UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
SEMINA YA VIJANA, ALHAMISI, 25/07/2024
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO: SABABU ZA KWANINI USIFANYE SEX KABLA YA NDOA
- Inaweza kukuletea urahibu (addiction).Kila mwenye urahibu haikuanza tu, lakini kwa kufanya kitu kile kile mara kwa mara. Mwili unapozoeshwa mambo kuyaacha inakuwa kazi ngumu sana pamoja na kujua madhara yake.
“Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee
matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya
anasa.” Zaburi 141:4
Namna ya kushinda urahibu wa kufanya sex kabla ya ndoa ni kutokuanza kabisa ili usiizoelee.
- Ili kuepuka kutoka nje ya ndoa hata ukiwa kwenye ndoa.
Mtu anayeweza kuzuia hisia za kufanya sex kabla ya ndoa amefuzu hata akiwa ndani ya ndoa anaweza kudhibiti tamaa ya kutoka nje ya ndoa.
Jaribu la kutoka nje ya ndoa ni endelevu kwa wanaume wote. Hata ukioa kama haujaudhibiti na kuuweza mwili wako basi utatoka tu nje ya ndoa ukiwa kwenye ndoa. Udhihirisho wa kuwa utalishinda jaribio la kutoka nje ya ndoa ni ukiweza kuushinda mwili kwenye uchumba.
“Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe
mumewe haki yake. Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo
hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa
mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije
akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.” 1 Wakorintho 7:3-5
Kuna mazingira ambayo inakuwa ngumu kupata sex hata ndani ya ndoa mfano mwenzi wako akiwa mgonjwa, yupo mbali na wewe nk, kama huwezi kujizuia inakuwa rahisi wewe kwenda kutafuta sex nje ya ndoa.
- Inaweza kuondoa shauku ya kuoa.
Kibiblia ndoa ni sababu ya msingi watu kukimbia uzinzi na kutokumtenda Mungu dhambi.
“Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.” 1 Wakorintho 7:2
“Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane, Ni heri
wakae kama mimi nilivyo. Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana
ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.” 1 Wakorintho 7:8-9
Inatakiwa uipate ndoa mkiwa wadogo, mnakuwa pamoja kwenye ndoa. Ili kuepuka kuzoea ndoa epuka kufanya sex kabla ya ndoa.
“Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako.” Mithali 5:18
0 Comments