google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUSUDI LAKO NA UPINZANI WA KICHAWI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 18.01.2026
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: KUSUDI LA MUNGU LITASIMAMA

2.KUSUDI LAKO NA UPINZANI WA KICHAWI

Mungu anapokuchagua kwaajili ya kusudi lake, kuna wakati maadui ni wengi wanaotaka kukuzuia. Ila hilo lisikukatishe tamaa kwa maana Mungu anaruhusu upite katika njia hiyo, ili aweze kukutengeneza kwaajili ya kuliendea lile kusudi sawasawa na mapenzi ya Mungu. Mungu akitaka kumwinua mtu, hutumia mtu.

Mungu alipotaka kumwinua Daudi, alimtumia Goliati ili aweze kulifanya lile ambalo wengine walishindwa. Yapo mambo yanayomtokea mtu mwilini ambayo chanzo chake ni rohoni. Mambo haya humpata mtu ili kumpinga asitimize kusudi lake, ingawa kusudi la Mungu juu ya mtu huyo ndilo litasimama. 

Mashetani wanauwezo wakujua hatima yako. Wanauwezo kuona kesho yako, na kazi yao wanashindana na wewe ili usiende kwenye kesho yako ambayo Mungu ameikusudia. Kuna kitu kikubwa kimewekwa na Mungu ndani yako, na mashetani wanajua. Hivyo hufanya kazi ya kukutengenezea matukio ya kukuzuia ama kukukatisha tamaa ili usitimize wito wako. Kwenye ulimwengu wa roho hakuna bahati mbaya, kila tukio linalompata mtu linakuwa limetengezwa kukuzuia.

“Basi akatuma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori, hata Pethori, ulio kando ya Mto, mpaka nchi ya wana wa watu wake, kwenda kumwita, akisema, Tazama, kuna watu waliotoka Misri; tazama, wanaufunika uso wa nchi, tena wanakaa kunikabili mimi. Basi, njoo wewe, nakusihi unilaanie watu hawa; maana wana nguvu kunishinda mimi. Labda nitawaweza, tupate kuwapiga, niwafukuze watoke katika nchi yangu, kwa maana najua ya kuwa yeye umbarikiye hubarikiwa, na yeye umlaaniye hulaaniwa. Wazee wa Moabu, na wazee wa Midiani, wakaenda, wakichukua ujira wa uganga mikononi mwao; wakamfikilia Balaamu, wakamwambia maneno ya Balaki. Akawaambia, Kaeni hapa usiku huu, nami nitawaletea jawabu kama BWANA atakavyoniambia; wakuu wa Moabu wakakaa na Balaamu.” Hesabu 22:5-8

Unapotumwa na Mungu, unageuka kutoka kuwa binadamu wa kawaida, badala yake anakuwa ni Mungu anaishi ndani yako kupitia wewe.  Hivyo, chochote unachokuwa unafanya inakuwa sio wewe bali Mungu anafanya kupitia wewe. Unakuwa ni mtu kabisa wa kawaida ila ndani yako, ni Mungu ndio anaeishi na kufanya mambo kupitia wewe. Ukitembea ni Mungu anatembea! Ukibariki ni Mungu anabariki! Yaani kila unalolifanya anakuwa ni Mungu anafanya kupitia wewe ili kusudi lake litimie. 

“Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La. Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako? Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.” Yohana 1:21-23

Kuna wito ndani yako ambao hukusukuma kupenda kufanya mambo fulani, ambayo ndio yanakupeleka kwenye lile kusudi la Mungu. Ingawa huwezi kuona kwa wakati huo, ila ndo Mungu anakuwa anakupeleka kwenye kusudi lako.

Unapoona maadaui wanakushambulia, ni kwasababu ya ule wito ambao una nguvu ya Mungu ndani yake. Na hiyo nguvu ndio inakushikilia ili uweze kuendelea mbele, hivyo hawawezi kukushinda inakubidi usiogope maana una nguvu ya kuwashinda.

“BWANA akamwambia, Mataifa mawili yako tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo.” Mwanzo 25:23

Kwanini wakati mwingine kwenye maisha unapitia wakati mgumu sana? Ni kwasababu wachawi, mashetani na wasoma nyota wanakuwa wameona kesho yako, na kile Mungu alichoweka ndani yako. Hivyo wanashindana na wewe ili usifikie kesho yako iliyoamriwa na Mungu. Mungu anapokuchagua haangalii sifa ulizonazo, hangalii elimu ulionayo, haangalii umaskini ulionao, badala yake humpa mtu sifa sawasawa na kusudi lake.

“Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.” Warumi 9:15-16

Hivyo, wachawi na mashetani wakiona kile kilicho ndani yako, wanakutumia magonjwa ndani ya mwili wako ili ukate tamaa. Wachawi hawalogi kwa kuangalia sura ama muonekano wako, wanapambana na kile ulichokibeba ndani yako. Kile ambacho Mungu ameweka ndani yako. Kuna wanawake matumbo yao yameandaliwa kuleta watu wa Mungu, hivyo mashetani hufunga matumbo yao wasizae kwa urahisi. Maana wakizaa wanakuwa wametimiza lile kusudi la Mungu la kuleta watumishi wa Mungu duniani. 

“Naye alikuwa na wake wawili; jina lake mmoja akiitwa Hana, na jina lake wa pili aliitwa Penina; naye huyo Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto. Na mtu huyo alikuwa akikwea kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea BWANA wa majeshi dhabihu katika Shilo. Na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, makuhani wa BWANA, walikuwako huko.”1Samweli 1:2-3

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI


Post a Comment

0 Comments