UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 10.05.2026
ASKOFU DKT GERSHOM MWAKILA
SOMO: KUBOMOA MADHABAHU ZA MATESO
Madhabahu
hutumika kuimarisha ama kudhoofisha jambo fulani kwenye maisha ya mtu. Yapo
mateso katika maisha ya mtu ambayo yanasababishwa na madhabahu za kishetani.
Madhabahu ikibomoka mateso katika maisha yako yanaondoka. Neno madhabahu
limeandikwa mara 363 kwenye biblia. Kuna madhabahu ya Mungu ambayo watu wa
Mungu huiendea, lakini pia kuna madhabahu ya Shetani ambayo watu wa shetani
huiendea.
“Kwa
kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa
kadiri ya wingi wa huruma zake. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala
kuwahuzunisha.” Maombolezo 3:3
MADHABAHU
NI NINI?
1.
Madhabahu ni mahali ambapo ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili unakutana.
Ulimwengu wa roho una pande mbili, ambazo ni ulimwengu wa nuru na ulimwengu wa
giza.
2.
Madhabahu ni mahali ambapo viumbe kutokea rohoni hupewa ruhusa kutenda kazi
katika ulimwengu wa mwili. Madhabahu ina ruhusu viumbe wa
rohoni kutenda kazi mwilini.
“Na
makutano yote ya watu walikuwa wakisali nje saa ya kufukiza uvumba. Akatokewa
na malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia.”
Luka1:10
3.
Madhabahu ni mahali ambapo maagano yanafanyika na yanaimarika.
Mfano, maagano ya ndoa huanzia madhabahuni. Na ili maagano ya ndoa yavunjike,
ni lazima iwepo na madhabahu nyingine itakayo husika.
Maagano
ni kama mkataba kati ya mtu na mtu. Mfano, ukiingika makataba wa kupanga kwenye
nyumba fulani na mkataba ukisainiwa, mwenye nyumba hawezi tena kuingia kwenye
hiyo nyumba bila ruhusa ya mpangaji. Ndivyo hivyo kwa Mungu na wanadamu, ili
yeye kuja katika maisha yako ni kupitia wewe kumkaribisha Yesu aingie ndani.
Ndiomaana mtu akitaka kuokoka huenda madhabahuni kwaajili ya kuweka agano la
wokovu na Mungu.
4.
Madhabahu ni daraja kutoka kwenye
ulimwengu wa mwili kwenda kwenye ulimwengu wa roho na kutoka kwenye ulimwengu
wa roho kwenda kwenye ulimwengu a mwili.
MADHABAHU
NA SADAKA
Kila
madhabahu inahitaji sadaka. Sadaka ni njia ambayo mtu anaweza kuitumia
kujiungamanisha na madhabahu fulani. Kwa kila agano ambalo Mungu hufanya na
watu wake, hujenga madhabahu na kuagiza sadaka itolewe kwenye madhabahu hiyo
ili kujiungamanisha na agano hilo.
Nuhu
baada ya gharika kuisha, aliposhuka kwenye safina alijenga madhabahu na kuweka
sadaka juu yake ili kufanya agano na Bwana. Unapotoa sadaka katika madhabahu
fulani, unajiungamanisha na agano la madhabahu hiyo. Hivyo ukifanya agano
katika madhabahu ya Mungu, Mungu anashuka na kuhusika na maisha yako katika
biashara, afya, ndoa na jambo lolote linalokuhusu.
Mungu
ni mwaminifu kwenye agano lake. Shida ya watu ni kwamba kama hana vitu
anamtumainia Bwana, ila akishapata vitu anamsahau aliyemwezesha kupata.
Anasahau kurudi mahali ambapo agano lilifanywa na linaimarishwa.
MADHABAHU
NA HALI YA MTU
Hali
yoyote uliyonayo imeachiwa kutoka kwenye madhabahu fulani, ama madhabahu ya
Mungu au ya Shetani. Mambo kama furaha, amani, ushindi, uaminifu, upendo na
mafanikio hutoka kwa Bwana. Mateso, shida, taabu, magonjwa hutoka kwenye
madhabahu za giza. Kila alichonacho mtu amepewa.
“Bwana akamtokea Abramu, akasema, Uzao
wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu Bwana aliyemtokea.” Mwanzo
12:7
Unavyokuwa
karibu na madhabahu ndivyo maagano yanaimarika zaidi. Madhabahuni ni mahali
amabapo kuna nguvu, na unavyokuwepo kwenye madhabahu ni kama unachaji na kuwa
na nguvu zaidi. Kuna mambo utahitaji fedha na mambo mengine utahitaji akili ya
kawaida ili kuyafanya, lakini yapo baadhi ya mambo huwezi kuyafanya bila nguvu
ya madhabahuni.
"Mwanzo
35:7"
Akajenga
huko madhabahu, akapaita mahali pale, El-Betheli; kwa sababu huko Mungu
alimtokea, hapo alipomkimbia ndugu yake.
AINA
YA MADHABAHU
Madhabahu
zipo za aina mbili kuna madhabahu za Mungu na madhabahu za kishetani. Madhabahu
za kishetani hufanya kazi kama madhabahu za Mungu isipokuwa tu, zenyewe hutenda
kazi katika uovu. Kwenye madhabahu za shetani kuna madhabahu zingine ndani
yake. Kuna madhabahu zinazohusika kuloga viongozi katika nchi na zingine kuloga
wananchi. Lakini pia kuna madhabahu za
hofu.
MADHABAHU
YA HOFU
Hofu
ni kinyume cha Imani. Mara nyingi kabla shetani hajaleta jambo lolote ovu,
hutanguliza hofu ili kuua imani. Hofu ni kuogopa hata kwenye mazingira ambayo
Mungu anatenda kazi. Silaha kubwa ya shetani ni mtu kuwa na hofu. Unaweza ukawa shujaa lakini ukaishi maisha ya
hofu.
Kama
una hofu, ni lazima kiwepo kitu kinachokufanya uwe na hofu. Yawezekana kuna
jambo liliwahi kukupata ama kuna hali iliwahi kukukabili ambayo ikazaa hofu
ndani yako. Madhabahu za Bwana humfanya aliye na hofu akawa shujaa, aliye
maskini akawa tajiri.
Ukiona
mambo yako hayaendi sawa, iko madhabahu amabayo inahusika. Ukiwa na hofu hata
mahali penye fursa utaogopa. Ukiwa na hofu hata mahali penye ajira utaogopa.
Kuna madhabahu ambazo huzuia watu wasipate ajira au nafasi au cheo. Zipo
madhabahu za hofu ambazo huipa nchi hofu.
Bwana
akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni
na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.” Hesabu 12:5
Zipo madhabahu zinazozuia viongozi wasitoke kwenye mkoa fulani. Ziko madhabahu zinazozuia mtu asifike kwenye hatima yake. Kuna madhabahu zinazui watu wasiwe na afya njema. Kuna mdhabahu zilizojengwa kwenye taifa kuzui maendeleo katika nchi. Kuna madhabahu zinazolaza watu ambapo watu huwaza katika kiwango cha chini. Zinawafanya watu wasihoji mambo muhimu katika nchi. Na ili uweze kupata, ni lazima madhabahu hizo zivunjwe.
MAOMBI
YA KUVUNJA MADHABAHU
“Kwa
jina la yesu kwanzia sasa naziendea madhabahu zote za hofu zilizojengwa
kuharibu maisha yangu kwa jina la Yesu, madhabahu za hofu zilizojengwa kuharibu
afya yangu, madhabahu za hofu zilizojegwa kuharibu kazi yangu kwa jina la Yesu
ninaziendea kwa damu ya Yesu. Madhabahu zote za hofu maala popote zilipojengwa
kwa jina la Yesu ninaziendea kwa mkono wa Bwana nazivunja,nazivunja nazibomoa kwa jina Yesu kama ambavyo Gidioni
alivyoambiwa akabomoe madhabahu ya Bahari na mimi leo nimeambiwa nikabomoe
madhabahu za kishetani zenye kutia hofu kwa Jina la Yesu mahala popote kwenye
mkoa wangu au wilaya au kijiji au tarafa au nyumba ilipojengwa madhabahu ya
hofu kwa jina la Yesu ninakwenda naibomoa kwa jina la yesu nnabomoa madhabahu
ya hofu nazibomoa leo kwa jina la Yesu” Amen

0 Comments