google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MAMBO YA KUZINGATIA ILI USIFANYE SEX KABLA YA NDOA 3

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
SEMINA YA MAHUSIANO ALHAMISI 13.09.2024
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO: MAMBO YA KUZINGATIA ILI USIFANYE SEX KABLA YA NDOA 3

Kuna mambo ambayo watu hufanya ili wawe namna fulani. Unapoona mtu anamaisha ya namna fulani kuna mambo ambayo anafanya na mengine hafanyi. Mara nyingi mambo yanayowajenga watu ni yale ya sirini. Unaweza kutamani maisha ya mtu ila kama hujui mambo anayofanya sirini basi huwezi kamwe kuwa kama yeye. 

Mungu hawezi kumlazimisha mtu aishi maisha fulani, unachagua mwenyewe. Maisha ya mtu ni machaguo aliyoyafanya jana, juzi na siku zilizopita.

“Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;” Kumbukumbu la Torati 30:15

Mungu hata akitaka usiharibike ni maamuzi yako ndio yatakayoamua hatima yako. Mungu alimuonya Kaini kuwa dhambi iko inamuotea mlangoni lakini Kaini akaamua kuifuata hio dhambi.

“BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.” Mwanzo 4:6-7

Matokeo ya maisha ya mtu hayatokei papo kwa papo, inaweza kuchukua muda mrefu sana hadi kuja kudhihirika. Kitu kibaya ni kuwa unaweza kusahau hata wewe mwenyewe mbegu ya matokeo unayoyaona uliipanda lini. Umri wa ujana ni umri ambao umeficha mbegu zinazopandwa, ambazo matokeo yake utayaona baadae sana. Matokeo hutaweza kuyaficha hata ukijaribu namna gani.

3. Usifanye Urafiki na Mtu ambaye Hana Dhamira kama ya Kwako.

Chagua rafiki ambaye ana amini kile unachokiamini. Marafiki ni wa muhimu na epuka urafiki na mtu anayeona sex kabla ya ndoa ni kawaida. Tabia nyingi za watu zinaanza na marafiki, marafiki wanaweza kukujenga au kukuharibu. Kama kuna mtu atakuathiri maisha yako kwa ukaribu sana ni rafiki.

“Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi; Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego.” Mithali 22:24-25

Kwenye mazungumzo ya marafiki kumejaa nguvu ya kukushawishi kufanya mambo ambayo hata wewe hukuwaza kufanya na baada ya muda utakuwa kama rafiki yako.

“Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.” 1 Wakorintho 15:33-34

Biblia ya kiingereza inasema;

“Don’t be fooled by those who say such things, for “bad company corrupts good character.” Think carefully about what is right, and stop sinning. For to your shame I say that some of you don’t know God at all.” 1 Corinthians 15:33-34

Bad company inayozungumzwa hapa ni watu ambao ni wa karibu kwako kama marafiki. Watu wengi wanaharibika kutokana na kushindwa kuachilia na kukaa mbali na marafiki wabaya kwa sababu tu mlisoma pamoja au mna historia kwenye jambo fulani. Hutaweza kukaa na mtu muhuni alafu ukategemea akujenge kwenye mema..

“Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.” Waefeso 4:29

Marafiki wanaweza kugeuza mtazamo wako ukaona mambo mabaya kuwa ni mambo mazuri. 

“Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.” Mithali 28:24

Njia ya mtu inaharibika au kujengeka kwa mambo matatu tu;

  •  Mambo anayoongea
  • Mambo anayoyawaza (anayotafakari)
  • Mambo anayoyatenda

Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.” Yoshua 1:8

Mambo mabaya nayoongea na marafiki yakikuingia kinachofuata unaendea njia ya uharibifu. 

Kuna aina mbili ya marafiki ambao ni muhimu kuwaepuka;
  • Marafiki wa duniani (hajaokoka) ambao wanaziendea njia za dhambi.
  • Marafiki wa kanisani wenye tabia za kidunia. Sio kila mtu wa kanisani inabidi pia awe rafiki yako.

Kuna watu ambao Paulo anawataja sio wa kuchangamana nao. 

“Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.” 1 wakorintho 5:10-11

Mfano wa mtu aliyefuata ushawishi wa rafiki yake mbaya kwenye Biblia ni Amnoni, Amnoni alishauriwa vibaya na rafiki yake kulala na ndugu yake Tamari. 

“Ikawa baada ya hayo, Absalomu, mwana wa Daudi, alikuwa na umbu mzuri, jina lake akiitwa Tamari, naye Amnoni, mwana wa Daudi, akampenda. Akasononeka Amnoni, hata akaugua, kwa ajili ya umbu lake Tamari, maana huyu msichana alikuwa mwanamwali, Amnoni akaona ni vigumu kumtendea neno lo lote. Lakini Amnoni alikuwa na rafiki, jina lake Yonadabu, mwana wa Shama, nduguye Daudi; naye Yonadabu alikuwa mtu mwerevu sana. Naye akamwambia, Kwa nini, Ee mwana wa mfalme, unakonda hivi siku kwa siku? Hutaki kuniambia? Amnoni akamwambia, Nampenda Tamari, umbu la ndugu yangu, Absalomu. Yonadabu akamwambia, Lala kitandani mwako ujifanye mgonjwa na babako atakapokuja kukutazama, umwambie, Mwache ndugu yangu, Tamari, aje, nakusihi, anipe mkate nile, akaandae chakula machoni pangu nikione, nikakile mkononi mwake.” 2 Samweli 13:1-5

Ili uwe salama usifanye sex kabla ya ndoa epuka kwa nguvu zote marafiki wasio na nia moja kama wewe kwenye masuala ya sex.

"BONYEZA HAPA KUANGALIA SEMINA NZIMA YA MAHUSIANO"

Post a Comment

0 Comments