google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

NGUVU YA MSALABA

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 07.12.2025
ASKOFU DKT GESHOM MWAKILA
SOMO: NGUVU YA MSALABA

Zamani mtu alikuwa akifanya makosa fulani, anahukumiwa hukumu ya kifo. Kifo hicho kinaweza kuwa kwa njia tofauti tofauti kama vile kuchomwa kwenye tanuru la moto, kupigwa mawe, ama kwa njia ya kusulubiwa msalabani. Yesu alihukumiwa kifo kwa njia ya msalaba. Kupitia mauti ya Yesu msalabani, na damu yake iliyomwagika imemkomboa mtu kutoka kwenye hukumu ya mauti na laana. 

“Tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.” Waebrania 12:12

Na ule uzima wa milele ni huu, kumjua Mungu wa kweli na Yesu Kristo mwanae. Kwa kumkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, ndipo damu yake Yesu iliyomwagika msalabani inakukomboa. Nawe unakombolewa kutoka kwenye mauti na kuingia katika uzima wa milele.

“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” Yohana 17:3 

Kuna mambo mengine yanampata mtu kwa sababu ya kutokusamehe. Nguvu ya msalaba inakupatia nguvu ya kusamehe, kama vile Yesu anavyowasamehe watu makosa yao yote. Ipo nguvu ya msalaba yenye kumfanya mtu kuwa kiumbe kipya, na kila mwana wa Mungu anayo amri ya kusamehe dhambi hapa duniani.

“Na walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, ndipo walipomsulibisha yeye, na wale wahalifu, mmoja upande wa kuume, na mmoja upande wa kushoto. Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.” Luka 23:33-34

Kuweza kupata uhakika wa maisha yako ni kuwa na imani kufuata kile Mungu anakwambia kupitia neno lake. Kwa kufanya hivyo kwa njia ya msalaba ya Yesu, inakupa uhakika kwa asilimia mia wa kufanikiwa, kustawi, kuponywa, kumiliki na mambo mengine yanayohusu maisha yako.

“Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Waibrania 11:6

Dhambi humfanya mtu asiweze kukubalika na Mungu, lakini msalaba wa Yesu unatupa kukubalika mbele za Mungu. Msalabani Yesu alibeba dhambi za ulimwengu, alifanyika laana ili wewe ukubalike mbele za Mungu na wanadamu. Kwa njia ya msalaba inamfanya mtu atoke kwenye kukataliwa hadi kukubalika.

“lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia” Isaya 59:2  

Kuna nguvu kwenye msalaba wa Yesu inayokata kiu ya mambo mabaya. Mambo hayo mabaya ni dhambi, kama vile ulevi, uzinzi, chuki, na hofu. Lakini pia kwa msalaba wa Yesu, ipo nguvu inayoweza kukuwekea kiu na shauku ya kufanya mapenzi ya Mungu kama vile kuomba, kufunga, kumsifu, kufungua watu, na kuhubiri injili. Kwa kupitia msalaba wa Yesu, unapata kiu ya kutamfuta Mungu.

 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.” 1 wakorintho 1:18

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments