UFUFUO NA UZIMA
CATHEDRAL
IBADA YA PASAKA 19.04.2026
ASKOFU DKT GERSHOM
MWAKILA
SOMO: MATUKIO YA
KICHAWI NA MASHETANI KATIKA UZAO WA WANADAMU
![]() |
“Kulikuwa na vita mbinguni;
Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao
pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana
tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye
Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika
zake wakatupwa pamoja naye.” Ufunuo 12:7-9
Joka pia huitwa ibilisi au shetani audanganyae
ulimwengu wote. Shetani ni Malaika wasioilinda enzi yao (Yuda 1:6);
ni Malaika waliokosa wakatupwa na wamewekewa mipaka (2 Petro 2:4).
Malaika hawa hufahamika pia kama Ibilisi na Malaika zake (Mathayo 25:41).
Wapo Malaika wa Mungu na Malaika wa Shetani. Malaika
wa Shetani ni Malaika wa giza ambao ni mawakala wa matatizo kwa wanadamu. Kila
tukio alipatalo mtu, limesababishwa na malaika; kama ni tukio zuri,
limesababishwa na Malaika wa nuru, na kama ni tukio baya, limesababishwa na
Malaika wa giza.
Wakati mwingine Shetani hujifanya kama Malaika wa
nuru ili afanikishe kusudi lake. Shetani anautaalamu wa kujigeuza awe kama
malaika wa Nuru. Kuna watu wengi wameharibikiwa kwasababu ya shetani
kuwapotosha kwa matendo na njia zionekanazo machoni kama njia za nuru lakini
mwishoni watu hao wanaharibikiwa. Mfano, tukio hufuata mtu, naye akadhani ni
jambo jema kwake liletalo nuru lakini mwisho wa jambo hilo ni mbaya. Shetani ni
mwenye hila anayejua namna ya kutumia hila zake.
“Wala
si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi
si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki,
ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.”2 Wakorintho 11:14-15,
na pia katika
kitabu cha m Mithali 16:25, Ayubu 2:1, na Waefeso 6:11
Malaika wote wanatabia zinazofanana; -
i.
Malaika
wanaweza wakatokea ghafla na kupotea ghafla.
Malaika wa Mungu wanauwezo wa
kuonekana na kupotea hapo hapo hata kama kuna ulinzi mkali, mfano, kuna mageti,
mbwa, masai; ulinzi wa namna hii hauwazui. Mashetani huingia bila kizuizi
chochote na kuleta uharibifu kwa mtu.
Yupo atulindaye, naye tunamhitaji
wakati wote - Zaburi 121.
ii.
Malaika
wanaweza kuvaa umbo lolote.
Malaika wanaweza kuwa mti,
wadudu, mtu, kitu, au chochote sawasawa na uhitaji wa siku hiyo.
iii.
Malaika
hawatendi kazi mpaka wawe wametumwa.
Malaika ni roho watumikao ambao
wanasubiri kuagizwa na kwenda kule waagizwapo; hii ni kwa Malaika wa Bwana na mashetani.
Mtu mwenye kuurithi wokovu anayo mamlaka ya kuwatuma Malaika. Wachawi pia
huwatuma mashetani.
Mfano1; Malaika wa Bwana walitumwa kwa
Yusufu kuhusu mkewe Mariamu kuwa atachukua mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu “Kuzaliwa
kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na
Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho
Mtakatifu. Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake
kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri. Basi alipokuwa akifikiri hayo,
tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa
Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho
Mtakatifu.” Mathayo 1:18-20
Mfano2: Daniel alitokewa na Malaika
Gabrieli katika ndoto (Daniel 9:20-27).
Malaika wa Mungu wanatumwa na Mungu na watumishi
wake, vivyo hivyo, Malaika wa giza wanatumwa na Shetani na watumishi wake
“Je! Yuko malaika aliyemwambia
wakati wo wote,Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya
nyayo zako? Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale
watakaourithi wokovu?” Waebrania 1:13-14.
Yupo Mungu atutiaye nguvu tuwapo katika dhiki; Yesu
alitiwa na nguvu alipokuwa kwenye dhiki. Mungu hutuma Malaika zake.
Mungu huketi katika sifa. Wana wa Mungu humsifu
Mungu kwa nyimbo za sifa ili ashuke kuwahudumia. Shetani naye hutukuzwa na
watumishi wake katika kazi zao na mashetani hupanda ili kutoa huduma ya
kishetani. Ukimuona mganga wa kienyeji, mchawi, mpiga mafundo na wengine wa
aina hiyo, ujue hao wanafanya kazi ya shetani.
Wana wa Mungu hutumia Neno la Mungu pekee lenye nguvu
kumuhudumia kila mtu sawasawa na shida yake. Mara tu litamkwapo Neno, Malaika
Mbinguni hushuka kuwahudumia wana wa Mungu
“Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu,
tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata
kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li
jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” Waebrania 4:12
Uzao wa wanadamu na uzao wa kishetani.
Kila aliyepo duniani ni ama amezaliwa na Mungu ama
amezaliwa na shetani, hivyo, kuna wana wa Mungu na wana wa shetani. Kuna namna
Mungu huongoza uzao wake, shetani pia. Kila mtu unayekutana naye, kula naye,
kukaa naye, kufanya naye kazi, kwenye biashara, kwenye ndoa, au maeneo yoyote,
ni ama mwana wa Mungu au mwana wa Ibilisi. Kanisani pia wapo wana wa Mungu na
wana wa ibilisi, na ndiyo maana wana wa Mungu tumedhihirishwa kuzivunja kazi za
Ibilisi
“atendaye dhambi ni wa Ibilisi;
kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu
alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.”1 Yohana 3:8.
Kila kilichozaliwa na Mungu ni Mungu na kila
kilichozaliwa na Ibilisi ni Ibilisi, kama vile kila kilichozaliwa na nyoka ni
nyoka na kilichozaliwa na mnyama ni mnyama. Uzao wa nyoka ni uzao wa kishetani.
Katika kitabu cha Mwanzo 3:14-15, Mungu aliweka uadui kati ya uzao
wa nyoka amba oni uzao wa kishetani, na uzao wa mwanamke ambao ni uzao wa Mungu.
Hii inatuonesha kuwa tangu mwanzo kuna uadui kati ya uzao wa Mungu na uzao wa
shetani na hata vizazi na vizazi. Uzao wa Mungu wana miili na wanaitwa wana wa
Mungu, na uzao wa shetani wana miili na wao wanaitwa wana wa Ibilisi.
Uzao wa mwanamke umepewa mamlaka ya kuponda kichwa
cha uzao wa nyoka. Hata hivyo hatupondi Kichwa cha nyoka kwa jinsi ya mwili;
tunampiga kwa silaha zenye uwezo katika Mungu
“Maana ingawa tunaenenda katika
mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si
za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha
mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na
tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; tena tukiwa tayari
kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia.”2 Wakorintho 10:3-6.
Kwa sababu hii, unapaswa, kama mwana wa Mungu,
kufyeka kwa mamlaka uliyopewa, kuponda kwa mamlaka uliyopewa, kung’oa kwa
mamlaka uliyopewa pando lolote lisilofaa; yampasa Mwana wa Mungu kutumia sauti
ya mamlaka.
Mathayo 12:34-37 inatuonesha jinsi Yesu
alivyoshangazwa kuona wana wa uzao wa nyoka wakiwa na muonekano tofauti na
wanenayo. Uzao wa nyoka umefanana kila kitu na baba yao; wananena kama baba
yao, asili ni kama baba yao, uongo nis awa na baba yao.
Ukiona mtu anakutendea ubaya ujue huyo ni wa uzao wa
nyoka, anaweza akawa kazini kwenu, nyumbani au sehemu yoyote. Mtu mwema katika
akiba njema hutoa mema, na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya. Uzao wa
nyoka hutoa mabaya, na uzao wa Mungu hutoa mema. Wana wa Mungu tumepewa mamlaka
juu ya uzao wa nyoka (Marko 16:17-18).
Mungu akizaa anaza Mungu, na kila kilichozaliwa na
Mungu huushinda ulimwengu. Mungu anakutambua kuwa wewe ni mwana wa pendo lake
na wewe ni mtoto wa Mungu. Wana wa Mungu ni uzao mteule ambao huushinda
ulimwengu (1 Yohana 5:4, 1Petro 2:9). Wana wa Mungu
wakitenda ni Mungu ametenda, wakisema ni Mungu amesema.
Siku zote utambulisho wetu kama wana wa Mungu
unapaswa kuwa wazi na Dhahiri kuwa sisi ni wana wa Mungu (1 Yohana 3:1).
Kwenye Biblia, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake namna ya kuomba ambayo inawatambulisha
wazi kuwa wao ni wana wa Mungu; “Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako uje”. Uhusiano wetu na Mungu ni wa Baba na wanaye (Wagalatia
3:26, Yohana 1:12).
Ushetani unatokea sana mahali ambapo pana wivu.
shetani amehama kutoka kuwa pepo na sasa yupo kwenye hatua ya kuwa mtu. Shetani
ana uwezo wa kuingia ndani ya mtu na kumfanya mtu aweze kufanya jambo la
kishetani. Wapo watu ambao ukikutana nao na mambo wanayoyatenda ni Ibilisi
kabisa (Yohana 8:44).
Kila mmoja hubeba kiu ya baba yake. Wana wa Mungu
tumebeba kiu ya Baba Yetu, ambayo ni kufungua watu, kusaidia watu, kuombea
watu, n.k; wana wa Ibilisi wamebeba kiu ya baba yao. Wana wa Mungu tunaye Roho
wa Baba yetu asemaye ndani yetu (Mathayo 10:19-20).
Uwezo wa Malaika kuwa Mtu.
Kama tulivyoona hapo mwanzo, Malaika wana uwezo wa kujigeuza
kuwa kitu chochote au hali yoyote ili kutimiza lengo Fulani (Waebrania
1:7).
- Malaika aweza kuwa maji na
kusababisha maafa (Ufunuo 16:5),
- Malaika aweza kuwa moto na
kusababisha maafa ya moto (Ufunuo 14:18),
Mfano wa
maafa ni 1 Wafalme 18:38 (Eliya).
Kwakuwa Malaika aweza kuwa kama ilivyoelezwa,
Malaika aweza pia kuwa mtu.
Mwanzo 18:1- ; -
- Bwana kamtokea Ibrahimu.
- Ibrahimu mbele ya macho yake
anaona watu watatu.
- Ibrahimu aliwakaribisha nyumbani
mwake, wakanawa miguu na wakala chakula.
- Ni malaika ambao wana tabia zote
alizonazo mtu wa kawaida.
Bwana anaongea na sisi kila siku akiwa ndani ya mtu/watu.
Sisi tunaona mtu/watu lakini ni Bwana.
Mwanzo 19:1- ; -
- Malaika wawili nyumbani kwa Lutu.
- Lutu aliwakaribisha saw ana
walivyokaribishwa na Ibrahimu.
- Walinawa miguu yao na walikula
chakula.
- Wenyeji wa Sodoma waliwaona kuwa
ni watu na kutaka kuwatendea ubaya.
- Wanaonekana ni watu machoni pa
watu lakini wana matukio ya kipekee, Mfano; walinyoosha mkono watu wakawa
vipofu.
Malaika wanaweza wakaoa na kuolewa kwasababu wanaweza
wakawa Binadamu. Kuna watu upo karibu nao na kuonekana ni wema sana na wakarimu,
na kama ni rafiki au mchumba wako ila kumbe sio binadamu ila kumbe ni malaika.
Wakikutendea mabaya ni Malaika wa giza waliovaa umbo la binadamu, na
wakikutendea wema ni Malaika wa nuru waliovaa umbo la binadamu.
Wapo wajumbe wa Mungu huja kwenye maisha yetu kama
watu wa kutushika mkono kututoa kwenye dhiki ili kutupeleka sehemu sahihi,
lakini wapo hukataa kushikwa mkono. Mfano ni mke wa Lutu; hata aliposhikwa
mkono na wale Malaika aligeuka nyuma na kuwa jiwe la chumvi (Mwanzo 19:16,
26).
Yoshua 5:13 ; -
- Mungu alituma askari wa
mbinguni/Malaika akiwa na upanga ambayo ni silaha; ni kwa sababu Yoshua alikuwa
vitani.
- Malaika wa Mungu hututokea ili kutusaidia
kwenye matukio yetu. Hututokea kama watu wa aina fulani inayoendana na hali au
tatizo lililopo; kama biashara, huja kwa sura ya biashara
“Yakobo akakaa peke yake; na mtu
mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri.” Mwanzo 32:24
Malaika wanapokutana na Mtu humuachia alama au tukio
fulani; hata kwa malaika wa kuzimu na wao wanatumia njia hiyo ya kusababisha
alama za matatizo juu ya watu wa Mungu na lengo ni kuwazuia wasiende kule ambako
Mungu amewakusudia waende.
- Yakobo alishindana na Malaika
aliyekuja kama mtu.
- Malaika alimgusa Yakobo kwenye
uvungu wa paja ili ateguke amwachie; Yakobo aliumia na kumwachia malaika.
Mtu huwa na udhaifu uliosababishwa na jambo la
Malaika lakini Malaika wa giza hupofusha watu wasiweze kuona udhaifu huo.
Malaika wa Giza na Matukio ya Kichawi.
Mwanzo 32:1-2
Zaburi 78:47-49 – Kundi la Malaika waletao mabaya. Kila ubaya,
hasara, huzuni, au mabaya yoyote yanaletwa na Malaika wa giza, mfano, mvua yam
awe iliyoua ng’ombe.
2 Samweli 24:15 – Mwalaika mwenye kuwaharibu watu. Yupo katika sura ya
mtu. Alinyoosha mkono wakafa watu elfu sabini.
Daudi alimuona Malaika; Malaika akivaa umbo la mtu
anaonekana. Yapo magonjwa au hali Fulani mbaya katika maisha yanasababishwa na
watu. Mfano, Malaika waletano mabaya huweka mipaka kwenye elimu, umasikini,
umri wa kuishi n.k. Ni mtu kabisa anakutamkia maneno ya uharibifu ila nyuma
yake kuna mjumbe/wajumbe wa uharibifu.
Mabaya yanatokana Kundi la malaika wa kuzimu, kila tatizo
linalokuja kuna malaika wanaoleta mabaya juu ya mtu na wamevaa sura ya
binadamu. Chanzo cha Ugonjwa kinatokana na malaika mmoja na kila atakaye pata
Ugonjwa huo wanakuwa na tabia zinazofanana.
Mungu alishafanya maisha yetu yafanikiwe kabla
hatujazaliwa. Yeye anatujua zaidi ya tunavyojijua. Wana wa Ibilisi wapo
kutuharibia kila kitu lakini bado Mungu anatusaidia.
Ili Mungu akusaidie, ni sharti uwe mtoto wake.
Ukizaliwa na Mungu unaushinda ulimwengu (1 Yohana 5:4). Ukimkiri
Yesu unakuwa umezaliwa mara ya pili. Tukiwa wana wa Mungu tu tunaruhusa ya
kuzivunja kazi za Ibilisi.


0 Comments