UFUFUO NA UZIMA
CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 13.10.2024
ASKOFU DKT
JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: ADUI WA NJIANI
![]() |
Kila mtu maisha anayoyaishi sio
kama ananvyo waza. adui wa njiani anakuja pale kwenye njia yako na adui huyo
lengo lake ni kuizuia kile kitu ambacho Mungu amekupa. Kuna mambo mtu ananataka
kufanya lakini kuna kizuizi ambacho kina zuia usifanye hilo jambo. Maisha yako
sio kwamba unafanya ili ufanikiwe ila kwasababu Mungu alisha panga kabla ya
kuumbwa kwa misingi ya Ulimwengu. Inakupasa kufanya vita na adui huyo ili
asiweze kukuzuia.
“Kumbuka aliyokufanya Amaleki
katika njia mlipokuwa mkitoka Misri; jinsi alivyokukuta katika njia,
akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako,
ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu. Basi itakuwa, hapo
atakapokwisha kukupumzisha BWANA, Mungu wako, katika adui zako wote walio
kando-kando, katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo
uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.” kumbukumbu ya torati
25:17-19
Kuna wakati Mungu anaruhusu
magumu uyapitie na anaweza kumtumia mtu yoyote iliaweze kukuimarisha na uweze
kuyafanya mapenzi ya Mungu itimie hatakama unamali. Mtu wa Mungu akipewa kitu na
Mungu ameshampa na hakuna mtu wa kukuporomosha. kinachotokana na Mungu lazima kitadumu
kwasababu ilishaamriwa kabla ya kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.
“BWANA akamwambia Abramu, Ujue
hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia
watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne. Hata na taifa lile,
watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.” Mwanzo 15:13-14
Pale unapo haidiwa na Mungu kwa habari
ya maisha yako ndipo pale adui anapojitokeza ili aweze kukuzuia kuya fanya
ambayo Mungu amekuhaidi. na adui huyo anapambana ili usiweze kuyafanya mapenzi
ya Mungu na kuna wakati unapitia mambo magumu. kuna wakati mtu anayapitia na
anatamani hata amwache Mungu ila bado anakuwa na matumaini ndio mtu huyo anayokusudi
la Mungu.
“usiogope, kwa maana mimi ni
pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam,
nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.” Isaya 41:10
Kabla ya kuwekwa kwa misingi ya
ulimwengu ulikuwepo tena ulikuwa mbinguni Pamoja na Mungu. baba na mama yako
baada ya kukutana katengeza ganda ambao ni mwili na kuingia wewe ambae ni roho
na kuwa ndani ya mwili.
“Neno la BWANA lilinijia,
kusema, Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka
tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.” Yeremia1:4-5
Mungu akipanga jambo ni lazima litimie
na hakuna mtu wakuzuia jambo hilo. Inakubidi uombe kwa bidii ili uweze kuyatimiza
yale makusudi ya Mungu na kumwangusha kila adui anayetaka kukuzuia kuelekea
kwenye hatima uliopangiwa. Usimdhalau mtu kwasababu wenye haki huwa hawawezi
kumwaibisha mtu kama ilivyo kwa Yusuph alitaka kumwacha Maria bila kumdalilisha
Maria pale alipokuwa ana ujauzito
“Kuzaliwa kwake Yesu Kristo
kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla
hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye
Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu
kumwacha kwa siri.” Mathayo 1:18-19
Kuna mtu hatakama amepigwa na adui wa njiani ila bado Mungu anakuwa na makusudi nayo. Kuna mambo mtu anayoyapitia ili yaweze kumfanya kuwa imara. Ili atakapo pata aweze kuwa na hekima wakati wa kumiliki kwake.
“Ana wingi wa siku katika mkono
wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.” Mithali 3:16
“INATUPASA KUMPIGA ADUI WANJIANI
ILI KUWEZA KWENDA KULE MUNGU ALIPOSUDIA KWENDA.” AMEN.
0 Comments