google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KINYWA CHA KICHAWI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 03.03.2024
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: KINYWA CHA KICHAWI

Maneno yanayotamkwa yana nguvu ya kubomoa ama kujenga, Maneno yanapotamkwa yanakuwa angani yakisubiri muda ili yatimie. Wakati wana wa Israeli wameangusha ukuta wa Yeriko, Yoshua akasema maneno ya laana kwa atakaye kuja kujenga ukuta wa Yeriko.

“Naye Yoshua akawaapisha kiapo wakati ule, akasema, Na alaaniwe mbele za BWANA mtu yule atakayeinuka na kuujenga tena mji huu wa Yeriko; ataweka msingi wake kwa kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake, tena atayasimamisha malango yake kwa kufiliwa na mtoto wake mwanamume aliye mdogo.” Yoshua 6:26.

Baada ya kupita miaka karibu mia tatu, akatokea mtu anaitwa Hieli Mbetheli akataka kuujenga ukuta, yale maneno ya laana yakatimia.

“Katika siku zake, Hieli Mbetheli akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu; sawasawa na neno la BWANA alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.” 1 Wafalme 16:34.

Lakini pia maneno ya Yoshua yalifanya maji ya Yeriko yawe machungu, yasiyofaa na yenye kufanya nchi kuzaa mapooza.

“Watu wa mjini wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza. Akasema, Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea. Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, BWANA asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza. Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.” 2 Wafalme 2:19-22.

Ahabu alinenewa maneno ya laana na Eliya kwa sababu alimuua Nabothi aliyemiliki shamba zuri la urithi ambalo alikataa kumuuzia. Ahabu na mkewe Yezebeli wakatengeneza kisa ambacho kilifanya Nabothi auwawe.

“Neno la BWANA likamjia Eliya Mtishbi, kusema, Ondoka, ushuke, ukutane na Ahabu mfalme wa Israeli, akaaye katika Samaria; yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ndiko alikoshukia ili alitamalaki. Ukamwambie, ukisema, BWANA asema hivi, Je! Umeua, ukatamalaki? Nawe utamwambia, kusema, BWANA asema hivi, Mahali pale mbwa walipoiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba na damu yako, naam, damu yako. Ahabu akamwambia Eliya, Je! Umenipata, ewe adui yangu? Akamwambia, Nimekupata, kwa sababu umejiuza utende yaliyo mabaya machoni pa BWANA. Angalia, nitaleta mabaya juu yako; nami nitakuangamiza kabisa, nitamkatia Ahabu kila mume, aliyefungwa na aliyeachwa katika Israeli. Kisha nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa ajili ya chukizo ulilonichukiza, hata kunighadhibisha, ukawakosesha Israeli. Tena BWANA alinena habari za Yezebeli, akisema, Mbwa watamla Yezebeli katika kiwanja cha Yezreeli. Mtu wa nyumba ya Ahabu afaye mjini, mbwa watamla, na yeye afaye mashambani ndege wa angani watamla.” 1 Wafalme 21:17-24.

Pia Ahabu alinenewa maneno na Mikaya Nabii ya kwamba asingerudi kutoka vitani lakini Ahabu aligoma kumsikiliza Mikaya na kumfunga.

“Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya, mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme; mkaseme, Mfalme asema hivi, Mtieni mtu huyu gerezani, mkamlishe kwa chakula cha shida, na maji ya shida, hata nitakaporudi kwa amani. Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, BWANA hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.” 1 Wafalme 22:26-28.

Maneno yote aliyonenewa Ahabu kutoka kwa Eliya (kuwa Mtu wa nyumba ya Ahabu afaye mjini, mbwa watamla) na Mikaya (Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, BWANA hakusema kwa mimi) yakaja kutimia. Pamoja na mbinu zote za kukwepa kuuwa lakini maneno ya laana yaliyokuwa juu yake yakatimia. Neno lile lililonewa linatafuta fursa litimie.

“Mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari lake, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana. Pigano likazidi siku ile; mfalme akategemezwa garini mwake, kinyume cha Washami, hata jioni akafa; damu ikatoka katika jeraha yake ndani ya gari. Ikapigwa mbiu jeshini, jua likichwa, kusema, Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake. Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria. Wakaliosha gari penye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake; (basi ndipo walipooga makahaba); sawasawa na neno la BWANA alilolinena.” 1 Wafalme 22:34-38.

Wachawi nao wanaweza kutamka neno likawa. Wana wa Israeli wanatoka nchi ya ahadi na utiisho juu yao, wakawa wanapita kwenye nchi ya Moabu, mfalme wa Moabu Balaki akawaogopa na hofu ikajaa moyoni mwake. Balaki akaenda kwa mchawi Baalamu ili awalaani wana wa Israeli. Mchawi anakinywa cha kutamka juu ya mtu ikawa maana Balaki anamwambia Baalamu yeyote umlaanie lazima iwe.

Wewe nawe kuna maneno unaweza kuwa umetamkiwa na kinywa cha kichawi. Ukitamkiwa maneno na kinywa cha kichawi kama vile Mungu anavyoliangalia neno ili alitimize.

“Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.” Yeremia 1:12.

Mashetani, mapepo, majini nao wanaweza kulisimamia neno la kinywa cha kichawi mpaka litimie. Maneno uliyotamkiwa kichawi yanaweza kutengeneza tabia, udhaifu nk, ambao utakufanya ushindwe kufikia hatima yako.

Lazima mtu mwenye mamlaka na kinywa cha ki Mungu yaani Baba atamke maneno mengine yatakayovunja maneno yaliyotamkwa na kinywa cha kichawi.

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA NZIMA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments