google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MASHIMO YA KICHAWI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 01.03.2026
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: MASHIMO YA KICHAWI  



“Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” Ufunuo 21:8

Mashimo ya kichawi ni ya rohoni, yaani hayawezi kuonekana kwa macho ya kawaida lakini yapo na ni halisi.

Shetani huwa haumbi chochote ila anaiba vitu vya Mungu nakuvitumia kwa uharibifu. Watu huwa na vipaji mbalimbali ambavyo Mungu huwapa ili wamtumikie, lakini Shetani anaweza kumchukua huyo mtu nakutumia vipaji vyake kwa uharibifu. Hivyo watu hao ni watu ambao wameibiwa na wanatumia vipaji vyao kwa kazi ya Shetani.

“Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.” Isaya 42:22

Kuna matatizo mtu anayapitia kwenye maisha yake, ila ni kwa sababu vitu vyake vina milikiwa na shetani. Kuna mtu anapata magonjwa ya moyo kumbe wachawi wanautumia moyo wake kwa ajili ya kazi zao. Kuna mtu mtu ni tasa ila kumbe wachawi wanatumia tumbo lake la uzazi kwaajili ya kuzalisha katika ulimwengu wa kichawi.

“Tazama, hayo yote ni Mungu anayeyafanya, Mara mbili, naam, hata mara tatu, kwa mtu, Ili kurudisha roho yake itoke shimoni, Ili atiwe mwanga kwa mwanga wa walio hai.” Ayubu 33:29-30

Ili uweze kufanya vita na wachawi ni lazima upigane ukiwa rohoni. Unapoomba unakuwa upo katika ulimwengu wa roho, nawe unakuwa unapigana vita na wachawi hao na kuwaokoa watu watu waliotekwa.

“Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” Waefeso 6:12

Kuongezeka au kupungua inategemea na watu unaoambatana nao. Ukiwa unawatu wenye tabia ya uovu, basi baada ya muda utakuwa muovu. Lakini kama umejizungushia watu wenye tabia njema na wana nguvu na wewe utakuwa na tabia njema. Ukiwa mwenye nguvu ukajizungushia wenye nguvu nawe utakuwa Jabali. Ukiwa mwenye nguvu ukajizungushia wenye udhaifu nawe utakuwa dhaifu.

NAFSI ILIYOIBIWA.

Mtu anaweza kuibiwa nafsi, na nafsi yake ikawekwa kwenye mashimo. Ndani ya nafsi ya mtu kuna mambo manne yanayounda nafsi ya mtu. Mambo hayo ni:

a)  i.  Nia

b)   ii. Utashi

c) iii.   Hisia

d)iv.    Kumbukumbu

 

Wachawi wanaona kilichopo ndani ya nafsi ya mtu, nao wanakiiba na kukitumia kwaajili ya kazi zao. Kuna mtu ndani yake amewekewa utashi na Mungu, wachawi wanaiba ule utashi wa mtu huyo na kutumia kwa ajili ya kazi zao za kichawi. Kuna mtu anatumia utashi wako kichawi na anafanikiwa.

Nafsi ya mtu inaweza kuchukuliwa kichawi, alafu wachawi wakatumia nafsi ya mtu huyo kumfanikisha mtu mwingine.

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI                                                                                                                                                                             





Post a Comment

0 Comments