google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 04.01.2026
ASKOFU DKT GESHOM MWAKILA
SOMO: NDOTO NA MAISHA YA MTU

Mungu anaongea namtu kwa njia mbambali anaweza akaongea kwa njia neno lake lakini anaweza akaongea kwa njia ya Mawazo au kwanjia ya ndoto. Ndoto ni vile mtu anavyo tamani kuwa. Kuna ndoto nyingine unazipata ukiwa umelala hayo yote Mungu anakuwa anaongea na wewe.

Kuna mtu anatakiwa awe wa aina fulani ila hawezi kuwa kwasababu ya kupuuzia ndoto ambayo Mungu amemuonesha. Kwenye biblia ndoto imeonekana kwa watu mbalimbali ikiwa ambapo Mungu alikuwa anaongena watu kwa njia ya Ndoto ili watu  waweze kutii maagizo ya Mungu anayowaambia kwenye ndoto.

“Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.” Mwanzo 20:3

Ndoto haziangalii mazingira, Mungu anaweza kuongea na mtu mahala popote bila kujali mazingira uliopo. Kwenye Biblia yakobo anaoneshwa na Mungu kwa njia ya Ndoto akiwa anaonesha na Mungu kuwa atalindwa popote atakapo kuwepo. mwota ndoto anauwezo wa kubadili majina kutoka kuwa la kawaida hadi kuwa kuwa lenye ukuu.

“Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale. Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.” Mwanzo 28:10-12

Makusudi ya Mungu hayabadili yanaweza yakabidilika vitu lakini huwezi kubadili makusudi ya Mungu. Mwota ndoto anaweza kubadili jina lake kutokea la kawaida hadi kuwa la ukuu. mwota ndoto huwa atapeliwi kirahisirahisi. Mtu akibadilisha jina mara moja Mungu anasajili Jina hilo mbinguni.inakubidi ulinde kinywa chako kwa kile unacho kizungumza. Huko ulikiota ndoto unatakiwa kunatendo ulifanye kwa ajili ya ukumbusho.

“Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.” Mwanzo 28:18-19

Ndoto ya tatu inahusiana na ya pili kwasababu ndoto ya mtu ni uhalisia usipoo tii ndoto unayoiota kuna mambo unayakosa ambayo Mungu amekuagiza ufanye kwa ajili ya kusudi lake. uapoota ndoto unatakiwa ufanye maamuzi ya haraka ya kufanya ili uweze kulitumikia kusudi la Mungu kwa wakati sahihi.

Mtu yeyeote anayetaka kumtesa muota ndoto lazima Mungu ataingilia kati na kushughulika na yule anayemtesa na kumlinda mwota ndoto ili kuyafanya yale alioyomwambia mtu ili yatokee. Kuna watu ni adui wa Ndoto ambapo kazi yao ni kuzuia usifanye sawasawa na ulivyo kuagiza Mungu. Mwenye ndoto huwa hawindi kwesababu Mungu huwa anashughulika na watu wanao wawinda watu wa Mungu.

Mungu huwa anaongea na Baba na baba anaongea na Watoto, Watoto huwa hawana Mungu ila Watoto wanakuwa wana Mungu wa baba yao. baba anaweza akawa wa kimwili au wa kiroho ila inatubidi kufuata maagizo ya wazazi wetu wa kiroho maana baba anapoongea na wewe hujue Mungu anaongea na wewe kupitia baba.

Kwa kutuoa sadaka inakufanya umiliki hiyo ndoto. Ndoto ndio inayo amualila mtu maisha yake yatakuaje baadae. mashambulizi mengi huwa yanashambuliwa ndotoni. Unawweza ukawa unaota unashambuliwa au unalishwa mavyakula kuna mambo unakuta yanazuiliwa. Inabidi kuyazuia mashambulizi kwa kuomba.

Post a Comment

0 Comments