google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KULISIMAMISHA KUSUDI LA MUNGU

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 12.02.2025
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: KULISIMAMISHA KUSUDI LA MUNGU

Mambo ambayo Mungu anataka kufanya kwa mtu ni lazima  mambo hayo yatimie, Mungu anaweza kufanya mambo yote hakuna la kumshinda, kwa kuomba inakufanya uondoe Kila mambo yanayotaka kuzuia kusudi la Mungu kwenye maisha yako, unacho paswa kujua kusudi la Mungu juu yako hakuna ya kuizuia.

“Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.”Ayubu 42:2

Jambo alilo likusudia Mungu lipo milele, unapokuwa unasuburia kuna wakati unachoka ila wewe sio wa kwanza. unapaswa kuwa mvumilivu kwa maana hata ingechukua mda mrefu kwa maana kusudi la Bwana litatimia juu yako. 

“Mna hila nyingi moyoni mwa mtu;Lakini shauri la BWANA ndilo litakalosimama.Haja ya mwanadamu ni hisani yake;Ni afadhali maskini kuliko mwongo.  Kumcha BWANA huelekea uhai;Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.” Mithali 19:21-22

Wewe kuna mambo unataka kuyapata lakini mambo hayo yapo kinyume na kusudi la Mungu. kila kilicho kuwa kinyume na makusudi ya Mungu juu yako haiwezi ikatimia.

kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.” Mathayo 26:39

Unae oa au kuolewa naye ameunganishwa na kusudi la Mungu,  Kumsikiliza mtu wa Mungu lina maana sana ni muhimu kuisikiliza. ni afadhali kuchelewa kufika kuliko kuwahi ukaishia njiani na kupata ajali. Inakubidi kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya kuitimiza kusudi la Mungu na usiwe na maamuzi ya harakaharaka.

“Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,” Luka 14: 28-29

Unaweza ukawa umeokoka ila kuna wakati maamuzi yanaweza yakakufanya ukaharibu mwishoni. ukawa umeanza vizuri ukaja kuharibu mwishoni ina kupasa kuvumilia kwamaana ahadi ya Mungu juu yako lazima itimie.

“Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho” Yakobo 5:7

Kusudi la Mungu limeungamanishwa na mtu unayekaanaye, Mungu akitaka kukuinua anakuunganisha na watu ambao watakupeleka kwenye kusudi la Mungu kwa maana binadamu hawezi kusimama peke yake. Ukitaka uwende kwenye kusudi lako na kilifikia inakupaswa kuambatana na wenzako,Mungu hana mwili akitaka akatakufanya kusudi lake ni lazima ajiunga manishe na binadamu. Familia ikiharibika taifa inaharibika kwasababu taifa chanzo chake ni familia. 

“Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.” Mwanzo 2:24

Mungu hawapi sifa wenye sifa ila humpa sifa aliye mchaguae na amtakae, chunguza moyo wako mwenyewe maana Mungu anajua kila mtu hatakama watu wanakuona kuwa ni mwema ila Mungu anakujua wewe ulivyo. Miongoni mwa watu kuna watu wabaya lakini mwisho wa watu hao una fanana. Anayeogopa vita hawezi kwenda juu. 

“Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;” 1Petro 2:9 

"BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI"

Post a Comment

0 Comments