UFUFUO
NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL
IBADA
YA JUMAPILI 11 FEBRUARI 2024
ASKOFU
DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: MUNGU
HUTUMIA WATU KUINUA WATU
Mungu akitaka kufanya jambo lolote huwa anaanza na mtu, ndio maana Tanzania imeanza na mtu yaani Baba wa Taifa, hivyo ndivyo kwa nchi nyingine kama Kenya. Hata taasisi kubwa duniani kama Bill Gates Foundation na Mwalimu Nyerere Foundation zinaanza na mtu.
Watu ni wa muhimu kuliko vitu, vitu vyote vimefichwa ndani ya watu. Kesho imeficha matukio mengi usiyotarijia hata yule anayeonekana dhaifu ndani yake anaweza kuwa amebeba kitu kikubwa iwe taasisi, kampuni, biashara, huduma nk.
Mungu huinua watu kupitia watu. Mungu akiamua kufanya jambo hutumia watu, hata kupitia watu wale wanaoonekana wa kawaida na dhaifu. Kupitia watu Mungu huinua watu, Hata Yohana alikwenda mbele za Yesu ambaye ni Mungu ili aitengeneze njia yake.
“Mwanzo
wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. Kama ilivyoandikwa katika nabii
Isaya, Tazama, Namtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia
yako. Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni
mapito yake. Yohana alitokea, akibatiza nyikani, na kuuhubiri ubatizo wa toba
liletalo ondoleo la dhambi. Wakamwendea nchi yote ya Uyahudi, nao wa
Yerusalemu wote, wakabatizwa katika mto wa Yordani, wakiziungama dhambi
zao. Na Yohana alikuwa amevaa singa za ngamia na mshipi wa ngozi kiunoni
mwake, akala nzige na asali ya mwitu. Akahubiri akisema, Yuaja nyuma yangu
aliye na nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuinama na kuilegeza gidamu
ya viatu vyake. Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho
Mtakatifu.” Marko 1:1-8.
Hakuna
mtu ni zaidi na hakuna mtu ambaye si kitu bali kila mtu ni sahihi kwenye eneo
alilotumwa. Wewe umetumwa na Mungu kufanya jambo la kiuchumi, jambo la kisiasa
nk. unapokuwa kwenye eneo hilo Mungu anafanya kazi kupitia wewe, mikono yake
inakuwa yako, akili yake inakuwa yako, jambo lolote unalotenda inakuwa ni Mungu
anafanya.
Hakuna siku Mungu atashuka kukusaidia au kukubeba, Mungu tayari yupo ndani yako, wewe fuata ile shauku yako na mtu ambaye Mungu tayari amemuweka kwa ajili yako.
Kutoka hapo ulipo unahitaji mtu akutaje, Sio wenye mbio ndio washindae, sio wenye bidii ndio wafanikiwao nk. Wakati na bahati huwapata wote.
“Nikarudi,
na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala
si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si
watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini
wakati na bahati huwapata wote.” Mhubiri 9:11.
Lazima awepo mtu wa kukutaja mbele za wakuu ili uinuke kutoka pale ulipo. Yusufu alifanya jambo ambalo lilifanya atajwe mbele ya Farao. Ingewezekana Mungu amtoa Yusufu
kutoka gerezani mpaka kuwa waziri mkuu, lakini ilibidi amtumie mtu kumuinua
Yusufu.
“Basi
mkuu wa wanyweshaji akamwambia Farao akisema, Nayakumbuka makosa yangu
leo. Farao aliwakasirikia watumwa wake, akanitia nifungwe nyumbani mwa
mkuu wa askari, mimi na mkuu wa waokaji. Tukaota ndoto usiku mmoja, mimi
na yeye; kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake tukaota. Na huko pamoja nasi
palikuwa na kijana; Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari, tukamhadithia, naye
akatufasiria ndoto zetu; akamfasiria kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake. Ikawa,
kama vile alivyotufasiria ndivyo ilivyotokea; mimi nalirudishwa katika kazi
yangu, na yeye alitundikwa.” Mwanzo 41:9-13.
Janga kubwa ni kukosa mtu wa kukutaja hata kama umesoma sana, usipigane kila vita na kila mtu, chagua vita nyingine kuacha zikupite. Ukitoka kutoka pahali pa chini kwenda juu, anainua mtu wa kukutaja mahari, ishi na watu vizuri ili awepo mtu wa kukuinua.
Utimilifu
wa mambo aliyokupangia Mungu kwenye maisha yako, unatimia pale mtu anapokutaja
kwa mtu mkuu. MUNGU ANAANZA NA WATU.
0 Comments