UFUFUO
NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL.
IBADA
YA JUMAPILI 7th MAY,2023.
ASKOFU
BARAKA THOMAS TEGGE.
SOMO:
USIOGOPE WALIO PAMOJA NA WEWE NI WENGI KULIKO WALIO NA PAMOJA NA ADUI.
Maisha
ya duniani yana watu wanaokupenda nawaokuwazia mema ukioa wanafurahi, ukipata
mimba wanafurahi lakini pia maisha kuna watu ukipata vitu wana kasirika
ukijenga, ukioa, ukichumbiwa wanachukia, pia wanafurahi ukiaribikiwa. Usidhani
kila mtu atakupenda hata uwe muovu vipi kuna watu watakupenda hata uwe mwema
vipi kuna watu watakuchukia. Nani anamfahamu mtu mmoja mwovu? Hata mimi
namfahamu mtu mmoja alikuwa na kikundi cha kigaidi anawaongoza watu alikuwa akipanga
mipango anawafundisha watu wake wanavaa mabomu wanaenda mahali wanajilipua
wanauwa watu maelefu. Nilidhania akifa watu watafurahi, lakini alipokufa watu
wakaandamana namfahamu alikuwa anaishi kule Iraq. Ameuwa watu wengi sana ila
siku alipouwawa watu wakaandamana watu wakakasirika ni muovu ila watu wanampenda,
unaweza kuwa mwema ila watu wakachukia wakasema usulubiwe. Kabla Yesu kusulubiwa
ilipigwa kura kati ya Yesu na Barba. Pilato akaitisha uchaguzi kuna wagombea
wawili wa kifo na msalaba ule pale. Kuna Yesu wa Nazareth muhubiri wa injili,
mponyaji, mfufua watu ana maneno yamejaa neema anasaidia watu hajawahi kumlaani
mtu hata watu walipomuita ana mapepo aliwasamehe hajawahi kumtendea jambo baya
mtu. Barba ni muuwaji, unahisi kati yao nani alitakiwa kupigiwa kura ya kufa?
Yesu alipigiwa kura ya kufa asulubiwe, Pilato akawauliza anakosea nini,
wakasema sio suala la kosa yeye afe tu sio kwamba amekosea kitu, furaha yetu akiwa
amesulubiwa ndio furaha yetu. Pilato akasema yeye ni mtawala na kuna sheria na
anaruhusiwa kuuwa ila wenye makosa, niambieni kosa lake nikimuhuku kifo niwe na
uthibitisho kwamba mimi Pilato nimeagiza Yesu wa Nazareth ameuwawa kwa kosa
hili na hili, wakasema sio suala la makosa ,Pilato akanawa mikono.
Katika
binadamu hatari sana ni wanadamu, Yesu alitakiwa aishi miaka mingi lakini sio
hivyo, nataka ujue kuanzia leo wote wanaokupiga vita kuna walioupande wao na
wote wanaokurufahia kuna walio upande wao, hakuna aliye katikati asiyepamoja
nami yu kinyume nami. Asiyekupenda anakuchukia huwezi kunipenda na kunichukia. Usiogope
walio kinyume chako maana walio pamoja na wewe ni wengi kuliko walio pamoja na
wao. Kuna mambo yanaonekana hayawezekani kwa kiwango kadri unavyokuwa kiroho
unagundua kuna mambo yanwezekana kwasababu ushajua yote yanawezekana, sasa
kanisani anakuja mtu aliyeokoka leo, jana, mwaka wote wako hapa inabidi
ufundishe wote wakuelewe ndio maana Mungu lazima awe ili kila mtu aelewe.
“Basi, mfalme wa Shamu alikuwa akifanya vita na Israeli.
Akafanya mashauri na watumishi wake, akasema, Kituo changu kitakuwapo mahali
fulani. Yule mtu wa Mungu akapeleka habari kwa mfalme wa Israeli,
kusema, Jihadhari, usipite mahali fulani; kwa sababu ndiko wanakoshukia Washami.
Mfalme wa Israeli akapeleka watu mpaka mahali pale alipoambiwa na yule mtu wa
Mungu, na kuhadharishwa; akajiokoa nafsi yake, si mara moja, wala si mara mbili.
Basi mfalme wa Shamu moyo wake ukamfadhaika sana kwa ajili ya jambo hili;
akawaita watumishi wake, akawaambia, Je! Hamtanionyesha, ni mtu yupi miongoni
mwenu aliye upande wa mfalme wa Israeli? 2 Wafalme 6:8-19
Mfalme
anapata picha kuwa kuna wafanyakazi ambao hawako upande wake, hata wewe unaweza
kuwa na mtu au rafiki una mwambia siri zako halafu baadae unazisikia upande wa
pili. Mfalme wa shamu anaulizia mipango wa vita anapanga na watu wake inakuwa
je mfalme wa Israel kila akienda anamkuta, ingekuwa ni mara moja au mbili
ningesema ni bahati. “Mmojawapo wa watumishi
wake akasema, La, bwana wangu, mfalme; lakini Elisha, yule nabii aliye katika
Israeli, humwambia mfalme wa Israeli maneno uyanenayo katika chumba chako cha
kulala. Akasema, Enendeni, mkamwangalie aliko, nipate kupeleka watu
kwenda kumchukua.Akaambiwa ya kwamba, Tazama, yuko Dothani. Kwa hiyo
akapeleka huko farasi, na magari, na jeshi kubwa; wakafika usiku, wakauzingira
mji ule pande zote. Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa
Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na
magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu,
tufanyeje? Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko
wale walio pamoja nao. Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi,
mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye
akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto
yaliyomzunguka Elisha pande zote. Na walipomtelemkia Elisha akamwomba
Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu
sawasawa na neno la Elisha. Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu
sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka
Samaria”. 2 Wafalme 6:8-19
Elisha
hakuitaji kwenda kuwaona ili achungulie wako wangapi akasema haijalishi wako
wengi kiasi gani ila najua walio upande wetu ni wengi kuliko walio upande wao,
hapa nataka unielewe hapa, Elishi haongei Habari za watu walio mzunguka, farasi
walionao, haongeichochote kuhusu hawa adui waliotumwa na mfalme wa Shamu,
akijilinganisha yeye na wao ataogopa na hilo ndio kosa alifanya Gehazi. Elisha
akipima wenzake na wenzao adui wanzake niwengi kuliko wenzao. Kuna mambo
tukiyasoma kwenye biblia tunahisi hivi watu wazamani walikuwa sio wakawaida,
ukimsikia Eliya, Elisha, Daudi, Daniel ni watu hatari, hapana walikuwa watu
kama sisi. Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi ni watu wakawaida ila
ni watu waliomuamini Mung una maneno yake, sitaki udhani wala kufikiri kwamba
Elisha aliona rohoni halafu akaona jeshi, hapana aliamini kile Mungu amesema
alikuwa anasoma biblia ya wakati ule ni ile ambayo kitabu hiki cha wafalme
hakikuwepo, maana hii imeandikwa baadae sana unaelezea habari ya mtu tayari ashafanya
, zamani biblia ilikuwa na vitabu vitano tu, hakuna Waefeso, wala Mathayo hapa
kuna Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati . Elisha alisoma ile
kumbukumbu ya torati 20 inasema utokapo kwenda vitani ukaona adui zako ni wengi
kuliko wewe na magari yao ni mengi kuliko yako usiwaogope, ukitoka ukaona kuna
watu wengi kinyume chako wana elimu kubwa
kuliko yako, uzoefu wakazi kuliko wewe, wana vifaru vikubwa kuliko wewe
usiwaogope. Huwa nasema tusipoamini maneno ya Mungu, basi Mungu hana msaada
kwetu hawezi kutusaidia maana Mungu akitaka kukusaidia hakupi fedha ila
hulituma neno lake. Hata leo amekuja akusaidie ametuma neno usiogope. “ Utokapo kwenda vitani kupigana na adui zako, na kuona
farasi, na magari, na watu wengi kuliko wewe, usiwaogope; kwa kuwa Bwana Mungu
wako, yu pamoja nawe, aliyekukweza kutoka nchi ya Misri. Na iwe,
msongeapo mapiganoni, kuhani na akaribie na kusema na watu, awaambie,
Sikizeni, enyi Israeli, hivi leo mwasongea mapiganoni juu ya adui zenu mioyo
yenu na isizime; msiche, wala msiteteme, wala msiingiwe na hofu kwa ajili ya
wao; kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania
juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi”.Kumbukumbu la Torati 20: 1-4.
Maisha ya duniani ni Maisha ya vita kila siku unapotoka kwenda kazini au
biasharani lazima ukumbuke kuwa unatoka kwenda vitani.
Vita
haimanishi utakutana na mtu akuambie tupigane vita, wewe siuna Yesu yeye anamapepo mpigane vita, hapana Maisha yetu
ni maisha ya vita unapoamka asubuhi ukumbuke unatoka kwenda vitani. Ni nani
anataka kwenda vitani halafu afe, unahisi hauna vita uko kazini maana unafanya kazi
Dawasco maana unawasaidia watu kupata maji vita inatoka wapi?
Ukiwa
na akili kila siku ni vita hutatoka bila kujipanga, kabla hujatoka nyumbani ni
lazima unene kwa lugha hata lisaa limoja, mkiomba kila wakati katika roho hiyo
ni silaha ya vita, nena angalau lisaa limoja halafu nenda kazini. Kwasababu
wenzako nao wanatoka wanakuja vitani usipofanya hivyo utashangaa boss wako
anakuchukia na wewe nimfanyakazi bora, ni kwasababu wenzio wanatoka wakienda
vitani, wana ufahamu huo ndio maana hawaanzi biashara bila kuwa na ufahamu huo
hata akienda dukani kuna kitu anachoma na asubuhi ameomba na moja wapo ya
maombi yao ni kuwalaza makafri na wewe ni mmojawapo wa kafri.
Wewe
unaamka saa mbili unaanza kukimbia kuwahi mwendokasi na ulilala saa mbili jana ndio maana una
umaskini wakutosha. Biblia inasema mtu anaye lala sana naumaskini wa kutosha.
Siku anachelewa kulala alikuwa anaangalia movie au anachat mambo ya kijinga na
mchumba wake. Anakesha anachat na alisema hawezi kuja mkesha kwasababu kesho
anaenda kazi lakini mpaka mkesha unaisha yupo anachat tu hajalala. Haiwezekani
ulale saa 10 alfajiri halafu asubuhi uamke uombe atamka saa mbili asubuhi na
kuwahi mwendokasi kuwahi ofisini. Ni hatari kuwa vitani na usijue uko vitani
kila ambacho unacho kuna ambaye anakitaka hata kama ni chako kihalali kuna mtu
anataka. Hata kama mumeo ni Sherphed shetani anazungukazunguka akimtafuta
ammeze, anasema Yesu shetani anawataka mitume, ana kazi gani na mitume je anataka
kufungua huduma, ila Yesu anasema shetani anawataka ili awapepete kama ngano,
nini maana ya kupepeptwa ni kile kili mpta petro baada ya kuppetwa ni yue
aliyesema wewe ni mana wa mungu aliyehai alipopepetwa akasema simjui mtu huyu.
Mume alipokuoa siku ya kwanza nilipokuona ndio siku niliyoanza kuishi wewe ndio
furaha ya maisha yangu na ibarikiwe siku ambayo mama yako alitunga mimba,
ibarikiwe siku ulipoitwa Happy na siku mama yako aliyokuzaa hapo bado hajapepetwa.
Ndio maana vijana wasiku hizi nirahisi kukupetwa. Wamtumainia Bwana ni kama
mlima wadumu hawaondoshwi, unafanya mizaha na mambo ya msingi wa maisha huna muda
wa kuombe na ibada.
Hii
ya kujiona watu wakawaida ila wenzetu hawako hivyo kila siku kabla ya kwenda kazini
lazima aombe hata mvua inyeshe iwe radi au laah. Acha mizaha na mambo ambayo ni
ngome yetu. Bwana ni ngome yetu na nuru yetu tumuogope nani watenda mabaya
waliponikaribia wanile nyama yangu watesi wangu walijikwaa wakaanguka. Wanakukaribia
ili wale nyama yako maana mume wako ni nyama katika nyama yako, na watesi
wanapenda nyama yako.
Shetani
huwa anazunguka zunguka na alipomuona Ayubu, alipomtaka ndani ya siku moja
Ayubu hana mali tena, hana watoto, mali wala ndoa imara ila ametikiswa. Wewe
huna muda kanisani mvua ikinyesha huendi ila kazini unaenda. Msikitini wanaenda
kusali Allah yukopale huwezi kuchat mbele yake ila mbele ya Jehovah Nisi unachat,
yeye anaongea na wewe unaongea na simu. Nawapenda waislamu maana wanajua maisha
yao yanamuhitaji sana mungu wao akiwaambia waombe mara tano kwa siku awe maskini
au Tajiri, ana pesa au hana pesa, amekula au hajala. Ila sisi hatujui unampenda
Mungu au ni shida tu unalala kanisani, siku ukipata kazi ukalipwa laki tatu na
ukapanga chumba Bonyokwa na kina feni atakuambia kanisani kuna joto. Lakini
wenzetu waislamu wanakaa chini na hawabaguani na wanaongozwa na imamu hajasoma
shule na hawamuongelei maana ni mtu wa rohoni, akiwa na kazi hawezi kukuajiri
wewe maana ni kafri, wanapenda wanakaa pamoja
wanadumu katika fundisho la imamu.
Sisi
vitu vidogo ambavyo tumevibatiza ni mafanikio na sio mafanikio, yaani
tunadanganyika sana na vitu vya kidunia yaani mtu akijenga tu kijumba akinunua
gari ashakuwa mtu mkubwa sana. Hutakikuelekezwa na kiongozi wako kwasababu
unamuona amependa mwendokasi amebanana na wewe uko kwenye gari yako. Akisema
tusome neno la sadaka unasema moyoni huna pesa ndio maana unaongea suala la
sadaka. Kuna watu wanaongea kinyume na mhubiri ni vile tu hajapewa kipaza
sauti. Wanaongea zaka ni hawa wasio na pesa, nitoe kanisani million moja ya
nini, yaani vitu vidogo unaona vikubwa hutaki kuonywa, kukaripiwa ili mtu
akukaripie lazima uwe china yake kama mnalingana hapana hii ndio leoalikuwa
nayo Sauli, maana alijikuza akawa kama Samweli. Samweli akimwambia hivi nay eye
anaongea kinyume chake anamrekebisha, kuwa tumeona hivi tutunze kondoo wengine
kwa ajili yadhabihu, Sauli umehasi sauti ya Bwana ila akakata na kusema
nimetii.
Ukiwa
mkubwa baba yako na mama yako hawezi kukuonya sababu ushakuwa mkubwa huwezi
kuonywa unakuwa mkali sana sababu una wagerasi, hata mambo watu wanakuzidi
wanakuonya unakata kusikiliza, umekuwa mkubwa mtu yeye yote anayekuzidi umri
hata kama unamzidi mfanikio anakuzidi maarifa kwahiyo anapokuambia jambo
msikilize.
Mtu
kwenye ndoa miaka 30 ameona mengi wewe una uchumba wa siku 30 acha ubishi,
kwakuwaulisoma kitabu cha mambo 7 ya kuwa na ndoa yenye furaha. Kwahiyo wenzetu
Maisha kwao ni vita ndio maana hawawezi kupuuzia, ikifika muda wa ibada hata
kama umekujakununua bidhaa za duka zima hata kama una billion moja atakwambia
muda wa swala lakama Allah amenipangia hiyo riziki nitaikuta. Kama sio riziki
yangu sio riziki kisicho riziki hakiliki anafunga duka mbele yako. Ila wewe
mkristo unasema Pastor muda ule ule wa ibada wateja wakafuruka bwana akaleta
wateja kama mafuriko. Hii ni vita na niya rohoni hata kama amesoma bado kuna
vitu vya rohoni anafanya hata kaka ni bilionea.
Mo
Dewji alikuwa anahojiwa atoe ratiba yake kwa siku, akasema siku yake inaanza
saa 11 kwa saa nzima ya sala, haombiili apate chakula cha mchana maana anacho ,
akienda kazini ile saa saba msikitini, jioni pia msikitini analala saa nne
usiku. Nataka tuamini maisha ni vita popote
ulipo uwe bisharani, gengeni ni vita utaona wenzako ni wengi wanafanya vile
vile kama wewe. Usiwaogope maana mimi Bwana naenda mbele zako inatakiwa Bwana
anende mbele yako ili usiwaogope na ili Bwana aende mbele yako kuna mambo
natakiwa kuyafanya. Maana wenzako wanao aliyepamoja nao maana kuna jambo
wamefanya asubuhi maana hakuna mambo yaroho ambayo wenzako wanafanya na
yasijibiwe. Maombi yoyote kwa Mungu yeyote huachilia viumbe wa rohoni kuja
kuyatekeleza kwa hiyo hawa viumbe waoachiliwa ndio hao wapo Pamoja nawewe na
wao.
Watu
wengi wanadhania maombi ya watu wasio na Mungu hayana maana hapana yana maana,
maana yanawavuta watu wa rohoni kwa upande wao, mtu yeyote anayeomba ujue
anafanya shughuli za rohoni na anaongea na roho nazinachiliwa kuna mashetani yanakuja
kumsaidia mtu maana amesema maneno kila siku asubuhi. Yeye ndio maana ana akili
ambayo haitokani na elimu yake, huyu mtu ukiwa nae kwenye biashara moja na wewe
hujafanya ya rohoni huwezi mshinda maana anao walioupande wake na wewe hauna
huwezi kufanikiwa. Maisha ni ya rohoni, utokapo kwenda kazini, biashara,
shuleni hata shuleni pia, ndio maana kuna mtu akifika shuleni haoni ubao mwalimu
akiwa anafundisha anasikia anaimbiwa nyimbo ni vita. Unaweza kuona unafanya
biashara na watu wanakupiga vita inaonekana wanamuunganiko mkubwa, mitaji
mikubwa kuliko wewe usiogope maana hawawezi kukushinda maana huwezi kumshinda
mtu mwenye Mungu kama anajua chakufanya. Hata kama una mtaji kidogo maana
atainuka hatua kwa hatua maana Bwana mwenyewe anatoka mbele yake, huwezi mshinda
mwanamke aliye na Mungu kwenye ndoa yake maana atamlinda mume wake tazama
naumba jambo jipya mwanamke atamlinda mume wake. Huwezi mlinda mume kwakukagua
simu yake ila kwa maombi. Bwana asipoulinda mji walindao wanakesha bure. Bwana
ni mlinzi ongea nae akulindie wanao, Isaka anataka kumlinda Yakobo anaongea na
Mungu alaaniwe mtu yeyote ambaye atamlaani Yakobo halafu Laban akawaza kumlaani
akatokewa na Mungu wa Isaka anamwambia aache hayo mambo. Laban akamwambia nina
uwezo wa kukulaani ila Mungu wa baba yako amenionya nitakufa.
Kama
unapenda kifo kabla ya wakati, vidonda vya tumbo, msongo wa mawazo basi mfuatilie
mume wako kila hatua ametoka mkesha anaongea na nani akiwa kanisani, basi
utaishi muda mrefu lazima umuamini Mungu anaweza kufanya mambo yote aliyokuahidi.
Mungu anaweza kutoka mbele yako akawalinda wanao, mume wako anaweza kulinda Zaidi
yako maana niende wapi nijiepushe na uso wa Bwana, wewe huwezi kwenda sehemu
zote ila Bwana anaweza.
Hawa
watu wametoka kwenda kumkamata Elisha, ishu ni nani yuko nao na sisi nani yupo
nasi, akamwambia Gehazi usiogope endelea na kazi zako. Ili vionekane kwa macho
ya nyama ilibidi Elisha aombe ili huyu Gehazi aone, Mungu akamfungua macho
Gehazi akaona waliowazunguka wamewazunguka ina maana wapo walipamoja na sisi,
Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu msaada uonekana wakati wa matesi kwetu Mungu
hapendi kumtesa mtu, mpenzi ufanikiwe na kuwa na afya kama vile roho yako ifanikiwavyo
kwenye kazi ufanikiwe kwenye biashara masomo ufanikiwe. Haya maisha huwezi
kufanikiwa mpaka Mungu akusaidie, huwezi fanikiwa popote kama Mungu hakusaidi
na Mungu amekupatia msaada na wako walio pamoja na wewe ni malizie kwa kusema
kwanini watu wa Mungu kuna wakati wanashindwa kama ni kweli wako wengi walio
rohoni zaidi ya wale walio na adui zako ni kwanini?
Kwa sababu; Kukosa
maarifa. Maarifa hayo ni kutokujua kuna walioupande wetu viumbe wa rohoni kile
ambacho unachoni. Unakuwa kama Gehazi, Elisha hakuomba ili waje ila aliomba
wadhihirishwe ili Gehazi awaone maana alipatwa hofu. Bwana yuko Pamoja na wewe
apekupeleka msaada yuko na wewe.
“Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe
umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa
kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako”. Hosea
4:6,
Mambo
gani inabidi ufanye ili viumbe hao wajue cha kufanya, viumbe wa rohoni wa giza
au wa nuru wanafanya kazi mpaka waagizwe. Viumbe wa rohoni wa nuru au wa giza
hutenda kazi mtu mwenye mamlaka akiongea maneno. Mashetani hawawezi ingia mtu
mpaka watumwe. “Na tazama, mmoja wao waliokuwa
pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa
Kuhani Mkuu, akamkata sikio. Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako
mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga. Ama
wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi
ya majeshi kumi na mawili ya malaika? Yatatimizwaje basi maandiko, ya
kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri?”. Mathayo 26:51-54
Jeshini
hawawezi kufanya kazi bila kufuata amri hata kama kuna vita imetoke Nchi ya
Kenya hawawezi kujiamria kwenda mpaka waambiwe, hata wewe una wanajeshi wa
rohoni lakini hawawezi kufanya kazi mpaka uwaagize.
“Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko
Refidimu. Musa akamwambia Yoshua, Tuchagulie watu, ukatoke upigane na
Waamaleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa
nayo mkononi mwangu. Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia,
akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima.
Ikawa, Musa alipouinua mkono wake, Israeli walishinda; na alipoushusha mkono
wake, Amaleki walishinda. Lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; basi
wakatwaa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza
mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika
hata jua lilipokuchwa. Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa
ukali wa upanga”. Kutoka 17:8-13
Kipi hutokea ukianza
kuomba na kipi hutokea usipoomba?
Kuna
mambo usipofanya unapoteza vita hata kama walio pamoja na wewe ni wengi. Malaika
uliopewa wanafanya kazi ukianza kuomba, Kornelio alikuwa anaomba Malaika akaja,
Danieli alikuwa anaomba Malaika akaja. Maelekezo ya Mungu ya dakika mbili
yanaweza kubadilisha maisha yako yote. Hutakiwi kushindwa kwenye jambo lolote
kwenye maisha kwa sababu walio pamoja na wewe ni wengi.
0 Comments