google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KALENDA ZA KICHAWI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
JUMAPILI 31 MACHI 2024
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: KALENDA ZA KICHAWI

Kuna ulimwengu wa aina mbili ulimwengu wa kiroho na ulimwengu wa kimwili chochote kinacho tokea ulimwengu wa mwili kimeanzia rohoni. Mambo hayajitengenezi yenyewe yanatengenezwa katika ulimwengu usioonekana. 

Ili mambo yatokee kuna kalenda ya kiroho na jambo lolote ili likupate lazima liendane na kalenda ya rohoni. Kanuni za kidunia zina kalenda, vivyo hivyo matukio yote yapo kwenye kalenda ya kiroho yanatimia katika ulimwengu wa mwili.

Kila maisha yana adui wake na wanakufuatilia kila mahali na hao ndio wanao tengeneza kalenda za kichawi zenye matukio mbalimbali.

Kuna kalenda za kishetani ambazo zimejaa matukio ya kishetani ili kupindua kal enda ya ki Mungu yenye matukio ya ki Mungu yalio pangwa na Mungu kukupata wewe. Yanayo kupata mwilini ni matokeo ya yale yalio pangwa katika ulimwengu wa roho.

“Baada ya hayo mfalme Ahasuero alimwongezea cheo Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, akampandisha, akamwekea kiti chake juu ya maakida wote waliokuwapo pamoja naye. Nao watumishi wote wa mfalme, walioketi mlangoni pa mfalme, wakainama na kumsujudia Hamani, maana ndivyo alivyoamuru mfalme kwa habari zake. Bali Mordekai hakuinama, wala kumsujudia. Basi watumishi wa mfalme walioketi mlangoni pa mfalme wakamwambia Mordekai, Mbona wewe waihalifu amri ya mfalme? Ikawa, waliposema naye kila siku asiwasikilize, wakamwarifu Hamani, ili kuona kama mambo yake Mordekai yatasimama; maana alikuwa amewaambia ya kuwa yeye ni Myahudi. Hata Hamani alipoona ya kwamba Mordekai hainami wala kumsujudia, alighadhibika sana. Akaona si shani kumtia mikono Mordekai peke yake; maana wamemjulisha kabila yake Mordekai; kwa hiyo Hamani alitaka kuwaangamiza Wayahudi wote waliokuwa wakikaa katika ufalme wote mzima wa Ahasuero, yaani, watu wake Mordekai. Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaanikura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari.” Esta 3.1-7.

Mambo yanampata mtu pale ambapo saa, siku na mwezi wa hilo jambo lililopangwa kutimia kwenye kalenda husika hutimia. Kalenda ndio inayoamua mambo gani yakupate kwa saa gani.

Kazi kubwa ya kishetani ili itimie inahitaji tarehe ya kutimia kwa ilo jambo ambayo ndio siku ya uovu. Siku ya uovu huwezi kuikwepa kwa kukodi gari, au kwa njia za kimwili, litatimia tu. Siku ya uovu inabadilika kwa kuomba, kilicho tengenezwa kiroho huwezi kukitengua kimwili bali kwa njia za kiroho tu. 

“Basi Mordeikai alipojua mambo yote yaliyofanyika, alizirarua nguo zake, akajivika gunia pamoja na majivu, akatoka hata kufika katikati ya mji, akalia kwa sauti kuu ya uchungu. Pia akafika hata mbele ya mlango wa mfalme; maana hakuna awezaye kuingia ndani ya mlango wa mfalme hali amevaa magunia. Na katika kila jimbo, ambako amri ya mfalme na mbiu yake imewasili, palikuwako msiba mkuu kwa Wayahudi, na kufunga, na kulia, na kuomboleza; hata na wengi wakalala juu ya gunia na majivu.” Esta 4.1-3.

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA NZIMA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments