google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

DHIKI YAKO ILIANZIA MADHABAHUNI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
SIKU YA WANAUME - 30.06.2024
PASTOR ANSFRIED MSIMBE
SOMO: DHIKI YAKO ILIANZIA MADHABAHUNI

"Utanifanyia madhabahu ya udongo, nawe utatoa dhabihu zako juu yake; sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani, kondoo zako, na ng’ombe zako, kila mahali nitakapotia ukumbusho wa jina langu, hapo ndipo nitakapokujilia na kukubarikia." Kutoka 20:24

Muanzilishi wa madhabahu ni Jehovah mwenyewe, ili Mungu aje akutane na wanadamu lazima iwepo madhabahu na ili Shetani aje akutane na wachawi lazima iwepo madhabahu, hakuna kinachofanyika kama hakuna madhabahu kwa sababu wanaofanya mambo yatokee ni wale wa rohoni.

"Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao." Ufunuo 6:9

Kuna watu wapo madhabahuni hata kama uko kanisani lakini jina lako wanalitumia lakini leo tutatupa moto kwenye madhabahu zao ili waweze kukuachilia, wachawi wana madhabahu na hiyo madhabahu wanataja jina lako, shida zote za duniani zipo kwenye madhabahu kwa sababu hiyo inakupasa siku zote kufanya vita.

"Balaamu akamwambia Balaki, Nijengee hapa madhabahu saba, ukaniandalie hapa ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba. Balaki akafanya kama Balaamu alivyonena. Balaki na Balaamu wakatoa sadaka, ng’ombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu." Hesabu 23:1-2

Ukiona mtoto hatulii nyumbani, akili haitulii, anawaza wizi, kuvuta bangi, unzinzi na uasherati ujue ipo madhabahu ndani yake inayofanya afanye vitu hivyo, tabia za watu wengine zinatokana na pepo walio ndani yao, na wengine unakuta ugonjwa, tabia mbaya anakufa nazo.

Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao. 3Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za BWANA zikawaka juu ya Israeli." Hesabu 25:1 

Ukijiungamanisha na Shetani wakati uko kwa Mungu, Mungu anakasirika sana na unaweza ukafia njiani, mtu yeyote ili awe na dhiki fulani iko madhabahu, unapokuwa umeungamanishwa na madhabahu unapolala usiku wanakulisha kutoka kwenye madhabahu yao, unaota unakula nyama, samaki mkubwa mzuri, kumbe ukila tu ndotoni magonjwa yanaanza kutokea mwilini, laana inakufuatiia, wakati mwingine unaota unakunywa soda kumbe unakunywa damu ya mtu. 

"Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni." Isaya 29:8

Ikawa usiku uo huo BWANA akamwambia, Mtwae ng’ombe wa baba yako, yaani ng’ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo; Waamuzi 6:25. madhabahu lazima ibomolewe ili wewe uweze kupata nafuu.

Dawa ya madhabahu ni kuibomoa, mchawi anakuletea matatizo, anakuloga wewe, anamloga mtoto wako, unachotakiwa kufanya ni kuibomoa madhabahu yake.

“Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; 3nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.” Torati 12:2-3 

Kabla ya kuvunja madhabahu unatakiwa kutubu ili usihesabiwe uovu, usimchokoze shetani wakati unakula kwake, toka kwanza ndio upambane nae.

"Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake." Marko 11:23

Huwezi kupokea neno lolote kwa Bwana wakati kuna watu umewashikiria, unatakiwa kusamehe kwanza ili na wewe uweze kusamehewa, kama haujasamehe na wewe huwezi kusamehewa, na hapa wengi huwa wanakwama kwa kuwa na ugumu wa kuwasamehe wengine, ukishasamehe unatuma Malaika wa Bwana anakwenda kufyeka madhabahu inayokushikiria.

"Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia." Isaya 59:1-2. Mungu anataka unyenyekevu.

"Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo." Yohana 9:31

Sisi tuna nguvu isiyo ya kawaida, tuna matatizo kwa sababu  moja tu ya dhambi kama tukikaa hapo vizuri ni tuna nguvu isiyo ya kawaida.

Post a Comment

0 Comments