UFUFUO NA UZIMA
CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 15.09.2024
ASKOFU DKT JOSEPHAT
GWAJIMA
SOMO: KARAMA YA MUNGU HAINA
MAJUTO - SEHEMU YA NNE
Kabla
ya kuzaliwa ulikuwepo na kabla ya kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu ulikuwapo. Kila
mtu alikuwa kwa Mungu naye amemtuma kwa ajili ya kazi fulani na kila kilicho
toka ndani ya Mungu sikuzote lazima kitashinda. Neno la Mungu ndilo litiao
uzima.
“BWANA alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake, Kabla ya matendo yake ya kale. Nalitukuka tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia” Mithali 8:22
Wewe unaweza kusahau kusudi ambalo Mungu
ameweka ndani yako lakini pamoja na hilo haimaanishi huna kusudi la Mungu. Mungu
anakukumbusha kusudi lako kwa kupitia neno la Mungu alilomuekea mtumishi wake. Neno la Mungu ni maneno ya uzima,
pale unapoanza kuelewa neno la Mungu unaanza kuelewa asili yako ya mbinguni maana
Mungu anakuwa anongea wewe ili ufanye kusudi lako.
Kuna watu wa aina mbili, kuna watu wenye nia ya ki Mungu na kuna wenye nia ya kishetani. Wewe ni wa Mbinguni na umetumwa kwa kazi maalumu ambapo baada ya kufanya kazi hio utarudi utarudi ulipotoka yaani Mbinguni.
Pale tunapofanya kusudi la Mungu tunapata faida
na baraka. Wewe na mimi tupo hapa duniani hadi kazi tulizopewa kufanya zitakapoisha.
“Alipozithibitisha
mbingu nalikuwako; Alipopiga duara katika uso wa bahari; Alipofanya imara
mawingu yaliyo juu; Chemchemi za bahari zilipopata nguvu Alipoipa bahari
mpaka wake, Kwamba maji yake yasiasi amri yake; Alipoiagiza misingi ya nchi; Ndipo
nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi; Nikawa furaha yake kila siku Nikifurahi
daima mbele zake;” Mithali 8:27
Kuna mambo mengine yamefichwa machoni pako ili kufanya
kile Mungu alichouagiza kwa kupitia mtumishi wake kwa kuhubiri neno la Mungu. na
pale tunapo sikia na kuelewa neno na kuwa na hisia ya kitu hicho hujue Mungu
anasema na wewe unatakiwa uchukue na kufanyia kazi ili uweze kupata matunda kwenye
Maisha.
Wewe unaweza kuwa adui ambaye hapendi ufike pale Mungu alipo kusudia, anaweza kuwa rafiki yako au mtu karibu. Unatakiwa uombe mara kwa mara ili umshinde adui huyo.” MIMI NA WEWE TULIKUWEPO KABLA YA KUUMBWA KWA MISINGI YA ULIMWENGU” AMEN.
0 Comments