google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MASHETANI KATIKA UZAO WA WANADAMU

UFUFUO NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 18 FEBRUARI 2024
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: MASHETANI KATIKA UZAO WA WANADAMU

“Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.” 1 Yohana 3:10.

Biblia inasema watoto wa Ibilisi ni bayana vivyo hivyo na watoto wa Mungu ni dhahiri. Yesu anasema ukimuona Baba umemuona mwana, kama mtu ni mtoto wa Mungu umemuona Mungu, kama mtu ni mtoto wa Ibilisi umemuona Ibilisi. Ukimuona Baba na mtoto ni wale wale. Yesu anawaita wana wa Ibilisi kama alivyo baba yao. 

“Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.” Yohana 8:44.

Neno Baba maana yake ni asili, mwanzilishi na chanzo, kama Baba alivyo wale anaowazaa wanakuwa kama yeye. Unaweza kukutana na mtu anashindana na wewe kwenye maisha kumbe ni mwana wa Ibilisi.

Yesu anaonyesha tena namna wana na baba ni wamoja; Watu wengine waliwaona watu lakini Yesu aliwaona siyo watu. 

“Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?” Mathayo 23:33.

Hata leo kuna watu wanaoonekana watu lakini asili yao sio ile unayoijua wewe. 

“Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?” Mathayo 3:7.

Tunajifunza kuwa wanaonekana watu lakini kumbe ni mashetani. Mtu kabisa anaonekana mtu kabisa ila kuna uwezekano akawa wa uzao wa shetani, ndiyo maana Yesu anawaita mashetani japo wanaonekana wanadamu.

“Na kama vile ulivyokiona kile chuma kimechanganyika na udongo wa matope, watajichanganya nafsi zao kwa mbegu za wanadamu; lakini hawatashikamana, kama vile chuma kisivyoshikamana na udongo.” Danieli 2:43.

Kila mtu unayemtazama kuna asili anayokuwa katokea. Ibrahimu walipokea wageni ambao walionekana ni wanadamu kabisa lakini hawakuwa wanadamu wa kawaida.

“BWANA akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari. Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako. Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu. Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema. Basi Ibrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate. Ibrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng’ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa. Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala. Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani. Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? BWANA akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo, umecheka. Mwanzo 18:1-15.

Kila mtu alipoumbwa Mungu kamuita kuwa mtu fulani, awe bora kwenye kitu fulani iwe siasa, biashara, elimu nk. Wana wa mashetani wanaona kile kilichokuwa ndani yako wanakuja ili kupindisha hatima yako. Unahitaji macho kuona maana anakuja kama mtu wa kawaida. Wana wa Mungu wanavaa miili vivyo hivyo wana wa Ibilisi wanavaa miili.

“Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la BWANA. Yoshua akapomoka kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake? Huyo amiri wa jeshi la BWANA akamwambia Yoshua, Vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo.” Yoshua 5:13-15.

Wasio watu wana makundi matatu;

  • Mtoto wa dawa - Mama aliyeolewa aliyekaa muda bila mtoto anaenda kutafuta mtoto kwa mganga ambaye anakuja kuzaliwa mtoto kabisa. Watoto wa dawa wanakuwa na shida kweli maana wamezaliwa kutoka kwenye nguvu za giza. Mwili ni wa mtu lakini ndani ni kitu tofauti kabisa. Mtoto wa dawa ametengwa wakfu tangu tumboni mwa mama yake kwa ajili ya makusudi fulani ya uharibifu. 
  • Shetani (roho) anavaa mwili - Shetani ambaye ni roho kabisa anavaa mwili na kufanya kazi za uharibifu duniani. 
  • Mapenzi ya ndotoni (Sexual dreams) – Mtu unapolala unaota unafanya mapenzi ndoto mpaka wakati mwingine mpaka unazaa mtoto, anakuwa jini amevaa sura ya mnyama au mtu unayemjua. Mwanadamu anaweza kulazwa usingizi na jambo likaendelea. Kama Mariamu alivyotunga mimba kwa uweza wa roho mtakatifu, kuna namna ya kichawi ya kufanya watu kutunga mimba.

Ulimwengu wa mwili miaka hii tunayoishi na tunayoelekea umegeuka kuwa uwanja wa vita baina ya ufalme wa Mungu na ufalme wa Ibilisi wote wakitenda kazi ndani ya watu, inahitaji macho kujua ni nani unayejihusisha nae iwe kwenye ndoa, kazi, biashara au siasa.

"BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA NZIMA YA JUMAPILI"

Post a Comment

0 Comments