google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

VIKAO VYA UHARIBIFU

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 14.12.2025
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO: VIKAO VYA UHARIBIFU

Mambo yote ambayo yanampata mtu inaweza yakawa mema au mabaya yanayoonekana ulimwengu huu, yanatengenezwa kwenye ulimwengu usio onekana (roho) na inatengenezwa na watu ambao hawana mwili. ambao wanakaa kwenye vikao kwenye ulimwengu usio onekana (roho).

“Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha BWANA bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako”. Ayubu 1:9-12 

Kuna mambo mtu anayapanga yanaweza kuwa Biashara, kazi, masomo na mambo mengine ambapo mtu amepanga kufanya. Ila kuna watu wameweka vikao kwenye ulimwengu usioonekana lengo lao ni kuzuia usilitimize jambo hilo aliopewa na Mungu. Na baada ya muda fulani hilo tukio litampata mtu katika ulimwengu wa mwili au unaoonekana.

Watu hao wanaopanga vikao hivyo vya uharibifu kwa kuweka mipango ya muda mrefu ambapo mtu kama asipo shughulika kwa sasa kuna matukio yanaweza kumpata kwa muda muda ambao umeamuliwa katika ulimwengu usio onekana.

Watu wengi wanapuuzia mambo ya rohoni ambapo mtu anaona kuwa hana muda wa kufanya hivyo ndio maana watu wengi wakuwa wanaishi maisha wasiotaka. Ni kwasababu mtu hajashughulika na mambo ya rohoni. Ukishughulika na mambo ya rohoni utaweza kuharibu mipango yao.Kuna mambo mtu amefichwa machoni pake  ili asiweze kujua mipango ya Shetani kuhusu maisha yake.

“Mikaya akasema, Sikia basi neno la BWANA; Nalimwona BWANA ameketi katika kiti chake cha enzi, na jeshi lote la mbinguni wamesimama upande wa mkono wake wa kuume na wa kushoto. BWANA akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi. Akatoka pepo, akasimama mbele za BWANA, akasema, Mimi nitamdanganya.”1wafalme 22:19-20

Kuna watu wanahisi matukio wanayopata ni bahati mbaya ila sio kweli ila kuna mipango imepangwa kwenye ulimwengu wa roho ambapo wanaweka matukio kwa wakati maalum.  

Kuna wakati mtu anaona anacho kifanya ni sahihi ila ni mpango uliwekwa kwenye vikao kwa kutaka kuharibu kusudi la Mungu juu ya mtu huyo vilivyo pangwa kwenye ulimwengu wa roho. Kuna mambo yanaonekana ni sahihi kwa sasa ila baada ya muda fulani yanaleta matokeo mabaya kwa mtu huyo. 

Mawazo ni mambo ya rohoni pale mtu atakapo waza vibaya yataleta matokeo mabaya, kwenye vikao vya uharifu pia wanaweka. Mawazo ndani ya mtu kama mtu huyo asiposhughulika anaweza kufanya mambo kupita mawazo ya Shetani na kuharibu kusudi la Mungu kwa maisha yako.

“Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,” Marko 7:20-21 

Kuna mambo mtu analea Watoto kutokana na Mawazo ya kishetani kuhisi kwa kumlea mtoto hivyo ni sahihi ila lengo la kutaka kuharibu uzao wako. Ni muhimu kushughulika kwenye ulimwengu wa Roho ili kuweza kuvunja vikao vya uharibifu. 

Mawazo ndio kitu cha muhimu ambapo kabla mtu ajanza kufanya jambo huwa Mawazo ndio yaanza baada ya hapo yanaleta mtazamo baada ya mtazamo ndipo jambo litatokea.watu wanafanya maamuzi kwa kuongozwa na mtu ambaye hana mwili na yupo katika ulimwengu usioonekana.

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI           

Post a Comment

0 Comments