google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

VITA YA HATIMA

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
JUMAPILI 05 MEI 2024
ASKOFU DR JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: VITA VYA HATIMA (THE BATTLE OF YOUR DESTINY)


Kila mtu aliyepo duniani hajui atakuwa nani baada ya miaka ya baadae. Mfano: Unasoma kidato cha kwanaza na una miaka 13 au 14 lakini utakapofika miaka 50 utakuwa nani, ule mwisho wako ndio hatima yako, u
takuwa nani baadae hio ndiyo HATIMA. Kesho imeficha mambo tusiyoyatarajia.

Kabla hujazaliwa Mungu alishaamua utakuwa nani. Ndoto ni kiashiria ya utakuwa nani lakini njia ya kufikia hapo Mungu hakuonyeshi na anafanya hivyo ili usiogope na kuacha kufuatilia hatima yako.

“Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.” Mwanzo 25:21

Mungu huwa anakupeleka sehemu kwanza kabla hujawaongoza wengine sehemu hio. Huwezi kuongoza watu sehemu ambayo hujafika. Mfano kwenye biblia, Musa alikimbilia Jangwani. Musa huyo huyo akawaongoza watu jangwani lakini hakuingia nchi ya ahadi maana hakuwahi kufika. Lakini wapelelezi waliotoa ripoti nzuri ya nchi hio ndio waliyowaongoza wana wa Israeli kufika nchi ya ahadi.

Kwa nini Yesu ndio njia ya kwenda Mbinguni, Ni kwa sababu yeye alishawahi kufika Mbinguni.

 Kuna matukio yanakupata wewe ni fundisho unalolipitia ili uweze kumsaidia mtu

“Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA. BWANA akamwambia, Mataifa mawili yako tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo.” Mwanzo 25:22-23

"Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake," Wagalatia 1:15

"Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado." Zaburi 139:16

Kipo kitabu kilichoandikwa kuhusu wewe na huwezi kufa mpaka yote yatimie, pia hakuna atakayebadilisha yaliyoandikwa. Ikishaandikwa imeandikwa. Mungu ana kitabu chake cha hatima zetu. Watu wanaweza kuwa na uadui na wewe sio kwa sababu umekosea bali ni kwa sababu ya hatima yako njema. Mfano:Yusufu aliota ndoto kwamba kaka zake wangemuinamia wakaamua kumuua.

Mungu akikupenda anakuunganisha na watu. Hao wanakuchukia kwa sababu ya hatima yako, anaweza kukuchongea njia nyingine ili usifike kwenye hatima yako. Lakini kama Bwana aishivyo, kile ulichoandikiwa kitafanikiwa.

 BONYEZA HAPA KUTAZAMA IBADA NZIMA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments