google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MAMBO YA KUZINGATIA ILI USIFANYE SEX KABLA YA NDOA 2

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
SEMINA YA MAHUSIANO ALHAMISI 05.09.2024
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO: MAMBO YA KUZINGATIA ILI USIFANYE SEX KABLA YA NDOA 2

Kuna wakati mtu akiwa mjinga, Mungu ana namna ya kuyachukilia mambo kama hayaoni. Lakini kuna wakati mtu akishalijua neno na sheria ya Mungu, akakosea, Mungu atamuadhibu sawasawa na makosa yake.

“Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu.” Matendo ya Mitume 17:30

2.   Epuka mambo yoyote yanayoamsha (kuchochea) hisia za mapenzi.

Kila mtu aliyemzima wa afya na akili huwa anapata hisia za mapenzi. Mtu wa Mungu ili asifanye dhambi inabidi ajilinde, na namna ya kushinda hisia za mapenzi ni kuepuka mambo yoyote ambayo yataamsha hisia za mapenzi.

“Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.” Mithali 4:23

Mwili wa mtu aliyeokoka hauna utofauti na mtu ambaye hajaokoka, kumbuka kinachozaliwa mara ya pili ni roho sio mwili. Ni jukumu la mtu aliyeokoka kuudhibiti mwili wake kutenda mambo fulani.

“Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule wovu hamgusi.” 1 Yohana 5:18

Kuchezea hisia za mapenzi ni sawasawa na mtu asiyetaka kuungua ila akacheza na moto. Hisia za mapenzi zipo kwa kila mtu ila zinakuwa zimelala, na zikiwa zimelala usiziamshe.

“Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.” Wimbo ulio bora 2:7

Hisia za mapenzi ni kati ya hisia zenye nguvu sana kwenye mwili wa mtu. 

Ukiwa kwenye mahusiano inakuwa hatari zaidi kwa kuwa ukishachochea hisia za mapenzi basi kuna mahali au mtu wa kuelekezea hisia hizo. Kipindi cha hatari ni pale watu wanapoanza mahusiano kwa kuwa wanakuwa na hisia za kuvutiwa na mwenzie. Hii hupelekea urahisi wa kuamsha hisia za mapenzi kwa mwenzie.

Mambo yanayoamsha hisia za mapenzi.

  • Maneno unayosikia (oral) kuhusu mapenzi. Maneno yana nguvu sana kuchochea hisia za mapenzi. Kuna maneno kutoka kwa mtu unayempenda na kuvutiwa nae akikwambia kwenye mahusiano ya uchumba hisia zako za mapenzi zinaamshwa na kuchochewa. 

  • Maneno unayoandikiwa (written) kuhusu mapenzi. Maneno unayo andikiwa yana nguvu kwa maana hata ukisahau kuna sehemu unaweza kuyapata na kuyarudia.

Kwenye kuandikiana message au kuambiana maneno lazima kuwe na mipaka. Kuna maneno ambayo mtambiana kwenye ndoa ili kuepusha hisia za mapenzi wakati wa uchumba.

  • Mambo unayoyaona. Epuka kuangalia picha au majarida machafu. Teknolojia imefanya mambo machafu yawe rahisi sana kuyapata sio kama zamani. Ukishaanza kuangalia hayo mambo machafu yanakutengeneza addiction (uraibu) ambapo huwezi kuangalia hizo picha chafu bila kuamsha hisia za mapenzi. Kama kweli una nia ya kuepuka mambo yanayoamsha hisia za mapenzi, epuka kuangalia picha chafu au filamu zenye maudhui ya mapenzi.

  • Mazingira ya faragha. Mazingira ya faragha yanaruhusu kufanya sex, kuna watu wanakuwa kweli hawana dhamira ya sex ila kuwa kwenye mazingira ya faragha inapelekea kufanya tendo hili. Mazingira ya faragha hutengeneza uwezo wa kufanya mambo fulani ambayo ni ya siri na huwezi kufanya mbele ya jamii/ umma kama sex tena mkiwa na hisia za mapenzi. Sehemu ya faragha hutengeneza uwezo wa yale maneno ya kusikia na kuandikiwa kuhusu mapenzi au mambo unayoyaona, kufanya iwezekane kutenda sex maana hayo yote huamsha hisia za mapenzi. Hata ukidhamiria ila kuna mazingira ukiwepo inaweza hatarisha na ukafanya sex. Tamari alikuwa na dhamira ya kutokufanya sex na kaka yake yaani Amnoni lakini mazingira ya faragha yakapelekea kufanyika tendo hilo.

“Amnoni akamwambia Tamari, Kilete chakula chumbani, nipate kula mkononi mwako. Basi Tamari akaitwaa mikate aliyoifanyiza, akamletea Amnoni nduguye mle chumbani. Naye alipokwisha kuileta karibu naye, ili ale, Amnoni akamkamata, akamwambia, Njoo ulale nami, ndugu yangu. 12Naye akamjibu, La, sivyo, ndugu yangu, usinitenze nguvu; kwani haifai kutendeka hivi katika Israeli; usitende upumbavu huu. Nami nichukue wapi aibu yangu? Wewe nawe utakuwa kama mmoja wa wapumbavu wa Israeli. Basi, sasa, nakusihi, useme na mfalme; kwa maana hatakukataza kunioa. Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.” 2 Samweli 13:10-14

Ili kushinda majaribu ya mazingira ya faragha ambayo yatapelekea kuamsha hisia za mapenzi na kutenda sex ni lazima udhamirie na kuepekuka mazingira hayo kabisa. Yusufu alikuwa na dhamira ya kutokufanya sex na mkewe Potifa lakini pia alikimbia mazingira ya faragha.

“Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami. Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu. Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu? Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala aongee naye. Ikawa, siku moja, akaingia nyumbani atende kazi yake, wala hapakuwa na mtu katika watu wa nyumbani humo ndani; huyo mwanamke akamshika nguo zake, akisema, Lala nami. Yusufu akaiacha nguo yake mkononi mwake, akakimbia, akatoka nje.” Mwanzo 39:7-12

Kushinda kufanya sex kabla ya ndoa lazima uwe na misimamo binafsi kabla hujaingia kwenye ndoa. Kilichompa ushindi Yusufu ni msimamo binafsi wa kukimbia mazingira ya faragha ambayo ni rafiki kufanya sex.

"BONYEZA HAPA KUANGALIA SEMINA NZIMA YA MAHUSIANO"

Post a Comment

0 Comments