UFUFUO NA UZIMA
CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 08.02.2026
ASKOFU DKT GERSHOM
MWAKILA
SOMO: TATIZO NDANI YA TATIZO
![]() |
Mtu anapokuwa na tatizo,
asipokubali uwepo wa tatizo hilo, linaweza kuzaa tatizo lingine kubwa zaidi.
Mfano wake ni Adamu na Hawa. Walipokula tunda walilokatazwa na Mungu, na
walipohojiwa hawakukubali makosa yao bali walianza kujitetea. Kutokana na kosa hilo,
walijificha mbali na uso wa Mungu, jambo lililosababisha laana juu yao. Hii
inaonesha kuwa kutokukubali kosa ni chanzo cha matatizo makubwa zaidi.
kasema, Nalisikia sauti yako
bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha. Akasema, Ni nani
aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza
usiyale? Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye
aliyenipa matunda ya mti huo, nikala. 13BWANA Mungu akamwambia mwanamke,
Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala. BWANA
Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko
wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na
mavumbi utakula siku zote za maisha yako; Mwanzo 3:10-14
Kila mtu ana tatizo moja au
zaidi. Matatizo yenyewe siyo shida kubwa sana; bali maamuzi ya namna ya
kulishughulikia tatizo hilo ndiyo jambo la msingi. Maamuzi hayo huamua kama
tatizo litapata suluhisho au litazaa tatizo jingine.
Katika matatizo yako, Mungu
anaweza kukuonesha njia na kukupa maelekezo ya jinsi ya kulitatua. Hata hivyo,
uamuzi wa kutekeleza au kutotekeleza unabaki kuwa wa kwako.
Katika Biblia, Kaini alitoa
sadaka ya mazao yasiyompendeza Mungu, na Mungu hakuipokea sadaka yake. Mungu
akamwonya kwa kumwambia, “Dhambi inakuotea mlangoni; yapasa uishinde.” Lakini
Kaini hakuitii sauti ya Mungu. Matokeo yake, tatizo hilo likazaa tatizo jingine
kubwa zaidi la kumuua ndugu yake Abeli, na baadaye akasema uongo mbele za
Mungu. Hivyo, tatizo lisipotatuliwa kwa mwongozo wa Mungu, huzalisha matatizo
mengine makubwa zaidi.
“Kama ukitenda vyema, hutapata
kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe,
walakini yapasa uishinde.” Mwanzo 4:7
Nyuma ya kila tatizo la mtu kuna
chanzo chake. Laana ni maneno mabaya anayosemewa mtu, iwe ni kutoka kwa mtu
mwingine au kama hukumu ya Mungu. Vivyo hivyo, baraka ni maneno mema
anayosemewa mtu na Mungu au mtu mwenye mamlaka ya kiroho. Baraka humfanya mtu
astawi na kumiliki.
Laana halali huwa na madhara
makubwa, na inaweza kusababisha umasikini, mauti, kukataliwa, magonjwa, pamoja
na kupata na kupoteza mara kwa mara.
Moja ya sababu zinazoweza
kumfanya mtu asifanikiwe ni athari ya maneno mabaya aliyotamkiwa. Maneno yana
uzito wa kiroho, hivyo ili kushughulikia maneno ni lazima kushughulikia kwa
njia ya rohoni. Watu wengi huamini katika uchawi kwa sababu wanaamini kuwa uchawi
unafanya kazi katika ulimwengu wa roho. Shetani anapotaka mtu asipone au
asifunguliwe, huteteresha imani yake ili asiweze kuamini katika nguvu za Mungu.
Mungu amemuumba mwanadamu
ategemee msaada kutoka katika ulimwengu wa roho. Roho ikiwa katika hali njema,
mambo mengine ya maisha kama biashara, afya na ustawi pia huenda vizuri.
Hata hivyo, Mungu anahitaji
uamuzi wako ili aweze kukutendea. Maamuzi yako ndiyo huamua tatizo lako
litapata tiba gani. Ukichagua kumruhusu Mungu ashughulikie tatizo lako, utapata
uponyaji na ufumbuzi.
Kuamini uchawi na ushirikina
kunaweza kumwingiza mtu katika vifungo na laana. Laana inaweza kusababisha
kushindwa kumiliki, kutostawi, kutofanikiwa, pamoja na kupata magonjwa na
mikosi. Ni muhimu kuacha kutegemea uchawi na unganga, na badala yake kumtegemea
Mungu, ili upate baraka katika kila eneo la maisha yako.


0 Comments