google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KIJANA NA NJIA ZAKE

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO:  KIJANA NA NJIA ZAKE
MKESHA WA ALHAMISI 12.04.2024

Umri wa ujana ni umri ambao ni vigumu kutii mamlaka. Lakini ili uweze kufanikiwa lazima uweze kutii mamlaka. Mawazo uliyonayo ni ya muhimu sana maana yana baini njia utakayoiendea. Kwa mfano; kama kijana unaweza kuamua kutokufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa na ukafanikiwa maana hio ndio njia uliyoichagua. Hivyo namna yako ya kuwaza inabaini sana njia utakayoiendea.

Namna ya kusafisha njia yako kama Kijana;

  •  Kutii mamlaka.

Mawazo yako yanabaini njia utakapita. Lakini ukiwa chini ya mamlaka hauendeshi maisha yako kwa mawazo yako bali mamlaka unayoifuata na kuitii inaweza kukusaidia kufanikiwa na kupita njia iliyosahihi. Mtu mwenye mamlaka anaweza kukusaidia kwa maneno ambayo atakuambia na itaathiri mawazo yako. Kuna wakati mtu mwenye mamlaka anaweza kuongea vitu usivyovielewa au usivyovipenda ila ukitii maneno hayo utakuwa katika njia sahihi.

  • Maombi.

Mungu ana namna mbili ya kuwaongoza watu;

  • Mungu anakuongoza kupitia mtu aliyekupa.
  • Mungu anakuongioza kupitia Mungu aliye ndani yako.

"Ee BWANA, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu." Yeremia 10:23

"Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama." Zaburi 32:8

"Watakuja kwa kulia, na kwa maombi nitawaongoza; nitawaendesha penye mito ya maji, katika njia iliyonyoka; katika njia hiyo hawatajikwaa; maana mimi ni baba wa Israeli, na Efraimu ni mzaliwa wa kwanza wangu." Yeremia 31:9

Maombi yana uwezo wa kubadili mawazo yako ili yakakubaliane na mawazo ya Mungu.

Post a Comment

0 Comments