya
mti huo, ila shetani akacheka akamwambia sio kweli ila mti huu unaleta kujua
mema na mabaya. Yule mwanamke akaona kumbe mti wafaa kula matunda yake,
aliposema nami roho ikaniingia unapomsikiliza shetani roho itakuingia, unaanza kuona
mambo yale uliyoona sio sawa ila unaanza kuyazoea na kuona ni ya kawaida, siku
zote uliamini kuwa mwanamke anapaswa kumtii mume wake ila baada ya kuangalia
tamthilia sana ukabadilika, unakuta katika tamthilia hiyo hakuna kipande
chochote kinaonyesha mwanamke anapaswa kumuhudumia mume wake. Hapo ndipo nyoka
alikusemesha, kuna watu ndoa zinasumbua maana anaishi maisha ya kwenye tamthilia
anasubiria mumewe amlete mauwa, umfungulie mlango wa gari hayo ni maisha ya tamthilia.
Unapomuoa binti wa hivyo itakusumbua. Namna ya kuona mambo ya ndoa ishaharibiwa
na shetani.
Binti
mmoja alikuja ofisini anataka tuongee akasema pastor unaweza kuamini mpaka saa
hizi saa sita mchumba wangu hajanitakiwa heri ya kuzaliwa kwenye kikundi cha
vijana kanisani hajatuma ujumbe huko, pia hajamuweka status, niliona ni upuuzi
mtupu. Ila kwakuwa mimi ni mchungaji nikamsikiliza, nikamwita kijana, akasema
nimemtumia meseji ndefu ya mapenzi saa sita usiku, amepanga maneno, ikamfikia binti
muda huo huo kwenye simu yake binafsi, binti akasema ameiona ila anataka atume ujumbe
kwenye kikundi cha vijana kanisani. Lakini haya yote ni mambo ameona kwa
mabinti wenzake au kwenye tamthilia ndio
anaamini nikupedwa huko. Hiki nikizazi cha maonyesho. Maisha yako ya sirini
unataka uyaweke hadharani ila hii ni kwasababu ameonyeshwa, amesikia, ameona
mahali kupitia kwa nyoka wa kwenye tamthilia. Kuna mambo ukianza kuyasikia
mtazamo unabadilika kile ulichoona mwanzoni kinafaa unaanza kuona tofauti,
aliposema nami roho ikaniingia ni hatari kuwasiliza baadhi ya watu ni hatari amejaa
sumu kuhusu viongozi wakanisani, maana uongo unaanza na mtazamo , ulisema bila
baba usingekuwa hapo ulivyo, alinitoa msukuleni ila sasa unasema Gwajima ni nani na uliamini baba ni mkuu kuliko wote
ila siku ulivyoongea na nyoka ndipo ulibadilika. Uongo hauna madhara kama
ukisikia usiamini ila ukiamini pale pale mtizamo wako unabadilika.
Sauli
anaambiwa na Samweli ulikuwa mdogo machoni pako mpaka siku ulipopakwa mafuta ila
sasa naongea na wewe unaongea, ndivyo walivyo watu walikuwa wadogo mpaka siku
walivyosikia sauti nyingine, ulikuwa na heshima unawaheshimu baba, mama, ila
siku roho ilipoingia ukaacha kumuheshimu. Watu wengi wakorofi ni watu wasiojua
mamlaka maana hawajawahi kukaa chini ya mamlaka. Mtu yeyote anayemuheshimu baba
yake mzazi hatapata shida kumuheshimu mchungaji wake. Tulikuwa na baba zetu wa kimwili
tukawastahii, je ni jambo gumu kujiweka chini ya baba wa kiroho? wale watoto
wako katika kuheshimu mamlaka.
“Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja
wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa
matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; kwa hiyo Bwana Mungu
akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.
Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya
Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima”.
Mwanzo 3:22-24
Mahali
walipokuwa wamewekwa wakafukuzwa maana wamemsikiliza mwingine na sio yule
aliyewaweka. Yule mwanamke mwanzoni aliogopa lakini ghafla akaacha kuogopa.
Nimtende Mungu huo uovu mkubwa namna hii.
Zamani ulikuwa unaogopa kutenda dhambi, kuongea na mwanamke ambaye hujamuoa,
ila sasa unajisifika na kusimulia hii ni kwasababu umesikia sauti ya nyoka, mshahara
wa dhambi ni mauti Mungu ameishasema wawe wamekuona au hawajakuona dhambi
inaitwa dhambi haijalishi umefanya na nini,. Msidanganyike chochote apandacho mtu
atakivuna amesema Paulo. Waheshimu baba
yako na mama yako ili uishi miaka mingi, Mungu akisema jambo hiyo ni sheria,
azinineye na mwanamke anaiangamiza nafsi yake mwenyewe hata kama sio leo
itatimia, alisikia sauti ya Mungu akiambiwa asile haya matunda na ana ujasiri
wakusema kabisa Mungu alisema usile matunda haya, ila roho ya udanganyifu ili pomuingia
akaona yafaa, akaona kumbe kuna siri
kuwa anaweza kuwa Mungu hakuwaza dunia yake ataiitaje na pia akapata ujasiri
wakumshawishi na Adamu, roho ya udanganyifu ndivyo ilivyo unadanganyika na
unapata ujasiri wa kumdanganya mwenzake. Yeye aliamini akiolewa nje yakanisa
atakuwa sana ila hakuwa sawa na anapata ujasiri wakuwaambiwa wengine waolewe ni
sawa ila hayuko sawa.
Roho
ya udanganyifu inafanyakazi kwa kuaminisha kuwa dhambi haina madhara,
inakuambia ukiishazini utubu maana dhambi zetu zijapokuwa nyekundu kama damu
atazisafisha na kuwa nyeupe kama lethuji. Binti mmoja alikuwa anaishi maisha ya
ndoa kabla hajaolewa, nikamwambia Yesu akija leo utasema je, na unafahamu
kabisa hii ni dhambi. Akasema pastor niko makini sana anasema siku zote akiwa
anazini huwa anatubu pale pale, nikashangaa haya ni masomo gani, alisoma.
Ila
haya mambo ni kwasababu mtu ana mtizamo mwingine anao na hauji hivyo hivyi ila
kuna roho ya uovu inakudanganyika. Neno linasema Mungu hadhihakiwi, ukipanda
uovu utavuna uovu. Shetani anakujaza moyo wako uongo, Petro anamwambia Anania
kwanini shetani amekujaza moyo wako, mtu anakuwa mbishi anakutwa amezini ila
anataka ushahidi. Maneno hutoka na kile kilichojaa moyoni ili useme uongo
lazima moyo wako ujae uongo ndipo useme, watu wanaishi maisha ya uongo anataka
kuwa furahisha watu anadanganya kwasababu
anaishi maisha yasio yake.
Kulazimisha
mambo kuhusu maisha yako inabidi udanyanye na kutenda dhambi, Mungu ni wa hatua
kwa hatua baki hapo ulipo, anzia hapo hapoo wewe sio wa kukaa Sinza nyumba
nzima wewe ni wa Msewe chumba kimoja. Utaishi maisha ya furaha sana na kuwa na
amani hatakama watu hawakuelewi ukiishi maisha yako Mungu aliyoamuru, baki pale
pale mpaka Mungu atakapo kuambia, kaa hapo jangwa utapita na utaikumbuka maana
bwana alikuongoza, mwanadamu hataishi kwa mkate, ni maisha magumu ila bwana
anataka akufundishe, utapita jangwani ila bwana alitaka uone njia, Mungu
aliwaacha jangwani na kuwalisha mana kwa sababu alitaka wajifunze.
Hata
mimi nimewahi kukaa jangwani, nakula mchele, mchele una tofauti na wali,
nimekaa kwenye pagale la mtu, sikuwa na kitu, sina pesa, siku inaisha hata sijui
imeishaje, sikuwa na chochote ila nilichumbia mchumba nikiwa jangwani ila
nilikuwa na maneno mazito. Nilikuwa nampanga mke wangu na mwambia mimi nitakuwa
mtu mkubwa sana, hakikisha una passport utakuwa unapeleka watoto marekani kusoma
ila sasa hivi wanasoma goba, kila mtu ana wakati wake wa jangwani hata kama upo
jangwani kuna wakati wa wakutoka. Mabinti wanaharibikiwa kwenye Maisha yao,
maana aniga maisha ya wale marafiki zake wa chuo. Kuna mtu mmoja ana mafuta na
amekaa jangwani miaka 15 na anasema ilikuwa vema kukaa jangwani ili kujifunza
njia za bwana. Unakuta binti ana madeni kanisani na hawa ndio wanaongoza
kuwaumiza wengine unakuta kuanzia juu mpaka chini amekopa, anadanganya atalipa
mwisho wa mwezi wakati hana kazi, anaishi maisha ya kuwafurahishwa watu, maisha
ya ulaghai, msubirie Bwana kuna wakati wako wakutoka, roho ya udanganyifu inakujaza
moyo.
Mtu
wa kwanza Mfalme Ahabu amekaaa kwa amani miaka 3 siku moja akapata wazo la
kwenda kupigana Ramoth-Gileadi na akaenda kuuliza kwa manabii ambao wamejazwa
na roho ya uongo. Akauliza kwani hakuna mtu wa bwana maana yake wale hawakuwa
wa Bwana. Shetani akitaka uharibikiwe anakupandia chuki unawachukia watu ambao
unawahitaji. “Wakakaa miaka mitatu pasipo vita
kati ya Shamu na Israeli. Ikawa, mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme Wa
Yuda akamshukia mfalme wa Israeli. Mfalme wa Israeli akawaambia
watumishi wake, Je! Hamjui ya kuwa Ramoth-Gileadi ni yetu? Nasi tumenyamaza
tusiitwae mkononi mwa mfalme wa Shamu?”1 Wafalme 22:1-3
“Mikaya akasema, Sikia basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana
ameketi katika kiti chake cha enzi, na jeshi lote la mbinguni wamesimama upande
wa mkono wake wa kuume na wa kushoto”. 1Wafalme 22:19
Akaitwa
Mikaya, Mikaya akasema mimi mfalme Ahabu nimemuona Bwana ila hawa manabii zako
wanaongea mambo ya kukufurahisha kwa sababu wamepewa posho, akasema ameona kifo
cha ajabu. Mungu ana namna ya kuongoza watu, Mungu anaongoza watu kwa kutuma
mamlaka. Shetani akitaka kumuua mtu anampa jambo litakalompelekea kifo. Unaambiwa
hiki acha utaharibikiwa lakini hutaki. Shetani anaweza kuvuvia watu wako wa
karibu ili wakuvuvie ukaolewe ufe. Petro alipokuwa anahubiri waliposikia maneno
Kornelio na wenzake wakajaa roho, kwa nini? kwa sababu maneno ni roho. Mtu
yeyote aliye kinyume cha Baba hata kama ni rafiki yako kaa naye mbali. Mtu
yeyote anayeongea vibaya kuhusu kanisa kaa naye mbali bila kujali beji yake. Ukijifanya
mwerevu kuliko Mungu utaharibikiwa, Mungu mwenyewe alimtupa shetani nje baada
ya kuharibikiwa. Hutafanikiwa kwenye maisha kama hutajua kanuni, mtu akimuasi
Baba ameasi watu wote wa Baba, kuambatana kuna gharama.
Huwezi
kwenda na mtu mwovu usiwe mwovu, wawili hawawezi kwenda pamoja isipokuwa
wamepatana. Mtu yeyote anayeasi kanisa ana sumu kuhusu viongozi, udanganyifu
unahisi kwamba unaweza kwenda kinyume na kanuni na bado ukawa uko sawa. Mtu
akiwa rafiki yako kuna mambo utamuuliza sio Mchungaji. Maandiko yanasema kuna
watu wameharibika akili zao, watu huwa wanaharibika, Sauli alipoharibika Mungu
alimkataa, chakula hata kama ni kizuri kikiharibika unakitupa. Mtu yeyote
anayeongea vibaya kuhusu kanisa, kuhusu viongozi hafai kuwa rafiki yako. Roho
ya udanganyifu inamfanya mtu hata kama Baba aliwahi kumsaidia lakini hawezi
kuona kama alisaidiwa. Ni udanganyifu kuanza kupambana na mtu aliekuzaa. “Tena shetani akasimama juu ya Israeli, akamshawishi Daudi
kuwahesabu Israeli. Basi Daudi akamwambia Yoabu, na wakuu wa watu,
Nendeni kawahesabu Israeli toka Beer-sheba mpaka Dani; mkanipashe habari, nipate
kujua jumla yao. Naye Yoabu akasema, Bwana na awaongeze watu wake mara
mia hesabu yao ilivyo; lakini, bwana wangu mfalme, si wote watumishi wa bwana
wangu? Mbona basi bwana wangu analitaka neno hili? Mbona awe sababu ya hatia
kwa Israeli? Lakini neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu. Kwa
hiyo Yoabu akaenda zake, akapita kati ya Israeli wote, akafika Yerusalemu “.
1 Mambo ya Nyakati 21:1-4
“Neno hilo likawa baya machoni pa Mungu; kwa hiyo akawapiga
Israeli. Naye Daudi akamwambia Mungu, Nimekosa sana, kwa kuwa nimelifanya
jambo hili; lakini sasa uuondolee mbali, nakusihi, uovu wa mtumwa wako; kwani
nimefanya upumbavu kabisa. Naye Bwana akanena na Gadi, mwonaji wake
Daudi, akisema, Nenda ukanene na Daudi, ukisema, Bwana asema hivi,
Nakuwekea mambo matatu; katika haya ujichagulie moja, nikutendee hilo. Basi
Gadi akamwendea Daudi, akamwambia, Bwana asema hivi, Kubali upendavyo;
miaka mitatu ya njaa; au miezi mitatu kuangamia mbele ya adui zako, ukipatwa na
upanga wa watesi wako; au siku tatu upanga wa Bwana, yaani tauni katika nchi,
na malaika wa Bwana akiharibu kati ya mipaka yote ya Israeli. Haya basi ufikiri
ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma” 1 Mambo ya Nyakati 21:7-12
Shetani
akitaka kuleta uharibifu kwa mtu anamfanya mtu aone jambo baya aone jema, baada
ya kufanya uharibifu unagundua kuwa umefanya jambo la baya. Mashetani ya
kudangaya unaweza kuyazuia, unaweza kuyafunga. Ukidanganyika hata huu ujumbe
unaona ni wa uongo, mambo ya kweli unaona ya uongo, mambo ya uongo unaona ni ya
kweli.
“Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye
ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. Akamshika yule
joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya
mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe
muda mchache. Na hiyo miaka elfu
itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; naye atatoka
kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu,
kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. Wakapanda
juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa.
Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala”. Ufunuo 20:1-3,7-9
Shetani akifungwa hawezi kudanganya japokuwa huwezi kumfunga shetani mwenyewe kwa sababu muda wake bado ila mapepo yake unaweza kuyafunga. Ili upigane na mtu lazima uone kwanza mnalingana, akija Mandonga hamuwezi kupigana nae kwa sababu sio saizi yako. Kupigana na mwenye mamlaka ni lazima ujiinue kwanza ila ni kazi ya shetani anakudanganya. Omba kumfunga mdanganyifu, roho iliyotumwa, mashetani waliotumwa, huwafunga wafalme wao kwa minyororo ya chuma AMEN.
0 Comments