google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

UNAWEZA KULOGWA BILA WEWE KUJUA

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 08.03.2026
ASKOFU DKT.GERSHOM MWAKILA
SOMO: UNAWEZA KULOGWA BILA WEWE KUJUA

Kwenye biblia neno ‘pepo’ limeandikwa mara 142, neno ‘mchawi’ limeandikwa mara 8, neno ‘wachawi’ limeandikwa mara 20, neno ‘uchawi’ limeandikwa mara 14, ‘uganga’ imeandikwa mara 8, ‘kulogwa kwa kupiga mafundo’ imeandikwa mara 3, Shetani imeandikwa mara 51, ‘Ibilisi’ imeandikwa mara 59 na neno ‘hirizi’ limeandikwa mara 3. Hii inaonesha ni kwa namna gani haya mambo yapo kwenye maisha ya watu na yanachangia kwa kiasi kikubwa kuharibu maisha ya watu.

Mtu anaweza kulogwa bila yeye kujua. Mtu anaweza kusema kwamba haamini uchawi, ingawa hiyo haiondoi kuwa uchawi upo. Kwa sababu biblia inasema kuwa uchawi upo, basi uchawi upo. Iwe unaamini ama huamini. Biblia inaonesha mtume Paulo alikuwa anajua ya kuwa uchawi upo na kuwa mtu anaweza kulogwa.

“Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?”  Wagalatia 3:1 

Ibilisi hakutendei mabaya kwasababu umemkosea, ila anakutendea kwa kukuonea maana ni asili yake kuonea watu. Ndio maana Yesu akaja  ili kutuweka mbali na uonevu wa Ibilisi.

Namna wachawi wanavyoweza kuloga watu

1.Unaweza kulogwa kwa kuzuiwa

Unaweza kufanya mambo yako kwa bidii lakini hupati mafanikio. Ni kwasababu wachawi wanazuia usipate baraka zako. Zipo mamlaka za rohoni ambazo kazi yao ni kuzuia mafanikio yako.  

“Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia.”1Wathesalonike 2:18

2.Unaweza kulogwa kwa kulazwa usingzi

Katika sayansi, mtu anapolazwa usingizi wanalenga kukata kitu wakitoe au kuweka kitu ndani ya mtu. Mfano mtu mwenye uvimbe tumboni anapoenda kufanyiwa oparesheni, wanakuchoma sindano ya usingizi na baada ya mtu kuamka anakuta uvimbe huo umeondolewa. Sayansi hii hata kwenye biblia imetumika. Mfano Mungu alimpa Adamu usingizi na akachukua ubavu wake na kumtengeneza mwanamke.

“BWANA Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,” Mwanzo 2:21 

Wachawi nawao wanapo loga mtu, wanasubiri mtu huyo alale usingizi ili waweze kupanda mbegu za matatizo na uharibifu ndani ya mtu. Wachawi wakikulaza wanaondoa kila kitu ambacho umepewa na Mungu. Wanafanya hivyo ukiwa umelala au wamekulaza usingizi. Nyuma ya kila tatizo ulionalo kuna kitu kimewekwa na wachawi au kimeondolewa ndani ya mtu.

3. Unaweza kulogwa ili ufe

Shetani anamipango ya uharibifu juu ya mtu na ana hila juu ya watu wa Mungu. Wachawi wanapotosha njia za Bwana kwa kufanya jambo zuri lionekane kuwa baya, ama wanapamba jambo baya lionekane zuri. Lengo nikusababisha mtu aweze kupita kwenye njia ya mauti. Usiende kwenye njia ambayo sio sahihi hata kama njia hiyo inafatwa na watu wengi. Ukiwa kwenye njia ya haki, hata kama ukiwa peke yako utashinda maana Bwana anakuwa pamoja na wewe.

“Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.” Wefeso 6:11,

Kuna mambo kwenye maisha yako yalipaswa kuwa yameshafanikiwa, lakini mambo hayo yamekufa. Na yule ambaye mambo yake yalipaswa yawe yamekufa, mambo yake yamefanikiwa kwa kuwa ameiba mafanikio yako kichawi. Mfano, unakuta mtu amevaa pete au bangiri ambazo si za urembo, bali ni zana za kishetani kwaajili ya kufanikisha mambo yake.



BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments