Mch,Josephat Gwajima.
Tangu agano la kale Mungu alikua anatolewa sadaka,na sadaka
ilikua inatumika kama mkataba kati ya mtu na Mungu katika lile jambo ambalo
anataka Mungu amfanyie.
Mchungaji Josephat Gwajima |
Mfano, Ibrahim alimtolea Mungu sadaka,na Mungu akamfanya
kuwa baba wa mataifa,Yakobo alimtolea Bwana sadaka na Mungu akafanya nae agano
la kumlinda na kumfikisha salama kule alikokua anakwenda. Unapomtolea Mungu
sadaka unaingia kwenye mapatano na Mungu juu ya suala ambalo unataka Mungu
akufanyie.
Leo sio lengo langu kuongelea sadaka hizo ambazo mtu anamtolea
Mungu,bali lengo langu ni kuzungumzia sadaka zinazotolewa kwa mashetani,sadaka
hizo ndizo ambazo zimepelekea maisha ya watu wengi kufungwa.
1 Wakorintho 10:20 “..wavitoavyo
sadaka
kwa mashetani wala si kwa Mungu..”
Hapa tunaona mashetani
wanaweza kupokea sadaka kama ambavyo Mungu anavyoweza kupokea sadaka.
Kwanini mashetani
wanapokea sadaka?
Kama ambavyo Mungu anapopokea sadaka linafanyika agano la
mtu na Mungu katika lile jambo ambalo anataka amsaidie,ndivyo ilivyo kwa
mashetani wanapopokea sadaka inakua kwa ajili ya kuwafunga watu na kuwashikilia
katika matatizo ya aina mbali mbali
Mambo matatu kujua
kuhusu sadaka ya mashetani;
Ø
Kuna sadaka ya kishetani
Ø
Mafundisho ya kishetani
Ø
Meza za kishetani
Dunia inaendeshwa na wivu,wanadamu wanakawaida ya kuoneana
wivu hasa pale anapoona mwenzake anafanya vizuri kuliko yeye kwasababu hiyo wivu
unampelekea mtu kufanya kitu chochote.
Watu wengi wanapomuona mwenzao anaendelea vizuri wana kawaida
ya kwenda kutoa sadaka kwa mashetani ili kuweza kumrudisha yule mtu chini.
NI MUHIMU KUELEWA!!
Kila mtu asiye upande wa Bwana yuko upande wa adui(shetani),ndo
sababu wachawi na waganga wa kienyeji wote watumishi wa shetani.
Watu wanapomuonea mtu wivu wanamuendea kwa mganga wa
kienyeji ili kumfunga yule mtu,wanawafunga ili mambo yake yaharibike.
Ndio sababu kuna baadhi ya watu wana matatizo ya aina mbali
mbali,kwa mfano kuna baadhi ya wanafunzi wakisoma wanaelewa lakini wakifika
kwenye mtihani hawakumbuki chochote,hii ni kwasababu wanakua wamefungwa na
waganga.
Sadaka za waganga wa
kienyeji
Mtu anapoenda kwa mganga ili kutaka jambo lifanyike kwa mtu
mwingine,mganga ana kawaida ya kuagiza sadaka kama kuku,mbuzi,ng’ombe au kitu
chochote kinachotoa damu.Mganga wa kienyeji hawezi kuomba matikiti maji,au
machungwa kwasababu kinachotakiwa ni damu ya agano ili kuweza kumfunga mtu,na
wakati mwingine wanamchanja mtu chale ili damu ya mtu yule mwenyewe itumike
kama sadaka.
Sadaka inapopelekwa kwa mganga ni kwa ajil i ya kutengeneza
mkataba kwa ajli ya kumfunga mtu.Waganga wa kienyeji ni watumishi wa shetani
asilimia mia moja na kazi yao ni kuwafunga watu wengine katika vifungo vya aina
mbalimbali.
Sadaka inapopelekwa kwa mganga wa kienyeji na kuchinjwa
mganga anawaita mashetani ambao wanaichukua ile sadaka na kuagizwa kwenda kumfunga
mtu kulingana na maelekezo ya mganga,na hapo ndipo mtu anaanza kuwa na
matatizo.
Ndio sababu ukristo sio kwenda kanisani kusalishwa bali ni kuwafungua
wote waliofungwa na Ibilisi na kuwaweka huru,ndio sababu wakati yesu yuko
duniani alifanya kazi kubwa ya kuwafungua waliofungwa.
Mashetani wanapenda sadaka za aina mbali mbali kama damu na
udi,baada ya kupokea sadaka mashetani hao wanaenda kwa mtu nakuanza kusababisha
matatizo ya aina mbali mbali.
Hii ndio sababu kama Mkristo unatakiwa ugundue shetani ni
adui na tunatakiwa kushindana nae kila siku (waefeso 6:12)
Kuna kuwa na uhusiano kati ya sadaka iliyotolewa na tatizo
la mtu alilonalo,mpaka uweze kuivunja nguvu ya sadaka ile ndio unapopata
ufumbuzi wa tatizo lako.Sadaka inakuwa na kawaida ya kusimama kuunganisha kati
ya mtu na tatizo lake
Sababu gani
inaoufanya ukristo uwe na nguvu leo duniani??
Kitu kinachoupa Ukristo nguvu leo duniani ni kutokana na sadaka
ambayo Mungu aliitoa pale msalabani kwa kumtoa mwanae.Sadaka ya damu ya Yesu
ndiyo inayofanyika kama mkataba kati yetu sisi na Mungu,na kazi ya hiyo sadaka ni
kutusamehe sisi makosa na dhambi zetu,kutuponya magonjwa,kukombolewa, kuwa
huru.nk.
Ndio inavyokua kwenye sadaka za mashetani zinakua na nguvu
ya kusababisha tatizo kuendelea kuwa kwenye maisha ya mtu,hii ndio sababu watu
wanazunguka sehemu mbali mbali kuombewa bila kupata ufumbuzi,mpaka utakapoweza
kuivunja nguvu ya sadaka hyio kwa damu ya yesu ndipo utakapo pata ufumbuzi
sahihi.
Mashetani yanapoingia
kwa mtu huwezi kujua kama yameingia lakini utakachogundua ni kuona mambo
yanaanza kwenda vibaya kila unalokua unafanya linakua halifanikiwi
Mtu anayeenda kanisani anaweza pia kufungwa na shetani
Mfano:
Ø
Paulo alizuiwa na shetani, Matendo 13:8
Mtume Paulo alikua anahubiri lakini mchawi alitaka
kupindisha injili aliyokua anahubiri
2 Wathesalonike 2:18
Paulo alizuiwa na shetani kwenda kuhubiri injiri
Ø
Shetani alisimama pembeni ya Yoshua aliyekua
kuhani mkuu na kushindana nae. Zakaria 3:1.
Ndio sababu biblia inasema usimpe ibilisi nafasi,unapompa
ibilisi nafasi hata kama umeokoka anapata nafasi ya kukufunga,njia ya kumshinda
shetani kwa asilimia miamoja ni kwa kufunga milango yote hasa ya dhambi katika
maisha yako.
Unapotoa sadaka kwa Mungu kunakua na mapatano ya kimungu ili
Mungu asimamie ustawi wako na maendeleo yako ,ndivyo walivyo mashetani wanapopewa sadaka wanakua
na nguvu ya kusimamia matatizo katika maisha ya mtu,hii ndio sababu kuna watu
wana mapepo ambayo yamekataaa kuachia maisha yao kwasababu sadaka hazijavunjwa.
Namna ya kuvunja
sadaka
Sadaka iliyotolewa katika maisha yako inaweza kuvunjwa kwa
kutumia jina na damu ya Yesu,unatakiwa uombe kwa kutumia jina la Yesu na damu
ya Yesu kuvunja kila sadaka iliyotolewa katika maisha yako ili kukufanya
uharibikiwe,unaharibu kila nguvu ya sadaka iliyosababisha taabu na shida katika
maisha yako.
Kwanini wahawi
wanatumia damu?
Uhai wa wa mwanadamu uko katika damu yake,na uhai wa mnyama
uk ndani ya damu yake.
Walawi 17:11 “..Kwakua uhai wa mwili uko katika hiyo damu ..”
Waganga wa kienyeji wanapotumia damu kufanya maaagano damu
ile inasimama kwa gharama ya uhai wa kiumbe kilichotolewa damu hiyo.
Mambo ya kufahamu
kuhusiana na damu
Mwanzo 4:10 “Akasema umefanya nini?sauti ya damu ya ndugu
yako inanililia kutoka katika ardhi..”
Ø
Damu ni uhai
Ø
Damu ina sauti
Ø
Damu inaweza kulia
Damu zinazotelewa kwa waganga wa kienyeji zinakua zinanena
mambo mabaya katika maisha yetu kila siku ndio sababu mtu aliyotolewa sadaka
kwa mganga wa kienyeji matatizo aliyonayo yanakua na kawaida ya kuongezeka siku
baada ya siku.
Sababu kwanini lazima tunyamazishe damu ni kwasababu damu
nyingine zote katika maisha yetu zinatakiwa kunyamaza kimya na damu ya Yesu
iweze kunena yale ambayo inatakiwa kunena katika maisha yetu
Waebrania 12:24 “..na Yesu Kristo mjumbe wa agano jipya, na damu
ya kunyunyiza inenayo mema kuliko ile ya Habili”
Damu ya Yesu inanena ushindi katika maisha yetu leo,inanena
uponyaji,inanena ukombozi na mafanikio katika maisha yetu katika jina la Yesu
0 Comments