UFUFUO
NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL.
IBADA
YA JUMAPILI 14th MAY 2023.
ASKOFU
BARAKA THOMAS TEGGE.
SOMO: USIOGOPE
WALIO PAMOJA NA WEWE NI WENGI KULIKO WALIO NA
PAMOJA
NA ADUI
Sisi watu wa Mungu ushindi wetu hutegemea Mungu wetu sio elimu zetu, ushindi wako wakila eneo la Maisha unamtegemea yeye. Mungu ameisha amua ushinde wewe ni mshindi na zaidi ya mshindi, hutakiwi kushindwa kabisa ukianza biashara, ndoa, masomo hutakiwi kushindwa kabisa, maana wako wengi walio pamoja na wewe, na upinzani ambao unakutana nao ni saizi yako, hutakiwi kulalamika au kulaumu au kulia unatakiwa uwakabili ikiwa unafahamu unao walio upande wako na ni wengi kuliko walio upande wawanaokupiga vita. Kuna mambo ambayo usipo yaelewa hata kama una msaada ule msaada haukusaidii. Shetani asingependa uelewe na atakushinda maana huelewi ikiwa kimsingi hatakiwi kukushinda. Imeandikwa wala hatukosi kuzifahamu fikra zake shetani asije akapata kutushinda maana anapata ushindi kwa watu wa Mungu wasipojua baadhi ya vitu.
Hao
walio upande wako ni wengi na wana nguvu za kuwashinda walio upande wa adui
zako. Unapopigwa vita usiwaone wanaokupiga vita bali uwaone wale waliopamoja
nao, iwe ni vita kwenye biashara, masomo, watoto, ndoa usiwaone watu ila ona
walio pamoja nao ambao una amri juu yao na una amri juu ya wakubwa wao.
Akawaita
wanafunzi wake akawapa amri juu ya pepo wa chafu ili wawatoe na wewe una amri
ya kuwatoa, walio pamoja na adui zako ni pepo wachafu na wewe una amri ya kuwatoa.
Akawaita wanafunzi akawapa mamlaka ya kukanyaga nguvu zote, nyoka na hakuna cha
kuwadhuru na wewe una mamlaka ya kuwa kanyaga, huwezi kumshinda mtu mwenye mamlaka.
Mimi huwezi ni shinda hapa nina mamlaka. Nikija kwako mimi sio askofu nakuwa
kama raia tu siwezi kukushinda una mamlaka na nikikushinda labda uwe huna
maarifa.
Huwezi
kushindwa na mtu una mamlaka juu yake. Una mamlaka ya kuwashinda walio pamoja
na adui zako wanao wavuvia mawazo kinyume chako, mchawi una amri ya kumshinda
maana una amri ya kumshinda boss wao mkubwa ambaye ni shetani una amri ya
kukanyanga nguvu zake zote. Jambo lolote ukilianza hutakiwi kushindwa chochote.
Na hapana kitu kitakacho wadhuru.
Una
mamlaka ya kuwashinda walio pamoja na adui zako maana una mamlaka ya kukanyaga
nguvu zao zote, kama Mungu asemacho ni kweli basi unayo mamlaka ya kumkanyaga
boss wao wachawi ambaye ni shetani. Ukiamua kumkanyaga una mkanyaga na hapana
kitu kitakacho wadhuru ila kuna wakati unapata madhara kwa sababu ni kutokuwa
na maarifa.
Kuna
mtu hajui wapo walio upande wake na tuna mamlaka ya wale walio upande wa adui,
sisi tuna walio upande wetu na wao wanao walio upande wao. Na aliye upande wetu
ni mkuu kuliko wote na anayaweza yote na hakuna gumu la kumshinda ndiye
aliyeumba mbingu na nchi yuko pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja nao.
Yeye
anayesikia neno lakini halitendi ni mpumbavu amesikia ana amri ila amri
haitumii kwahiyo anaonewa kwa sababu hatendi na una mamlaka ya kumshambulia
shetani, Elisha anaye walio upande wake na wamemzunguka kwasababu walio upande
wao wamemwambia. Adui anafahamu mipango yako unako elekea wanafahamu umechumbia
kisirisiri na wao wanafahamu na wanamfahamu sana mchumba wako. Kwa Pastor Msimbe
umegoma kujaa form ila wao wanafahamu uchumba wako na maongezi yenu yote
wanafahamu, wajue wasijue aliyepamoja na wewe ni mkuu kuliko aliyepamoja na
adui zako usiogope.
Kuwa
na Mungu haimanishi hautapigwa na changamoto hazitakuwepo, kuwa nae ndio hasa
itakuletea changamoto, lazima ujue kukabiliana na changamoto zinazokuja kwako na
ukiwa na Mungu usidhanie ukichumbiwa kufuata utaratibu wa Mungu ndio hapana
upinzani, Yesu anawaambiwa wanafunzi tuvuke kwenda ng`ambo, kuna kitu amevuviwa
kufanya ng`ambo mawazo ya kuvuka ng`ambo sio ya wanafunzi wa Yesu ila ni ya Yesu
pekee yake ila hapa katikati kuna upinzani na maandiko yanasema wakamchuka vile
vile kama alivyo.
Usiseme
baada ya kuolewa vita imeibuka unadhania sio mapenzi ya Mungu, au kuanza
biashara unakutana na vita, hapo ndipo mahala pekee sasa hayo ndio mapenzi ya Mungu.
Maana vita ijapo nitokea hata hapo nitatumaini, Mungu anategemea upigwe vita.
Mungu anapenda vita anapenda kuona wanae wanapigana na wale wa upande wapili.
Ni kama watoto wanasema mbwa wangu anangata kuliko wako, basi mlete na mbwa
wangu wapigane, akishinda mbwa wako unakuwa na heshima, Mungu nae anataka
aheshimiwe uwavunje vipande vipande adui zako Mungu nae aseme yule ni mwanangu.
Sisi Ufufuo na Uzima hatujawahi kupoteza vita maana baba yetu ni mtu wavita
tangu ujana wake.
Vita
inafundishwa kwa kupigwa vita, una dondoshwa uwanja wa vita , anasema Daudi
Bwana ananifundisha mikono yangu vita, lazima Bwana akufundishe vita maana maisha
yamejaa vita, vita kwenye kila jambo, vita kwenye biashara ulikuwa unauza udaga
ukaona vita ukahamia kwenye biashara ya maharage hata huko kuna vita, ulikuwa
kwenye huduma ukaona vita ukaacha huduma ukaingia kwenye mwanaharakati wa ndoa hata huko kuna vita, hata ukiacha ndoa kuna
vita ya mabinti walioolewa na ambap hawajaolewa kuna vita , pigana vita. Huna
pakwenda jipange pigana. Ni vita kote kote Bwana ndio maana anakufundisha vita.
Kuwa na Mungu haimanishi hakuna vita ila ndio kuna vita haswa. Kama ni siasa kuna
vita, masomo kuna vita. “Siku ile kulipokuwa
jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng'ambo. Wakauacha mkutano,
wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja
naye. Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata
kikaanza kujaa maji. Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu
ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?
Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo
ukakoma, kukawa shwari kuu”. Marko 4:35-39
Vita
ipo kwenye chombo ambacho Yesu yupo, kimepigwa na upepo na kimejaa maji.
Yesu siku zote alikuwa anayafanya mapenzi ya Mungu asilimia 100 na kila
alichofanya Mungu alimuongoza, na wewe unavuka ng`ambo ya huduma, ndoa,
biashara kwenye mchakato wakuvuka chombo kinajaa maji, wavuvi wanafahamu chombo
kikijaa maji basi kinaanza kuzama, maji yakianza kuingia basi kuna shida.
Walianza
safari wakiwa na mwokozi na pengine walikuwa wakisifu lakini ghafla upepo huo.
Wakamlalamikia anasinzia kwenye safari kama ile. Nafahamu watu wawili walilala
katikati ya upepo, ambao ni Yesu na wapili ni Yona. Yesu aliwakemea maana
alitegemea wangekabiliana na usumbufu wa ile hali kuwauliza iko wapi imani yenu,”
Akawaambia Mbona mmekuwa waoga? Hamna Imani bado?” Marko 4:40, alitegemea
wangeukemea upepo maana ameisha wafundisha na amewapa amri juu ya upepo.
Unaenda
mahali umetokea upinzani na Yesu unaye kwenye chombo chako , hiki ndicho Yesu
anatarajia ufanye maana una imani, na mwenye Imani amuhamshi Yesu ila ana ukemea
upepo. Huu upepo ni shetani amejigeuza kuwa upepo maana ulipo kemewa ukasikia
na ukafanya kitu ulichoambiwa ufanye. Ni mtu asiye na mwili yuko nyuma ya upepo,
safari ingeishia hapo kwa ajili ya upepo maana alikuwa anaelekea ng`ambo kule
kuna mtu ana mapepo, Yesu anaenda kumfungua na shetani anajua Yesu akienda amepoteza
mtu ndio maana shetani analeta upepo, ila Mungu ametupa amri.
Ina
maana wangekaa kimya wasimuamshe Yesu wangezama wakafa ila Yesu asingekufa ,
Yohana Yakobo na Andrea wangeogelea Lawi
na mashaka nae na Yuda angekuwa wakwanza
kufa . Ila Yesu anataka kuwa fundisha ikitokea changamoto wanafunzi wake wasemeshaa
upepo maana nyuma yake kuna mtu asiye na mwili. Mambo ya kujiliza liza na
kupenda kuonewa huruma hapana, jifunze kusemesha mambo.
Sema
upepo unaopiga uchumba wangu tulia iwe shari kuu nivuke nikaolewe, acha maneno
mengi neno la Kristo lijae moyoni. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye
nguvu, kwa msaada wa Bwana nafatia jeshi kwa msaada wa Bwana naruka ukuta, kwa Imani
walifukuza majeshi na wafukuza, wakimbize hao ndio maneno yakuongea katikati ya
changamoto, ukiamka semesha ni biashara semesha ndoa wanakusikia mwenye amri
asipoongea mambo hayatokei, mwenye mamlaka huwa anasema. Yale mambo
yakujihurumia ni mtu wa mjini mwenye elimu shetani haheshimu elimu yako.
Mambo
yakujifanya maombi huhitaji kwasababu una mali una kila kitu, sikiliza shetani
atakapokuja kutembelea atafuta vyote una muhitaji Mungu maana shetani
alimpoteza billionea ndani ya siku moja. Yasemeshe matukio maana nyuma kuna
aliyepamoja nawe. Unapoona mtu ana Sali na kunena kwa lugha unamuona kama hana
kitu ana shida ndio maana anasali. Wakiitwa walifanikiwa tutaenda walioenda
shule tutaenda na bado tuna mtumikia Mungu. Msaada wa Bwana lazima uongee ndipo
atafanya kazi. Unaweza kupambana mwenyewe kwenye vita yako ila umejidekeza.
Unayaweza mambo yote katika yeye atutiaye nguvu kila uumbaji una sauti ya
kusikia.
Unaweza kuwa unakaa kanisani na umuelewi muhubiri hizo ni nguvu za shetani ana kuwekea upinzani, mambo yote ambayo yanaonekana ni magumu, unataka kuanza biashara kwenda china, anza kuongea waambie waachie njia au mambo kwenye familia ya ndoa mna changamoto umekaa na mkeo unaongea nae muda lakini hakuelewi ukimrekebsha ni mkali mno leo isemeshe ndoa, wapige, vunja haribu uikoe ndoa yako. Kuna nguvu rohoni inakujengea chukia na watu ambao ni wa muhimu sana kwako, inakutenge na watu wako wa muhimu kama Sauli anakuwa na vita na Daudi ambaye anampigia kinanda roho chafu ina muondokea ila anampiga vita kama mimi unakuwa na vita wakati nakuhubiria hayo ni mashetani kama mgerasi, mtu anakuchukia bila sababu ila sio yeye ni mashetani, Mungu akitaka kukusaidia anakutumia mtu.
Anasema
ewe Yerusalemu uwauwae manabii na wale walitumwa kwako mara ngapi nimetaka
kukuweka chini yambawa zangu kama kuku awekavyo vifaranga vyake ila hukutaka kwasababu
ya hiyo nyumba yako imeachwa mkiwa, ni mtu wa makasiriko, kuchukia maana anayetumwa
umemkasirikia huwezi kupokea kutoka kwa Mungu ikiwa aliyetumwa na Mungu
ujampokea. Tuombe kwa tusemeshe kemea matukio, biashara, safari, ndoa ambayo
haiendi kwa jina la Yesu na baada ya
hapo unaamuru iweje vile utakavyo. AMEN.
0 Comments