google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

BARAKA ZA KORESHI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 01.02.2026
ASKOFU DKT GERSHOM MWAKILA
SOMO: BARAKA ZA KORESHI 

Isaya 45:1–2

“Haya ndiyo BWANA amwambiayo Koreshi, masihi wake, ambaye nimemshika mkono wake wa kuume, ili kutiisha mataifa mbele yake; nami nitalegeza viuno vya wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa. Nitakwenda mbele yako na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba na kukata-kata mapingo ya chuma.”

Koreshi ni mfano wa mtu anayemtumikia Mungu kwa uaminifu. Kumtumikia Mungu ni kuwatumikia watu kwa upendo, haki na uadilifu. Hivyo, Koreshi ni yule anayewasaidia wengine kutoka katika utumwa wa aina mbalimbali na kuwaweka huru, huku akitimiza mapenzi ya Mungu katika maisha yake.

Kufanya mapenzi ya Mungu ni kuishi na kutenda kulingana na kusudi aliloliweka Mungu ndani ya kila mtu. Maandiko yanaonyesha kuwa Mfalme Koreshi aliwaacha huru wana wa Israeli kutoka utumwani. Hii inatufundisha kuwa kila mwanadamu ana kusudi maalum alilopewa na Mungu, ambalo anapaswa kulitimiza. Mfano mkuu ni Mungu alivaa mwili katika Yesu Kristo ili kutimiza kusudi la ukombozi wa wanadamu.

Zipo baraka zinazomfuata mtu anapoamua kwa dhati kumtumikia Mungu. Baraka hizo ni pamoja na uponyaji, heshima, kuongezewa siku za kuishi, na kufanikiwa katika kazi na mipango ya maisha.

Ezra 1:1–3
“Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la BWANA alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, BWANA akamwamsha roho yake Koreshi… akasema, BWANA, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu…”

Maandiko haya yanaonyesha kuwa Mungu alimwamsha Koreshi kutekeleza kusudi lake. Vivyo hivyo, Mungu humwamsha kila mtu anayejitoa kumtumikia ili awe chombo cha kutimiza mapenzi yake duniani.

Baraka za Koreshi

Zifuatazo ni baraka alizopata Koreshi, ambazo pia humpata mtu yeyote anayechagua kumtumikia Mungu kwa uaminifu:

  1. Kushikwa mkono wa kuume na Bwana
    Mungu hulinda, huokoa na huongoza kutoka hatari, dhiki, aibu, tabu na mauti, hadi mahali salama.
  2. Kutiishwa kwa mataifa mbele yako
    Mungu huondoa hofu na kukupa heshima mbele za watu.
  3. Kulegezwa kwa viuno vya wafalme ili milango ifunguke
    Mungu huondoa vikwazo na kufungua milango ya ushindi katika maisha yako.
  4. Bwana kukutangulia mbele yako na kunyoosha njia zako
    Hutengeneza njia hata pale ambapo haikuwepo, katika kazi, ndoa, elimu na maeneo mengine ya maisha.
  5. Kuvunjwa kwa milango ya shaba na mapingo ya chuma
    Mungu huondoa vikwazo vigumu vinavyokuzuia kufikia kusudi lako.
  6. Kupata hazina za gizani
    Mungu hukupatia baraka zilizofichwa na mafanikio ya kudumu.            

Kwa hiyo, mtu anapoamua kumtumikia Mungu kwa moyo wote, Mungu huondoa vifungo mbalimbali katika maisha yake na kumwezesha kutimiza kusudi lake.

Post a Comment

0 Comments