google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KANUNI NA SHERIA ZA UCHUMBA

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
ALHAMIS 26 APRIL 2024
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO: KANUNI NA SHERIA ZA UCHUMBA

Dating system ni namna ya kidunia kufikia jambo la ki-Mungu (Ndoa). Kuna mambo katika Maisha utayapata kwa kufuata kanuni. Ukiomba sana bila kufuata kanuni huwezi kupata unachokitaka.

Sheria zisipofuatwa hata kama hukupanga kufanya dhambi utajikuta umetenda dhambi hio.

Sheria za uchumba lazima elimu ya msingi ifuatwe, usipofuata elimu ya msingi unaharibu uchumba, na huwezi kabisa kuwa na ndoa imara, nyumba isipokuwa na msingi imara inatengeneza ufa na baadae inavunjika unapata hasara ya kujenga ukuta ndoa ni kama nyumba, ili usijenge ukuta jenga msingi imara kwenye mahusiano ya uchumba fuata sheria za uchumba.

Kuna baadhi ya mambo lazima umfanyie Mchungaji wako ili aweze kukutamkia maneno ya baraka, kinacho angaliwa sio ukubwa wala uthamani wa kitu bali ni moyo wa upendo, inabidi ufanye kitu ili uwe sehemu ya maisha ya Mchungaji wako kiongozi, fanya kitu chochote.

6. Usiwe na mchumba zaidi ya mmoja.
Kuna makundi mawili, kundi la kwanza ni mtu anachumbia lakini hana utulivu, hii ina maana kuwa anaanza mahusiano ambayo sio rasmi anaanza mambo ambayo yanamfanya yule binti aamini anapendwa kweli lakini kumbe hamaanishi, ana anza kumuambia binti maneno yakumfanya binti asimuamini mtu mwingine zaidi yake yeye, baadae anakuja anamuacha na kwa kuwa mahusiano haya yalikuwa ni siri kati yao wawili basi binti anaachwa na maumivu anavunjika moyo.

Ukisha mpenda binti mmoja ukamtamkia maneno hakikisha una maanisha ukishindwa kuwa na msimamo hata ukija kuoa huwezi kabisa kutulia kwenye ndoa, maana hukuwa na msimamo tangu mwanzo, ulishindwa kuzitiisha hisia zako tangu mwanzo. Ukishaanza mahusiano na mtu usiangalie tena mabinti wengine maana mabinti wazuri wataendelea kuwepo

Katika mahusiano ya uchumba kununiana ni jambo la kawaida sana, tegemea kutofautiana na kupatana sana, haya ni mambo ya kawaida sana katika Maisha ya mahusiano ya uchumba, katika ndoa na katika Maisha  ya kawaida huwa tunatofautiana na wenzetu lakini haiwi milele bali huwa tunaelewana na kupatana na Maisha yanaendelea. Jiandae kuwa mchumba wako atakukwaza na hutakiwi wala huruhusiwi kabisa kumchukia ili kuepusha kuharibu mahusiano kwa sababu ambazo sio za lazima. Hii itakusaidia sana, ukiwa na mchumba pakatokea na mgogoro jaribu kusuluhisha au nenda kwa mamlaka husika ili mpate suluhu. Usiruhusu watu wakaja kukutuliza maana watu wanapokuja kukutuliza wanaweza wakaondoka na moyo wako, linda sana moyo wako usiruhusu moyo wako kupokea maneno kutoka kwa kila mtu maana sio kila mtu atakuwa na nia njema na mahusiano ya uchumba wako.

7. Msianze kuvaa nguo za kufanana
kipindi cha uchumba si sawa kuvaa nguo za kufanana, subirini mpaka muingie kwenye ndoa.

8. Usianze kumhudumia Binti kabla ya kumuoa
Usianze kumhudumia mchumba mahitaji yake binafsi kabla hajawa mke wako ili usije ukavunjika moyo. Kijana usimsomeshe binti, usimlipie kodi, binti usijirahisishe kwa vijana kama kwenda kupika kufua kudeki kutandika kupiga pasi hairuhusiwi kabisa haitakiwi ni marufuku.

9. Binti usianze kumhudumia kijana
Binti hairuhusiwi kwenda kwa kijana kumpikia wakati wa uchumba, kumfulia nguo zake au kufanya usafi nyumbani kwake. 

10. Msianze miradi ya kifedha pamoja
Kuna mambo mkianza pamoja ama ni biashara au kujenga baadae mkija kuachana lazima mmoja ataumia na hili haliepukiki ili kuepusha ni vizuri sana kuepuka kuwekeza pamoja.

11. Shughulikia misingi mibovu inayopatikana ndani ya Familia
Ni vizuri sana kuambiana ukweli katika yale mambo ya msingi ili muweze kushughulikia misingi mibovu katika familia. Mfano; kama mama yako aliolewa akaachika hapo unakuwa tayari umeshapata msingi mbovu wa kuharibu msingi wa ndoa, kama baba yako alifariki katika umri mdogo ni vizuri kusema ili muweze kuharibu vifo vya ghafla katika ndoa yenu. Kwa kufanya hivi itasaidia sana kuwa na ndoa imara sana maana kila misingi mibovu inakuwa imeshaharibika kabisa na inawezekana kabisa kuanzia kwenu familia ikawa imara sana. Ujifunze kuona mambo kuanzia kwenye chanzo chake ili uweze kulitatua tatizo na liishe kabisa.

Kuna mambo mtu wa Mungu akifanya  anazuia muendelezo wa matukio mabaya katika familia au katika  jamii inayomzunguka, watu wengine wanaoa wanaacha kumbe ni jambo la rohoni, likishughulikiwa linaisha kabisa na familia yenu inakuwa imara kabisa, usishindane na  matatizo katika familia shindana na vyanzo vya matizo, katika familia ili tatizo liishe kabisa ng’oa mizizi ya tatizo usikate matawi ya mti, ng’oa mizizi matawi hayawezi kustawi tena, tatizo ni kama matawi chanzo cha tatizo ni sawa na mizizi ya mti.



Post a Comment

0 Comments