google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MSAADA UTOKAO JUU

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI – 15.03.2026
ASKOFU DKT. JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: MSAADA UTOKAO JUU 

Duniani kuna matatizo mengi yanayowakabili wanadamu, kama vile magonjwa, umaskini na changamoto nyingine mbalimbali za maisha. Ili mtu aweze kutatua tatizo lolote katika maisha yake, ni muhimu kwanza kufahamu chanzo cha tatizo hilo. Ukijua chanzo cha tatizo, unaweza kulitatua kwa urahisi zaidi. Mara nyingi matatizo mengi hutokana na kulogwa, yaani uchawi. Katika vitabu vitakatifu kama Biblia na Quruan Tukufu, imeelezwa wazi kuwa uchawi upo na kwamba kulogwa kunaweza kutokea.

Biblia inasema: “Wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.” (Kumbukumbu la Torati 18:11).

Mauti haiji tu bila sababu, bali huletwa na mwenye nguvu ya mauti ambaye ni shetani. Shetani hutumia watu wake, yaani wachawi, ambao wanaweza kusababisha mtu kuwa na hofu ya mauti au hata kifo chenyewe. 

Neno la Mungu linasema: “awaache huru wale ambao maisha yao yote, kwa hofu ya mauti, walikuwa katika hali ya utumwa.” (Waebrania 2:15).

Wachawi wanaweza kutengeneza viumbe wa kichawi ambavyo mtu anaweza kuviona kama vitu vya kawaida, ilhali vimetengenezwa kwa nguvu za kichawi. Pia wanaweza kusababisha matatizo mbalimbali kama magonjwa, ajali, mauti, mikosi, au kukataliwa katika maisha.

Wakati mwingine huunda viumbe wa kichawi kama wanyama au hata watu kwa madhumuni yao ya kichawi.

Mara nyingi wachawi hutengeneza matatizo juu ya mtu, na mtu huyo huona kana kwamba ni matatizo ya kawaida, bila kujua kwamba nyuma yake kuna nguvu za kichawi zinatenda kazi. Wakati mwingine matatizo hayo yanaweza kusababisha kifo, na baada ya hapo mtu huyo kudaiwa kufanywa mtumwa wa kiroho au msukule kwa ajili ya kuwahudumia wachawi.

Mchawi ni nani?

Mchawi ni mtu anayehusishwa na nguvu za giza, na hutumika na shetani kwa lengo la kuwatesa au kuwadhuru watu. Sifa kubwa ya wachawi wanaweza kutambua nyota ya mtu na kujua hatima au mafanikio yake ya baadaye. Katika Biblia pia kuna simulizi kuhusu mamajusi waliotambua nyota ya kuzaliwa kwa Yesu. Sifa nyingine ya wachawi wanaweza kuingilia nyota ya mtu na kuitumia kwa manufaa ya watu wengine.

Wengine huamini kuwa mafanikio ya maisha ya mtu yanahusishwa na nyota yake. Hivyo kuna watu ambao hawajasoma sana lakini wamefanikiwa maishani, na wengine husema kwamba mafanikio hayo yanahusishwa na nyota yao, si tu elimu waliyonayo.

Katika biblia kuna mfano unaoonyesha jinsi mtu anaweza kufungwa au kuzuiwa na nguvu za kiroho kwa muda mrefu. Wachawi wanaweza kuweka kile kinachoitwa mipaka au “fensi” za kichawi, ambazo humzuia mtu kufikia maeneo au hatua fulani katika maisha yake. Mara nyingi mtu akitafuta suluhisho, huenda kwa mganga wa kienyeji bila kujua waganga nao ni wachawi.

Njia mojawapo inayofundishwa katika imani ya Kikristo ya kupambana na nguvu za giza ni kwa kumwomba Mungu na kutaja jina la Yesu. Kulitaja jina la Yesu kuna nguvu ya kuvunja mamlaka ya nguvu za giza.

Chanzo kikuu cha matatizo mengi ya kiroho hutokana na dhambi. Shetani hupata nafasi ya kumtesa mtu pale anapokuwa katika hali ya dhambi.

Njia za kujikinga na nguvu hizo ni pamoja na:

i. Kuondoa dhambi ya asili
Dhambi ya asili ilianza tangu wakati wa Adamu na Hawa. Ili mtu ajikinge dhidi ya nguvu za shetani, anatakiwa kutubu dhambi zake na kumwomba Mungu msamaha.

ii. Kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako
Mtu anapomkubali Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake,hupata faida mbalimbali za kiroho, zikiwemo:

a.    a.  Jina lake kufutwa katika kitabu cha hukumu na kuandikwa katika kitabu cha uzima wa milele.

b.    b.   Mungu kuwa Baba yake (Mwana wa Mungu).

c.     c.  Wachawi hawatakuroga tena.

d.    d.  Utapata ulinzi wa Mungu

 

 

Post a Comment

0 Comments